Vigezo, masharti kuzingatiwe ili kuboresha elimu (waliozoea elimu ya mkato wasahau)

kalulukalunde

JF-Expert Member
May 27, 2016
1,056
1,083
“WALIOZOEA elimu ya mkato wasahau hilo sasa kwa sababu nimepewa jukumu la kuhakikisha elimu ya Tanzania inakuwa bora zaidi na yenye kuleta manufaa. Ni lazima utaratibu ufuatwe,”ni kauli ya Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako.

Anasema, Watanzania wanapaswa kufaidi matunda ya usomi wao na kwamba, hilo litawezekana endapo wataipata elimu bora katika kila ngazi, kuanzia shule ya msingi, sekondari na vyuoni.

Kwa mujibu wa Profesa Ndalichako, ili kufika hapo ni lazima yafanyike mabadiliko kwa ushirikiano na wananchi. “Mabadiliko katika sekta ya elimu yanataka ushirikiano wa kutosha kati ya Waziri wa Elimu, wizara anayoisimamia na wananchi.

Vinginevyo kuyapata ni vigumu,”anasema. Anasema, anafahamu kwa hali ya kawaida na kwa asili binadamu hapendi mabadiliko, hivyo unahitaji kufanya ayakubali, ayapokee na kuyazoea. Kwa mujibu wa Profesa Ndalichako, ili elimu ya Tanzania iwe na tija ni lazima afanye mabadiliko ili kuhakikisha kuwa kila kitu katika sekta hiyo kinakwenda sawa na wananchi wanafaidika.

Anabainisha kuwa, katika sekta ya elimu, Tanzania ilikuwa imefika mahali kila mtu alikuwa akijifanyia mambo yake bila kuzingatia utaratibu. Anawatuhumu waliopewa dhamana ya kuisimamia sekta hiyo kuwa walifanya kazi kiholela na kuruhusu njia za mkato.

Anasema, wanafunzi, walimu, wadau wa elimu na wasimamizi wa sekta hiyo nao wamekuwa wakitafuta njia za mkato kufanikisha masuala yao na matokeo yake wamesababisha elimu iwe holela.

“Kwa sababu hali hiyo ililetwa na mifumo pia katika sekta ya elimu, kuibadili kunahitaji nipewe ushirikiano na kila mmoja ili, pamoja na kuhakikisha ubora wa elimu kwa ngazi zote, niondoe mambo ya mkato mkato,” anasema Profesa Ndalichako. Anawaomba Watanzania wamuelewe na kufahamu kuwa, hana nia mbaya na wala hajapanga kumwonea au kumpendelea mtu kwa kubadilisha mifumo iliyopo.

Kwa kuzingatia maelezo ya Waziri Ndalichako, nia ya mabadiliko katika mifumo ya sekta ya elimu ni njema ya kuleta mifumo mizuri na thabiti itakayochochea mabadiliko chanya katika sekta ya elimu nchini ili vijana na Watanzania wote waone matunda ya kuelimika kwao. Anasema, anataka elimu ya Tanzania isimame katika ubora wake, kwa sababu sasa kuna malalamiko kuhusu sekta hiyo.

“Ninataka vijana wawe na mchango katika taifa na watu wafurahie matunda ya elimu wanayoipata na si kulalamika,”anasema Profesa Ndalichako. Soko la pamoja la EAC Professa Ndalichako anasema, kwa sababu tuko katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na kwa kuwa linaanzishwa soko la pamoja la jumuiya hiyo, ni lazima vijana wa Tanzania wajengewe mazingira wapate elimu bora ili wanufaike na soko hilo hasa la ajira na uchumi kwa ujumla.

EAC ina nchi sita wanachama ikiwemo Tanzania, Rwanda, Burundi, Kenya, Uganda na Sudan Kusini. Profesa Ndalichako anasema, kwa kuwa yeye ni Waziri wa Elimu, anawajibika kuhakikisha anafahamu Tanzania itasimama wapi katika soko la EAC kwa kuweka mazingira ya elimu bora, itakayowawezesha hasa vijana kunufaika na fursa zinazopatikana huko.

“Sitaki Watanzania wawe wasindikizaji tu katika soko hilo la Jumuiya ya Afrika Mashariki ndio maana naomba ushirikiano wao katika kuibadili mifumo iliyopo. Ninawaahidi kuwa dereva mwaminifu kuliendesha hili gari vizuri lifike linakotakiwa kwa usalama,” anasema.

Anawaomba Watanzania wawe abiria wema na wenye nia ya dhati kutaka sekta ya elimu ifikie mafanikio yanayokusudiwa na wala si kuanza kulitoa gari hilo upepo kwa sababu kufanya hivyo kutalifanya likwame kabla ya kumaliza safari.

Lugha ya kufundishia Kuhusu lugha ya kufundishia, Waziri Ndalichako anasema, ingawa Kiswahili ni lugha ya taifa la Tanzania, Kiingereza kinaendelea kutumika ili kuwawezesha Watanzania kushindana kwenye soko la ajira ndani na nje ya nchi. Anasema, kumekuwa na mitazamo tofauti miongoni mwa Watanzania na hasa wadau wa elimu kwa kuwa wengine wanataka itumike lugha ya taifa kufundishia kuanzia shule za awali hadi vyuo vikuu na wengine wanataka kitumike Kiingereza.

“Suala la lugha linatugawa Watanzania kwa kweli. Sisi wizara tumekuwa tukipeleka maoni ya Watanzania kwenye mijadala ya lugha ipi itumike kufundishia lakini mara zote tunapowafikia wataalamu inakuwa ni vigumu kufikia maoni mwafaka,” anasema Profesa Ndalichako.

Anasema, kwa sasa suala hilo limeachwa wazi kuruhusu mijadala iendelee kwa sababu, wakati wengine wakitaka Kiswahili, wengi wanatoa maoni kuonesha wanahitaji Kiingereza kitumike kuwawezesha wananchi kuwasiliana katika kipindi hiki ambacho dunia imekuwa kama kijiji kwa sababu ya utandawazi.

Chanzo: Habari leo
 
Huyu mama anania ya dhati. Tumuunge mkono. Nilishangazwa sana na kitendo cha waziri aliyepita kubadili "grading system" ambayo kwa kweli lengo lake lilikuwa ni kupanua magoli. Sasa tuna vijana wako vyuo vikuu ambao uwezo wao uko chini saaaana.
 
Huyu mama anania ya dhati. Tumuunge mkono. Nilishangazwa sana na kitendo cha waziri aliyepita kubadili "grading system" ambayo kwa kweli lengo lake lilikuwa ni kupanua magoli. Sasa tuna vijana wako vyuo vikuu ambao uwezo wao uko chini saaaana.
 
Go on mama ndalichako...kamwe usiruhusu siasa ziingilie katika Elimu... andaaa Muswada peleka Bungeni... suala la elimu kwa miaka hii 10 au 15 lisiguswe na mwanasiasa yoyote liwe china ya sheriaaa ambayo itaonyesha dira ya elimu yetu inatakiwa kwenda wapi... hata aje wazir wa elimu nani kazi yake ni kusimamia Dira tuliyoweka na sio kunadili badili mambo kila siku...na Akitaka kufanya mabadiliko ni lazima yapitishwe na Bunge... suala hapa mama ni sheria tu... la sivyo wanasiasa hawa sio watu wa kuwaamini wanaweza kukuundia zengwee wakuondoe muda wowote pale tu utakapogusa masilahi yao... Mama Tumia taaluma yako kujenga mfumo dhabitiii hata wakikutoaaa vizazi na vizazi vitakukumbuka kwa kujenga Elimu yetu.... Viva Mama Viva Mungu yupo mbele yako.....
 
Go on mama ndalichako...kamwe usiruhusu siasa ziingilie katika Elimu... andaaa Muswada peleka Bungeni... suala la elimu kwa miaka hii 10 au 15 lisiguswe na mwanasiasa yoyote liwe chini ya sheriaaa ambayo itaonyesha dira ya elimu yetu inatakiwa kwenda wapi... hata aje wazir wa elimu nani kazi yake ni kusimamia Dira tuliyoweka na sio kubadili badili mambo kila siku...na Akitaka kufanya mabadiliko ni lazima yapitishwe na Bunge... suala hapa mama ni sheria tu... la sivyo wanasiasa hawa sio watu wa kuwaamini wanaweza kukuundia zengwee wakuondoe muda wowote pale tu utakapogusa masilahi yao... Mama Tumia taaluma yako kujenga mfumo dhabitiii hata wakikutoaaa vizazi na vizazi vitakukumbuka kwa kujenga Elimu yetu.... Viva Mama Viva Mungu yupo mbele yako.....
 
Ondoa wahadhiri uchwara vyuoni.
Ondoa wanafunzi uchwara vyuoni.
Boresha ubora na udhibiti wa mitihani.
Ondoa walimu uchwara mashuleni.
Peleka wanafunzi wenye sifa sekondari.

Boresha maslahi ya watumishi wa sekta ya Elimu.
 
“WALIOZOEA elimu ya mkato wasahau hilo sasa kwa sababu nimepewa jukumu la kuhakikisha elimu ya Tanzania inakuwa bora zaidi na yenye kuleta manufaa. Ni lazima utaratibu ufuatwe,”ni kauli ya Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako.

Anasema, Watanzania wanapaswa kufaidi matunda ya usomi wao na kwamba, hilo litawezekana endapo wataipata elimu bora katika kila ngazi, kuanzia shule ya msingi, sekondari na vyuoni.

Kwa mujibu wa Profesa Ndalichako, ili kufika hapo ni lazima yafanyike mabadiliko kwa ushirikiano na wananchi. “Mabadiliko katika sekta ya elimu yanataka ushirikiano wa kutosha kati ya Waziri wa Elimu, wizara anayoisimamia na wananchi.

Vinginevyo kuyapata ni vigumu,”anasema. Anasema, anafahamu kwa hali ya kawaida na kwa asili binadamu hapendi mabadiliko, hivyo unahitaji kufanya ayakubali, ayapokee na kuyazoea. Kwa mujibu wa Profesa Ndalichako, ili elimu ya Tanzania iwe na tija ni lazima afanye mabadiliko ili kuhakikisha kuwa kila kitu katika sekta hiyo kinakwenda sawa na wananchi wanafaidika.

Anabainisha kuwa, katika sekta ya elimu, Tanzania ilikuwa imefika mahali kila mtu alikuwa akijifanyia mambo yake bila kuzingatia utaratibu. Anawatuhumu waliopewa dhamana ya kuisimamia sekta hiyo kuwa walifanya kazi kiholela na kuruhusu njia za mkato.

Anasema, wanafunzi, walimu, wadau wa elimu na wasimamizi wa sekta hiyo nao wamekuwa wakitafuta njia za mkato kufanikisha masuala yao na matokeo yake wamesababisha elimu iwe holela.

“Kwa sababu hali hiyo ililetwa na mifumo pia katika sekta ya elimu, kuibadili kunahitaji nipewe ushirikiano na kila mmoja ili, pamoja na kuhakikisha ubora wa elimu kwa ngazi zote, niondoe mambo ya mkato mkato,” anasema Profesa Ndalichako. Anawaomba Watanzania wamuelewe na kufahamu kuwa, hana nia mbaya na wala hajapanga kumwonea au kumpendelea mtu kwa kubadilisha mifumo iliyopo.

Kwa kuzingatia maelezo ya Waziri Ndalichako, nia ya mabadiliko katika mifumo ya sekta ya elimu ni njema ya kuleta mifumo mizuri na thabiti itakayochochea mabadiliko chanya katika sekta ya elimu nchini ili vijana na Watanzania wote waone matunda ya kuelimika kwao. Anasema, anataka elimu ya Tanzania isimame katika ubora wake, kwa sababu sasa kuna malalamiko kuhusu sekta hiyo.

“Ninataka vijana wawe na mchango katika taifa na watu wafurahie matunda ya elimu wanayoipata na si kulalamika,”anasema Profesa Ndalichako. Soko la pamoja la EAC Professa Ndalichako anasema, kwa sababu tuko katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na kwa kuwa linaanzishwa soko la pamoja la jumuiya hiyo, ni lazima vijana wa Tanzania wajengewe mazingira wapate elimu bora ili wanufaike na soko hilo hasa la ajira na uchumi kwa ujumla.

EAC ina nchi sita wanachama ikiwemo Tanzania, Rwanda, Burundi, Kenya, Uganda na Sudan Kusini. Profesa Ndalichako anasema, kwa kuwa yeye ni Waziri wa Elimu, anawajibika kuhakikisha anafahamu Tanzania itasimama wapi katika soko la EAC kwa kuweka mazingira ya elimu bora, itakayowawezesha hasa vijana kunufaika na fursa zinazopatikana huko.

“Sitaki Watanzania wawe wasindikizaji tu katika soko hilo la Jumuiya ya Afrika Mashariki ndio maana naomba ushirikiano wao katika kuibadili mifumo iliyopo. Ninawaahidi kuwa dereva mwaminifu kuliendesha hili gari vizuri lifike linakotakiwa kwa usalama,” anasema.

Anawaomba Watanzania wawe abiria wema na wenye nia ya dhati kutaka sekta ya elimu ifikie mafanikio yanayokusudiwa na wala si kuanza kulitoa gari hilo upepo kwa sababu kufanya hivyo kutalifanya likwame kabla ya kumaliza safari.

Lugha ya kufundishia Kuhusu lugha ya kufundishia, Waziri Ndalichako anasema, ingawa Kiswahili ni lugha ya taifa la Tanzania, Kiingereza kinaendelea kutumika ili kuwawezesha Watanzania kushindana kwenye soko la ajira ndani na nje ya nchi. Anasema, kumekuwa na mitazamo tofauti miongoni mwa Watanzania na hasa wadau wa elimu kwa kuwa wengine wanataka itumike lugha ya taifa kufundishia kuanzia shule za awali hadi vyuo vikuu na wengine wanataka kitumike Kiingereza.

“Suala la lugha linatugawa Watanzania kwa kweli. Sisi wizara tumekuwa tukipeleka maoni ya Watanzania kwenye mijadala ya lugha ipi itumike kufundishia lakini mara zote tunapowafikia wataalamu inakuwa ni vigumu kufikia maoni mwafaka,” anasema Profesa Ndalichako.

Anasema, kwa sasa suala hilo limeachwa wazi kuruhusu mijadala iendelee kwa sababu, wakati wengine wakitaka Kiswahili, wengi wanatoa maoni kuonesha wanahitaji Kiingereza kitumike kuwawezesha wananchi kuwasiliana katika kipindi hiki ambacho dunia imekuwa kama kijiji kwa sababu ya utandawazi.
Jesi-khaaa!!:rolleyes::rolleyes: Mkuki kwa nguruwe
 
Walimu wamepuuzwa tangu nchi imepata uhuru....

Wanafunzi wamepewa nafasi kubwa kuwazidi tangu enzi na enzi.......

Zana za kujifunza na kujifunzia ni kitendawili kisichoteguliwa kwa miaka.........

Wazazi wamewaachia walimu suala la malezi ya watoto wao.....na walimu wanajifanya hawajali.......


Serekali inafanya bora liende..........yaani kila kitu ni kufunika kombe mwanaharamu apite.

Sera za elimu ni butu aziakisi hitaji halisi la mtu mwenyewe anaejifunza, jamii na taifa kwa ujumla..........


Dira ya taifa ktk elimu haijulikani mpaka sasa na wadau woote wa elimu hata mm sijui.......

Wadau hawashirikishwi ktk uandaaji wa mipango, sera wala kufanya maamuzi yanayowahusu...kweli nyie uko mnayajua mawazo yao???


Napita tu.....ila dhana ya elimu yaitaji fikra changamfu.......wapo wachache wenye maono na mitazamo chanya juu ya elimu...kuwa makini na washauri wako na ushirikishe wadau kwa mapana mana penye wengi kuna fikra nyingi zenye faida......
 
Ondoa wahadhiri uchwara vyuoni.
Ondoa wanafunzi uchwara vyuoni.
Boresha ubora na udhibiti wa mitihani.
Ondoa walimu uchwara mashuleni.
Peleka wanafunzi wenye sifa sekondari.

Boresha maslahi ya watumishi wa sekta ya Elimu.

hii ni kazi ya miaka 5 mpaka 10.
cha muhimu ni kumuombea UHAI tu ili atekeleze nia yake iliyo thabiti.
ila pia ni muhimu kulay down kila kitu maana hata kesho asipo kuwepo basi atakaye kuja aendeleze, so apeleke dira ya elimu bungeni.
 
Ondoa wahadhiri uchwara vyuoni.
Ondoa wanafunzi uchwara vyuoni.
Boresha ubora na udhibiti wa mitihani.
Ondoa walimu uchwara mashuleni.
Peleka wanafunzi wenye sifa sekondari.

Boresha maslahi ya watumishi wa sekta ya Elimu.
Hasa vyuoni kuna walimu mpaka unashangaa amefikaje pale!
 
Arudishe pia shule za sekondari za watoto wenye vipaji maalumu na ziwe zenye ubora na viwango vinavyozidi shule za binafsi

Hizi shule za vipaji maalumu hazikuwa na maana yeyote. Maana zilikuwa hazina mwendelezo wowote ktk vyuo. Hata katika uzalishaji hatuwaoni hawa wanafunzi waliosoma shule hizo wakifanya mqmbo ya maana.

Cha msingi elimu iboreshwe.
 
Hasa vyuoni kuna walimu mpaka unashangaa amefikaje pale!

Yaani mkuu ni aibu. Nilipokuwa sekondari nilikuwa nikidhani kuwa profesa anazungumza point kama Obama halafu wana kingereza kizuri kama cha malkia Elizabeth. Kumbe bwana looo! Hata walimu wangu wa primary wana afadhali. Hovyo kabisa.
 
Hatua nzuri sana.Kama kweli wanasikiliza wananchi wanasema nini, mawaziri, wasiruhusiwe kusomesha watoto wao kwenye shule binafsi.

Shule za ufundi zifufuliwe!
 
Mwl na waziri wa wizara ninayoitumikia ninakuamini na kukubali sana hasa katika yale masomo yako ya tafiti na upimaji wa elimu.
Ni kweli lugha ya kufundishia ni mtego mkubwa sana kwako na kama inakupendeza basi, turejeshe kufundisha masomo yote kwa lugha ya kiingereza kuanzia darasa la nne na kuendelea hadi chuo kikuu kwani nchi nyingi zinatumia lugha hii kufundisha na pia ni lugha ya soko ambayo itamsaidia mtanzania kupata exposure nje ya mipaka. Oneni hata kazi za majumbani kwa wageni zinafanywa na wazambia, wamalawi, wakenya na waganda.
Tena uliharakishe hili mwakani tuanze nalo kwani linawezekana. Usitusahau sisi walimu japo tunapuuzwa sana na wanasiasa tena wengine tuliwafundisha wenyewe. Rudisha refresher course kwa walimu.
 
Kwa ulimwengu wa sasa tukisema kiswahili kiwe ndiyo lugha ya kufundishia tunajidanganya, kwa mtazamo wangu kiswahili kiwa kama somo la lugha linalo jitegemea, masomo ya mengine ya sanaa, historia, siasa,maarifa, hesabu na sayansi yafundishwa wa kingereza toka la kwanza au la tatu, hii itaidia mtoto kumjenga mapema, kukabiliana na changamoto za elimu ya juu. Tengeneza picha Mwalimu wa kingereza anaingia kwa wiki mara tatu darasa anafundisha lugha ya kingereza, masomo mengine lugha ya kiswahili alafu akifika sekondari lugha ya kufundishia inabadilika, kiswahili kinakuwa somo la lugha kingereza kinakuwa lugha ya kufundishia, hatari mpaka hapo mwanafunzi anakuwa na kazi ya ziada Kutransate masomo kwa mosomo kwa lugha ya kingereza na kuendelea kujifunza lugha ya kingereza. Na kama mwanafunzi watakuwa watawekewa lugha ya kufundishia kingereza itakuwa ni rahisi kwao, kujifunza kiswahili kama somo, na itakuwa hakina shida sana maana hata nyumbani unakuwepo muda mwengi wa kukitumia. Dunia imekuwa imekuwa kama Kijiji ndiyo maana simu his wachina, wafaransa, nao wanajifunza kingereza kukabiliana na changamoto za dunia ya sasa.
 
Kufanikiwa kwa hili ni kuwa kuwa na sera madhubuti ya elimu yenye kusimamiwa na sheria na kanuni zake. Mfumo uliopo umeharibu elimu na kuwa na majaribio kwa kugeuza mitaala kila leo. Vyuo vikuu kuna wahadhili hata kuwaongoza wanafunzi kwenye final projects hawawezi, chimbuko la watu wa mitaani kuwafanyia project wanafunzi. Tanzania ya viwanda inaongelewa wakati mitaala ya ufundi imedunishwa, kama vile kufutwa sylabus ya ftc ya miaka 3 na kubandikwa diploma ya miaka 2, nak . Jitahidi mama, Mungu yuko nawe.
 
Back
Top Bottom