Da Vince Leofric
Member
- Oct 15, 2013
- 9
- 2
Imekua ni kawaida sana katika jamii yetu kuskia vioja vitokanavyo na mapenzi: mara utaskia "anywa sumu, ajinyonga" na mengineyo yanayochukiza ambayo hayaleti haiba nzuri kwa jamii haswa kwa vijana ambao ndio hasa msingi wa Tanzania yetu ya kesho... Nikiingia kwenye mzizi wa mada yangu hii, moja kwa moja naipeleka kwa vijana wa kiume. Ki ukweli matatizo mengi katika mahusiano hasa ya kimapenzi yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na tabia ya wanaume wengi ambao walijikuta wakiendeshwa na hisia na mihemko yao ya kimwili ambayo ni ya mda mfupi, iliyopelekea kutumia mali walizokua nazo ambazo zinatamanika machoni pa wanawake wengi kwa lengo la kuwa nao kama wapenzi wao, huku wakijua fika kwamba hakukua na msingi wa mapenzi ya kweli ambayo hutoka rohoni. Hatima yake vijana wengi wakajikuta wakipanda penzi kwa wanawake wasiokua na mapenzi kwao, bali walikubalika kwa misingi ya pesa na vitu vionekanavyo kwa macho. Hatima yake ni kuporomoka kwa maadili ya jamii, uaminifu katika jamii umepotea, ndoa nyingi zinavunjika, vijana wengi wamepoteza hamasa ya kujenga familia sio kama zamani na kikubwa zaidi kama alivyosema mwanauchumi maarufu Joseph Stiglitz kwamba "countries behave like individuals"..... inamaanisha kuwa uchumi wa kijamii unaporomoka.......... Hivyo vijana wenzangu haswa wa kiume ambao historia, dini, mila na desturi zinatupendelea dhidi ya wenzetu kambi ya upinzani (KE), inatupasa turudie misingi mizuri ya kuanzisha mahusiano " TUSIJE PANDA PENZI PASIPO MAPENZI" ,,,,,:crying::crying: