Chapa Nalo Jr
JF-Expert Member
- Dec 8, 2010
- 7,521
- 6,517
Wewe mleta mada hapa ni muhuni tu. Na huenda hili la safari limekugusa au umetumwa na mtu ambaye ameguswa na safari hizi kudhibitiwa. Hapa Magufuli kagonga msumali mahala penyewe. Kuna watu wamepewa ofisi lakini hawazifanyii kazi zaidi ya wao wenyewe kujaribu kufuatilia ni wapi na lini itatokea safari ya kwenda nje ya nchi. Hili hali hitaji utafiti. Toa sababu za kwenda nje ya nchi na eleza ni faida gani nchi itapata kwa safari yako. Heshima ya mabalozi ilipotea kabisa baada ya Kikwete kuwawakilisha wao kwenye kila jambo hata lile la kwenda kutazama jinsi ya kutengeneza soseji za nguruwe. Tena hii thread inatakiwa kufutwa mara moja kwani ina katisha tamaa na kutaka kumvuruga Rais kwa maamuzi sahihi.
Mleta mada katoa toka gazeti mwananchi. Ila kwa kweli hili agizo limesababisha na mengine yote kuhusu fadha yawe shida huku serikalini.