Martoism
Member
- May 31, 2012
- 36
- 21
Mbunge wa Musoma Mjini mh , Nyerere anatarajiwa kufanya mikutano kwa siku mbili mfululizo jimbo la Isimani Mkoani Iringa. Mikutano hiyo itafanyika tar.11 na 12 Januari 2015 .
Pamoja na mambo mengine mikutano hiyo inabeba ujumbe wa kuwashukuru wananchi kwa kuichagua CHADEMA na kutoa elimu ya demokrasia kwa Umma dhidi ya ushiriki wa wananchi katika kura ya HAPANA kwa katiba Mpya na kujiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la wapiga kura.
Aidha Mwaliko huu umetokana na Makamu mkt wa BAVICHA Taifa Patrick Ole Sosopi ambaye atakuwa mwenyeji wa mh, Nyerere .
Ole Sosopi amekuwa akipata vitisho na ahadi za kutaja kuwa anahitaji kiasi gani cha fedha kutoka kwa Waziri wa Nchi Sera na Uratibu wa Bunge mh, William Vangimembe Lukuvi ili aweze kumwachia Jimbo la Isimani apite bila kupingwa.
Sosopi amekanusha vikali kutokuogopa vitisho hivyo na akaenda mbali zaidi kueleza kuwa kama huko nyuma Jimbo liliwahi kuuuzwa yeye hana bei na Wanaisimani wawe tayari kumchagua kwenye Uchaguzi mkuu ujao wa mwezi Octoba kwani yeye ni Kijana Mahiri Mweledi na Mzalendo kwa Taifa .
Lukuvi amenukuliwa maeneo mengi akisema kuwa Mbunge wa kumwondoa yenye Isimani bado hajazaliwa. Huku akiongea kwa hofu kubwa katika mkutano wake katika Kata ya Malengamakali (Mkulula) ambako amezaliwa Makamu mkt wa BAVICHA Taifa alimbeza kuwa hawezi kuwa Mbunge wa Isimani kwa kuwa hajawahi kuwa hata mkt wa Kitongoji.
"Mimi Nina vyeo vingi huko Serikalini , nlishawahi kuwa mkuu wa Wilaya na Mkoa sasa huyu kijana ( Sosopi) hata hajawahi kuwa mkt wa Kitongoji atauweza Ubunge ? " aliskika akihoji wananchi huku akizomewa kwa mayowe.
Pamoja na mambo mengine mikutano hiyo inabeba ujumbe wa kuwashukuru wananchi kwa kuichagua CHADEMA na kutoa elimu ya demokrasia kwa Umma dhidi ya ushiriki wa wananchi katika kura ya HAPANA kwa katiba Mpya na kujiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la wapiga kura.
Aidha Mwaliko huu umetokana na Makamu mkt wa BAVICHA Taifa Patrick Ole Sosopi ambaye atakuwa mwenyeji wa mh, Nyerere .
Ole Sosopi amekuwa akipata vitisho na ahadi za kutaja kuwa anahitaji kiasi gani cha fedha kutoka kwa Waziri wa Nchi Sera na Uratibu wa Bunge mh, William Vangimembe Lukuvi ili aweze kumwachia Jimbo la Isimani apite bila kupingwa.
Sosopi amekanusha vikali kutokuogopa vitisho hivyo na akaenda mbali zaidi kueleza kuwa kama huko nyuma Jimbo liliwahi kuuuzwa yeye hana bei na Wanaisimani wawe tayari kumchagua kwenye Uchaguzi mkuu ujao wa mwezi Octoba kwani yeye ni Kijana Mahiri Mweledi na Mzalendo kwa Taifa .
Lukuvi amenukuliwa maeneo mengi akisema kuwa Mbunge wa kumwondoa yenye Isimani bado hajazaliwa. Huku akiongea kwa hofu kubwa katika mkutano wake katika Kata ya Malengamakali (Mkulula) ambako amezaliwa Makamu mkt wa BAVICHA Taifa alimbeza kuwa hawezi kuwa Mbunge wa Isimani kwa kuwa hajawahi kuwa hata mkt wa Kitongoji.
"Mimi Nina vyeo vingi huko Serikalini , nlishawahi kuwa mkuu wa Wilaya na Mkoa sasa huyu kijana ( Sosopi) hata hajawahi kuwa mkt wa Kitongoji atauweza Ubunge ? " aliskika akihoji wananchi huku akizomewa kwa mayowe.