Uzi maalum: Mrejesho,vikao vya mabaharia

No Escape

JF-Expert Member
Mar 7, 2016
6,663
7,737
Katika vikao vyetu mbalimbali tunavyokaa huwa tunapitisha miswada mbalimbali ila bado naona kuna baadhi ya wenzetu wanatuangusha. Sasa miswada yetu tuliyokubaliana tutaiweka hapahapa ili haya mambo yasiwe yanajirudia:

1. Mwanaume kuomba ushauri baada ya kumfumania mwenza wako hii usituletee hapa

2. Mwanaume kukimbia baada ya kumjaza mtoto wa watu ujauzito sisi hatuna ushauri.

3. Mwanaume kulialia demu wako amekuacha Aisee mmalizane hukohuko kama utajinyonga utajua mwenyewe.

4. Mwanaume unampenda demu halafu eti unaomba ushauri umuanzaje na wakati pesa unayo, usituletee hapa

5. Mwanaume unalala na mwanafunzi mpaka unamtia mimba halafu unashindwa ufanye nini unakuja kutusumbua hapa, acha uoga miaka 30 sio mingi we nenda tu gerezani na huko kuna binadamu kama wewe.
 
Nina ombi.

Kiwango cha kuhonga tupunguzeni 7800 ni nyingi sana bado ikiwa 3000 itapendeza.

Swala la kusomesha hili bado nafikiri tuendelee kulijadili inakuwaje.

Mwanachama hai hapa kadi no B1994
 
troublemaker,
Natambua uwepo wako, Kuhusu kiwango cha kuhonga kinajulikana kilishajidiliwa kitatokana na mapenzi yenu Ila usije kutulilia eti Demu wangu anapenda pesa wakati unatoa mwenyewe.
Hilo la kusomesha limeleta changamoto, tumegundua kuna mabaharia wenzteu wanasomeshwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom