Vijana wazelendo vyuo vikuu wamshukia Mbowe

Vijana wazelendo vyuo vikuu wamshukia Mbowe

Sawa kabisa. Hata hivyo kwa maoni yangu naona kama maandamano hayana mantiki, afterall kipindi chenyewe cha bunge kinaenda mwishoni na watu wameshalamba na wanaendelea kulamba mamilioni yao. Hata watu wakiandamana, hiyo pesa waliyochukua itarudi? Wapange hoja nyingine, hiyo itawaumiza wananchi walalahoi wenzangu bure tu.
Mm nadhani kila mtu anayo haki ya kutoa maoni yake humu jf, shindaneni kwa hoja sio kwa matusi, kulazimisha wengine wakubaliane na mtazamo wako sio sahihi sana ,toa hoja ijadiliwe
 
ni nyinyi wanafunzi ambao huwa mnaandamana kutaka pesa za kujikimu au ni nyinyi mkiishiwa huwa mnaenda kujiuza mpate chochote cha kula?? majibu tafadhari
 
We we umetumwa mpumbavu mkubwa tulikutana wapi tukamlaani KAMANDA MBOWE?una uzalendo gani we we na ninani we we ktk nchi hii?elimu gani uliyonayo ya yeboyebo ?
 
Vijana wenye njaa mbaya! mnatamani kuendeleza ufisadi wa kiccm, mlaaniwe.
 
Tujitahidi kujenga hoja na zijadiliwe kwa weledi kwa manufaa ya taifa,tusipende kushabikiwa kwa kila kitu.Ukiona mwenzio kAjibu kwa mtazamo wake ambao haukufurahishi ni bora ukakaa kimya kuliko kutukana.
Nakatiza zangu tu!
 
Wewe ulie_post ii acha utumwa aseee afu io umoja wa vijana wa elimu cjui ya vyuo vikuu umetoka wap acheni kutumika kisiasa
 
Usituhusishe wanachuo wote kwenye sifa za kijinga,kama umetumwa uwe wazi
 
Kama kweli taarifa hii imeandaliwa na wasomi wa vyuo vikuu, basi tuna hali mbaya na tunahitaji uongozi mpya ili kufanya marekekebisho makubwa kwenye mitaala yetu ya elimu.
Kwa wasomi wanaofikiri na kutoa kauli kama hizi kwa pamoja lazima viongozi walioko madarakani kupitia chama cha Mapinduzi waseme kuwa mfumo wetu wa elimu ni bora kana wanavyosema sasa.
Poleni wasomi wetu maana huo nao ni mtazamo na hasa kama ulikuwa na njaa na ukapewa chakula na mchawi au mtu mbaya lazima utamtete kuwa ni mtu mzuri.
Hapa ndipo tulipofikia.
" No rational decission on a crucial matters"
 
Nasoma chuo kikuu, mimi si mmoja wenu. Nashukuru kwa kutokitaja chuo changu maana hatufugi pumba za hivi.

Huu umoja umesajiliwa wapi?
Ninyi ni akina nani kwa majina?
Vyuo vikuu watu husoma hata ngazi ya cheti, ninyi mpo ngazi gani?
Nani kawakusanya, kusha kawaambia mtoe kauli hii kwa niaba ya wanavyuo bila ridhaa yetu kupitia serikali za wanafunzi?

Kama ni wasomi mseme vizuri, hivi huwa mnatoa matamko kuhusu hali ya uchumi wa nchi na ajira baada ya elimu yenu vyuoni?

Luther King Jr aliandamana bila kukata tamaa, hatukuambiwa aliandamana na familia yake bali watu waliomwunga mkono, ingawa damu yake ilimwagika lakini iliweka alama isiyofutika.

Watu wanakufa kwa njaa, magonjwa, vita vya ardhi n.k Hao damu zao hazijawauma ninyi wasomi njaa?
 
Back
Top Bottom