"Visit Tanzania" ya Simba SC ni nzuri lakini...

mikedean

JF-Expert Member
Mar 15, 2018
3,255
4,599
Ni suala la uzalendo na zuri kutangaza nchi ya Tanzania nje ya Tanzania. Timu ya Simba inapaswa kupewa heko kwa Hilo.

Simba itapata kutembelea nchi za Sudan, Misri na Kongo. Nchi hizi za kiafrika Zina ukaribu mkubwa na Tanzania isipokuwa Sudan. Hivyo wasudan watakumbuka kuwa Kuna nchi inaitwa Tanzania.

Jambo linalonitatiza ni kuingiza dili hilo bure kabisa. Hii sio nzuri, Simba ilipaswa kupata chochote. Angalau kingesaidia kuwapa motisha wachezaji Kama hela isingetumiwa na Simba SC. Kama ni uzalendo basi wangepunguza walau hata mil 200.ili iwasaidie hata kwa kulipia hotel.

Kwa sababu klabu ya Simba ni mali ya Mo Dewji Ndio maana sio ajabu wanafanya haya. Ni kama Man City ya Sheikh Mansoor
Sidhani kama Man City kuingiza dili na Etihad inamaana Mansoor sio mzalendo Bali Ile ni biashara.Tunaposema mpira ni biashara,hii ilikuwa fursa ya kupata kuingiza mapato.

Mwenyekiti wa Simba ajaye anapaswa asiwe mtu wa kuburuzwa. Anapaswa awe ndiye msimamizi wa madili kama haya Ili Simba ya wanachama iwe na chochote.Yamkini Mo akawa Hana shida na hela hizo, ila Simba ya wanachama ambayo inasemekana Ina hisa 51% ambayo kwa Hakika ni asilimia hewa. Hizi Ndio pesa ambazo Simba ilipaswa kuwa nazo.

Leo Barbra ameingia huo mkataba kwa BARAKA za kaimu mwenyekiti au kwa BARAKA za Mwenyekiti wa Bodi? Narudia tena hili dili Halina maslahi kwa Simba. Ilipaswa mwenye hisa 51% Ndio awe na sauti. Sasa swali ni kuwa Barbra yuko kwa maslahi ya Simba ya Mo au Simba SC?

Sijaandika kwa nia mbaya au kuwa Simba wamekosea Ila nahisi serikali ilipaswa ichangie.simba inatumia uwanja wa taifa mechi moja ni Mil.4 na unatoa kabla ya mechi.Basi Simba nao wangepewa kutumia uwanja huu bure kwa mechi za nyumbani za CAF champions ligi Kama fadhila.

Kuchangiwa kwa hoja karibu
 
Simba sc si ya wanachama Tena Hilo liko wazi, hii ishakuwa Mali ya Moo full stop. Hao wanachama na hisa zao Ni geresha tu kutaka kuizuga serikali.
Vyura acheni kuwashwa nendeni nyie Wizara ya Utalii mkapewe Fedha kwa niaba ya Simba basi. Kuna watu wameteseka saaaana leo kwa Uzalendo wa Simba Lunyansi
 
Vyura acheni kuwashwa nendeni nyie Wizara ya Utalii mkapewe Fedha kwa niaba ya Simba basi. Kuna watu wameteseka saaaana leo kwa Uzalendo wa Simba Lunyansi
Nadhani wewe ndiyo unateseka kuliko maana si kwa povu Hilo. Kwani nolichodanganya nini hapo? Simba sc ya wanachama ipoo? Hizo 51% zipoo ?
 
Hiki ni kipindi cha transion tu, na pia lazima utafute mzamini ambaye hatoletewa kinyingo na sportpesa, kwa sababu sportpesa anamaamuzi ya hiyo nafasi kuliko simba, kimsingi hiyo nafasi imeshalipiwa na sportpesa hata kama imeondolewa logo yao.

Ni vyema hiyo nafasi tumeitumia kizalendo kuliko ilivyokuwa plain kama mwaka juzi. Kibiashara unajiuliza ingeleta picha gani kwa sportpesa waliotoa mabilioni kama simba ingewatafuta letsay vodacom?

Wakati mkataba wa sportpesa bado una run? Hayo ni mawazo yangu binafsi, yanaweza yakakosa uharisia pia.
 
Ni suala la uzalendo na zuri kutangaza nchi ya Tanzania nje ya Tanzania. Timu ya Simba inapaswa kupewa heko kwa Hilo...
Kwani simba wamesema huo mkataba ni bure tu simba itaitangaza Tanzania bila kulipwa chochote?

Shida tunabeba maneno ya kwenye vijiwe. Pili hoja zako za mwisho kuhusu nani wa kuhandle mikataba nahisi ujasoma vzr katiba ya simba, ungesoma usingeandika ulichoandika
 
Ni suala la uzalendo na zuri kutangaza nchi ya Tanzania nje ya Tanzania. Timu ya Simba inapaswa kupewa heko kwa Hilo...
Hata katika Makampuni makubwa yaliyojiorodhesha ktk masoko ya hisa Management inaamua kwa niaba ya Wanahisa ktk harakati zao za uendeshaji taasisi, maamuzi ya management yanaweza kugharimu taasisi au yaweza kuleta faida lakini wamepewa dhamana ya kuiendesha team.Hilo ni suala la kimanagement.
 
Kwenye taasisi yoyote kuna kurudisha kwa jamii nk. Katika hili Simba wanahitaji heko na makofi mengi wamefikiria zaidi nchi kuliko wao. Wangeweza kuamua ktk kipindi hiki watafute wadhamini tena kwa donge nono (madhalani $100,000) kwa kila game moja. Wangepiga mpunga ila wameamua kurudisha kwa jamii.

Tuache majungu tuwapongeze esp CEO. Ni wazo bora n zuri
 
Hujui lolote kuhusu mfumo wa hisa unavyofanya kazi, 51% ya wanachama ni kikundi cha watu wengi, mfumo wa hisa ni mtu sio watu mwenye hisa nyingi ndio anakua mwenyekiti wa bodi. Unaspeculate eti Barbara kapewa ruhusa na nani? Hivi mo au mwenyekiti wa Simba? Swali hili linaonyesha namna gani hujui mfumo wa uendeshwaji wa klabu.

Hao wote hawana mamlaka ya kutoa maamuzi yoyote, chombo chenye mamlaka hayo ni bodi ya wagurugenzi. Unaonyesha huoni faida ya kiuchumi Simba kuvaa Jezi hizo, Kwa kutumia jezi hizo Simba itakuza zaidi brand yake, mauzo ya jezi kutokana na logo ya visit Tanzania, na pia itatangaza utalii wa nchi yake, Simba ni ya Tanzania na wala si Burundi. Manufaa ya nchi yanatija kwa Simba pia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Simba sio wajinga kama mnavofikilia, kuna mipango ya muda mrefu na mipango ya muda mfupi, wanachokifanya simba ni mipango ya muda mrefu, wana zamilia kushiriki na kufika mbali michuano ya club bingwa kwa muda mrefu hivo kufanya hiyo advertisement bure lengo ni kujitangaza wao pia lakini pia kuusoma mchezo.

Watafatilia kama hiyo issue itafanikiwa kwa asilimia ngapi, na baada ya hapo ndipo serikali italazimika kuingia mkataba wa pesa na simba, ata serikali sio wajinga kuingia kichwa kichwa na kulipa pesa ikiwa michuano inafanyikia Africa na watalii asilimia kubwa wanatoka nje ya bara la Africa, kwahiyo hapa target ni kwa ambao watafilia michuano hii kwenye luninga hivo imekaa indirect way, kwa leo mtaona bure ni ujinga ila simba itakuja kupiga pesa badae.

Lakini pia simba wamewapa nafasi ya kujua wenye makampuni kama wanaweza kutangazwa Africa kupitia club bingwa, mfano next season kama simba watafanikiwa kufika huku tena inaweza kuingia mkataba wa pesa na serikali au kampuni ingine yoyote ambayo itataka kunufaika na simba mfano ORYX GAS. tatizo wabongo tunafikilia karibu sana, ni sawa na mhitimu wa chuo akiambiwa anza kufanya kazi kwa kujitolea anaona kama ni dharau kumbe anajipa nafasi ya kujitangaza.
 
Hujui lolote kuhusu mfumo wa hisa unavyofanya kazi, 51% ya wanachama ni kikundi cha watu wengi, mfumo wa hisa ni mtu sio watu mwenye hisa nyingi ndio anakua mwenyekiti wa bodi. Unaspeculate eti Barbara kapewa ruhusa na nani? ...
Neno tu visit Tanzania hiyo jezi itanunuliwa na ambao si wanasimba pia ,imekaa kizalendo

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Ni suala la uzalendo na zuri kutangaza nchi ya Tanzania nje ya Tanzania. Timu ya Simba inapaswa kupewa heko kwa Hilo...
Wewe uliskia wapi au ulikuwepo wakati wanasaini mkataba wakasema ni bure? Sasa kama ni bure wamesaini mkataba wa nini acha choko choko bwana wewe andaa yenu visit kidimbwi.
 
Hakuna ubunifu wowote, ujinga na utaahira tu, wagekuwa wabunifu wangetafuta maneno yanayo-deliver the same message lakini ambayo hayajatumiwa na nchi au mtu yoyote. Poor simba
 
Back
Top Bottom