Viongozi 2 wa IS wauawa Mosul, Iraq

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397

160609110418_iraq_mosul_5_640x360_bbc_nocredit.jpg

Viongozi wawili wakuu wa kundi la kigaidi la Islamic State waliuawa katika mashambulizi ya angani ya vikosi vya muungano vinavyoongozwa na Marekani, katika mji wa Mosul nchini Afghanistan mwezi ulopita.

Msemaji huyo anasema vikosi vya muungano vimeanza kuwafurusha wapiganaji hao katika eneo la kusini mwa Mosul.

Haya yanajiri baada ya vikosi hivyo kuchukua udhibiti wa mji wa Fallujah kutoka mikononi mwa IS. Shambulizi hilo la angani karibu na mji wa Mosul lilifanyika wiki ilopita.

160609104528_iraq_mosul_2_640x360_bbc_nocredit.jpg


Mosul ni mji wa pili kwa ukubwa nchini Iraq, na unasemekana kuwa ngome kuu ya islamic state.

Kulingana na Pentagon, makamanda wawili wakuu wa kundi hilo waliuawa akiwemo naibu waziri wa vita Basim Muhammad Ahmad , na kamanda mkuu wa kundi hilo Hatim Talib al-Hamduni.

Kwa sasa inaonekana lengo kuu la vikosi vya Iraq litakuwa kuchukua udhibiti wa mji wa Mosul.

Msemaji wa Pentagon anasema mauaji ya viongozi hao, pamoja na mashambulzi ya angani dhidi ya kundi hilo kwa kipindi cha mwezi mmoja uliopita, yameathiri pakubwa uongozi wa kundi hilo mjini Mosul.
Hii itatoa nafasi bora kwa vikosi vya Iraq kunyakua mji huo, kwa usaidizi wa muungano wa majeshi ya kimataifa.

Chanzo: BBC
 

Attachments

  • upload_2016-7-2_12-15-47.gif
    upload_2016-7-2_12-15-47.gif
    51 bytes · Views: 27
Nangoja siku itakapofika Nikiona neno ''IRAQ'' Basi zitahusu habari za shughuli za kiuchumi......#VITAMBAYASANA
 
Back
Top Bottom