Atclkwanza
JF-Expert Member
- Dec 20, 2015
- 823
- 998
Wana JF,
Kuna nyumba nimepanga mitaa yaTabata usiku shida tupu, kukabwa kila siku, nikiamka asubuhi nakutwa nimechanjwa chale mgongoni, kifuani na kwenye mapaja karibu na yale mawe mawili.
Kilichoniogopesha hapa binti yangu usiku wa kuamkia jana amepigwa konzi ameamka analalamika kuwa kuna mtu kampiga konzi bila kumuona na anasikia kichwa kinauma.
Wife wangu ni mlokole sasa yeye ndo shida zaidi ila yeye kuchanjwa hachanjwi ila anaota wanamfukuza na mapanga au wanamtumbukiza kwenye shimo mara zote, huwa anawashida ila akikurupuka pressure inashuka anakuwa hoi.
Wakuu jana usiku nimechelewa kulala kidogo sasa mapaka yakawa yanalia dirishani kwangu kwa sauti ambazo siyo kama paka wa kawaida.
Nikatoa amri kwamba nawajua nyie siyo paka, cha kushangaza nikasikia filimbi ikipigwa hapo hapo dirishani kwangu nikaogopa sana, nikastahimili uoga usinishinde nikatoka nje ya nyumba yangu bila kukuta kitu ila nilihisi kama mtu nimepishana naye mangoni.
Hili suala linanitokea karibu kila siku hasa kuchanjwa chale usiku, ilibibidi nifuatilie historia ya nyumba kidogo ila jibu nililoambiwa na huyo mtu ni kwamba ilikaa bila mtu kwa muda wa miezi sita, nilijaribu kumuuliza ni kwanini ilikaa bila mtu wakati nyumba iko vizuri a kaniambia hajui.
Wakuu kwa sababu nyumba ni ya kupanga nitahama, nimeamua nilete maswaibu hapa ili kama kuna mtu yalishawahi kumsibu au anaidia na haya mambo naomba ushauri wake kwa maswali haya.
A)Kwanini nachanjwa mwilini?
B)Kule kuhisi kama mtu napishana naye halafu simuoni na hili limeekaaje na kuhusu mtoto wangu kupigwa konzi Je?
B)Na wife kukimbizwa na mapanga na kujaribu kumtumbukiza kwenye shimo hili nini?
N:B Kuna mama jirani akimuona mke wangu au mimi anatuogopa kabisa hata tukimsalimia anatuitikia bila kutuangalia usoni hapa ni hisia tu.
Kuna nyumba nimepanga mitaa yaTabata usiku shida tupu, kukabwa kila siku, nikiamka asubuhi nakutwa nimechanjwa chale mgongoni, kifuani na kwenye mapaja karibu na yale mawe mawili.
Kilichoniogopesha hapa binti yangu usiku wa kuamkia jana amepigwa konzi ameamka analalamika kuwa kuna mtu kampiga konzi bila kumuona na anasikia kichwa kinauma.
Wife wangu ni mlokole sasa yeye ndo shida zaidi ila yeye kuchanjwa hachanjwi ila anaota wanamfukuza na mapanga au wanamtumbukiza kwenye shimo mara zote, huwa anawashida ila akikurupuka pressure inashuka anakuwa hoi.
Wakuu jana usiku nimechelewa kulala kidogo sasa mapaka yakawa yanalia dirishani kwangu kwa sauti ambazo siyo kama paka wa kawaida.
Nikatoa amri kwamba nawajua nyie siyo paka, cha kushangaza nikasikia filimbi ikipigwa hapo hapo dirishani kwangu nikaogopa sana, nikastahimili uoga usinishinde nikatoka nje ya nyumba yangu bila kukuta kitu ila nilihisi kama mtu nimepishana naye mangoni.
Hili suala linanitokea karibu kila siku hasa kuchanjwa chale usiku, ilibibidi nifuatilie historia ya nyumba kidogo ila jibu nililoambiwa na huyo mtu ni kwamba ilikaa bila mtu kwa muda wa miezi sita, nilijaribu kumuuliza ni kwanini ilikaa bila mtu wakati nyumba iko vizuri a kaniambia hajui.
Wakuu kwa sababu nyumba ni ya kupanga nitahama, nimeamua nilete maswaibu hapa ili kama kuna mtu yalishawahi kumsibu au anaidia na haya mambo naomba ushauri wake kwa maswali haya.
A)Kwanini nachanjwa mwilini?
B)Kule kuhisi kama mtu napishana naye halafu simuoni na hili limeekaaje na kuhusu mtoto wangu kupigwa konzi Je?
B)Na wife kukimbizwa na mapanga na kujaribu kumtumbukiza kwenye shimo hili nini?
N:B Kuna mama jirani akimuona mke wangu au mimi anatuogopa kabisa hata tukimsalimia anatuitikia bila kutuangalia usoni hapa ni hisia tu.