Traxtion
JF-Expert Member
- Dec 10, 2021
- 5,895
- 11,788
DODOMA: Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa amewataka wadau wote wanaosimamia ujenzi wa Kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Msalato kushirikiana ili ujenzi huo ukamilike ifikapo Mei mwaka huu.
Akizungumza jijini Dodoma, leo Januari 14, 2026 wakati akikagua maendeleo ya ujenzi huo, Prof. Mbarawa amesema hatua ya ukamilishaji wa ujenzi (finishing), inahitaji umakini, kujali thamani ya fedha na ubora wa vifaa unaoendana na mahitaji.
"Mameneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mamalaka ya Viwanja vya ndege (TAA), Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) pamoja na Zimamoto na Uhamimiaji shirikianeni kikamilifu ili vifaa na mifumo ya uendeshaji isomane na kurahisisha utendaji wa kazi kiwanjani hapo," amesisitiza Prof. Mbarawa.
Kwa upande wake, Meneja wa TANROADS mkoa wa Dodoma Eng. Zuhura Amani amesema wamejipanga kumsimamia kikamilifu mkandarasi anaejenga kiwanja hicho ili kikamilike kwa wakati.
Nae Mkurugenzi wa Kiwanja kiwanja hicho, Clemence Mbaruck amesema watahakikisha ujenzi unakamilika kwa viwango na tayari watumishi 170 tayari wameshahamishiwa Dodoma kwa ajili ya kuanza kazi kwenye kiwanja hicho mara baada ya kufunguliwa rasmi.
Zaidi ya shillingi bilioni 370 zinatumika kwa ajili wa ujenzi huo na kukamilika kwake kutachochea ukuaji wa uchumi kwa wakazi wa Dodoma kwani kutaruhusu ndege aina mbalimbali za kitaifa na kimataifa kutua kiwanjani hapo.
Source
#HabarileoUPDATES
________________
Japo sielewi serikali itafanyaje ili kusaidia hii Msalato Airport iwe na flight za kutosha maana watu wengi Tanzania wanatumia mabasi, na wale wanaosafiri kutoka nje mara nyingi wanatua Dar es Salaam, Arusha au Zanzibar. Mikoani safari ni chache ndio maa kunakuwa na viwanja vidogo.
Kwa hiyo serikali inapaswa kuipa sababu jiji la Dodoma kupata safari nyingi za ndege ili uwanja mkubwa kama huu usiwe na flights za kuhesabu, bali iwe one of the busiest airports in the region
Akizungumza jijini Dodoma, leo Januari 14, 2026 wakati akikagua maendeleo ya ujenzi huo, Prof. Mbarawa amesema hatua ya ukamilishaji wa ujenzi (finishing), inahitaji umakini, kujali thamani ya fedha na ubora wa vifaa unaoendana na mahitaji.
"Mameneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mamalaka ya Viwanja vya ndege (TAA), Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) pamoja na Zimamoto na Uhamimiaji shirikianeni kikamilifu ili vifaa na mifumo ya uendeshaji isomane na kurahisisha utendaji wa kazi kiwanjani hapo," amesisitiza Prof. Mbarawa.
Kwa upande wake, Meneja wa TANROADS mkoa wa Dodoma Eng. Zuhura Amani amesema wamejipanga kumsimamia kikamilifu mkandarasi anaejenga kiwanja hicho ili kikamilike kwa wakati.
Nae Mkurugenzi wa Kiwanja kiwanja hicho, Clemence Mbaruck amesema watahakikisha ujenzi unakamilika kwa viwango na tayari watumishi 170 tayari wameshahamishiwa Dodoma kwa ajili ya kuanza kazi kwenye kiwanja hicho mara baada ya kufunguliwa rasmi.
Zaidi ya shillingi bilioni 370 zinatumika kwa ajili wa ujenzi huo na kukamilika kwake kutachochea ukuaji wa uchumi kwa wakazi wa Dodoma kwani kutaruhusu ndege aina mbalimbali za kitaifa na kimataifa kutua kiwanjani hapo.
Source
#HabarileoUPDATES
________________
Japo sielewi serikali itafanyaje ili kusaidia hii Msalato Airport iwe na flight za kutosha maana watu wengi Tanzania wanatumia mabasi, na wale wanaosafiri kutoka nje mara nyingi wanatua Dar es Salaam, Arusha au Zanzibar. Mikoani safari ni chache ndio maa kunakuwa na viwanja vidogo.
Kwa hiyo serikali inapaswa kuipa sababu jiji la Dodoma kupata safari nyingi za ndege ili uwanja mkubwa kama huu usiwe na flights za kuhesabu, bali iwe one of the busiest airports in the region