Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,908
- 945
MBUNGE DANIEL SILLO ASHIRIKI UZINDUZI WA JENGO KITUO CHA POLISI KATA YA GALLAPO
Mbunge wa Babati vijijini na mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Daniel Sillo Julai 18, 2023 ameshiriki kwenye uzinduzi wa jengo la kituo cha polisi kata ya Gallapo kilichozinduliwa na Waziri wa mambo ya ndani Mhe Mhandisi Hamadi Masaun
Pia Mhe Sillo alimuomba waziri kuletewa gari la polisi, wananchi wapatiwe vitambulisho vya taifa, kituo kifanye kazi masaa 24 pamoja na hayo aliomba kujengewa kituo cha polisi kata ya Bashinet
Ambapo waziri alisema vitambulisho vya taifa vitakuwa tayari kabla ya mwezi desemba na pia wataleta magari na pikipiki sambamba la hilo alilichukuwa swala la ujenzi wa kituo cha polisi Bashinet na kuwaagiza uongozi wa polisi kufanya kazi Kwa saa 24 kwa kuwa kituo hicho kiko daraja C
Mbunge wa Babati vijijini na mwenyekiti wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe Daniel Sillo akisalimiana na wananchi wenzake wa jimbo la Babati vijijini katika kata ya Gallapo mara baada ya uzinduzi wa kituo cha polisi kilichozinduliwa na Waziri wa mambo ya ndani Mhe Mhandisi Hamadi Masaun