Uwanja sawa, lakini Bil. 2 hapana!

Makonyeza

Member
Feb 2, 2020
67
248
Uwanja sawa, lakini Bilion mbili hapana!

Kwanza nina declare interest, mimi ni Yanga damu, na sijaandika haya kwa sababu mimi ni Yanga, Lah!
Miaka nenda miaka rudi masimango ya wadau wa Mpira kwa timu zetu mbili kubwa ni suala la uwanja, watu wanahoji kwa Club iliyoanzishwa mwaka 11 February 1935 mpaka leo kukodi uwanja wa mazoezi, hii hapana!

Kwa hili bila kumung'unya maneno, nasema kongole kwa wana Simba kama kweli mna dhamira ya dhati ya kuujenga uwanja wenu.
Japo sijui hiyo bajeti ya Bilion thelathini mmeipataje na kujiwekea lengo ilhali hata michoro hamna.

Lakini anyways, hiyo sio ishu kwangu, inawezekana mmeamua kufanya Siri japo najua hamna kitu kama hicho. Kwenye hayo mambo ya umma hakunaga siri coz mwisho wa siku lazima utangaze tenda ili kuipata kampuni ya kuifanya hiyo kazi ambayo ndio itakupa andiko la gharama halisi za ujenzi.

Lakini Kuna ukakasi mkubwa, kiongozi ameamsha kampeni hiyo akiahidi kuchangia Bil. 2, hii kwangu naweka BIG NO.
Kwanza nikuhakikishieni, kimahesabu Inawezekana kabisa kuuujenga uwanja wa Mpira wenye viwango vyovyote kwa michango, asikudanganye mtu eti haliwezekani, akabeza, muache abeze, kwani hata uwanja wa taifa si umejengwa na michango yetu hiyo hiyo iliyobadilishwa tu Jina ikaitwa KODI.

Hesabu rahisi tu, kwani wanachama Milioni nne wa Simba wakilipa Ada Yao ya uanachama kwa mwaka si inapatikana Bilion 48?, tena inavuka na lengo, kwa hili Simba mnaweza msikatishwe tamaa, na hata Yanga wakiamua wataweza, ni suala la kuamua tu!

Sasa nirudi kwenye hoja yangu ya msingi, bwana mkubwa yeye ameahidi kutoa Bilioni mbili, si haba, ni fedha pia na inaweza kuwa msaada mkubwa sana kwenye kampeni ya uhamasishaji uchangiaji!

Lakini shida yangu ni moja tu, hivi kimahesabu hizo Bilioni Mbili si asilimia 7.5 tu ya Bilioni 30?
Yes,sijabahatisha bhana, ni asilimia saba unusu tu.

Sasa kama ni hivyo, watu wa Simba msiogope kuhoji, mimi nakuonesheni njia ya kuanzia kuhoji, huyo Tajiri si inadaiwa amenunua hisa zile 49%?

Sasa kama mlikuwa hamjui ni kwamba kila asset itakayosajiliwa kwa Jina la Simba sports Club asilimia 49% itakuwa ni ya bwana mkubwa, bila kujali hiyo Mali imepatikanaje.

Hii ndio kusema kwamba, hata huo uwanja kama hati yake inasoma au itasoma Jina la Simba SPORTS club, Shea yenu WANA simba ni ile asilimia 51% na 49% inayobaki ni Mali ya bwana mkubwa.

Maana yangu ni kwamba kwa bwana mkubwa kuchangia Bil 2 ya uwanja maana yake amechangia asilimia 7.5 tu lakini kwenye hati za umiliki atachukua 49%,sijui mnanielewa!??
Si juzi mmetangaza mmeingia kwenye mfumo wa hisa na yeye amelipa Bil. 20?

Yaani maana yake zaidi ni kwamba zile 41.5% za umiliki wake katika uwanja zote atanunuliwa na wanachama na wapenzi WA simba,hii haiko sawa bhana, Sasa hapa ndio wale jamaa wa FCC inabidi watumiwe kuhoji kwa sababu tunazungumzia umiliki wa hisa, tunazungumzia biashara hapa ambao mwisho wa mwaka watu inabidi wakae mezani kugawana kilichopatilana na kila mtu atapata kulingana na uwiano wa umiliki wake wa HISA.

LAKINI nisiwakatisheni tamaa, mna hiyari aidha mumnunulie Tajiri wenu hizo Shea 41.5% au mmwambie ukweli bila kumuogopa kwamba huo anaoita mchango si mchango ni fedha za manunuzi ya hisa zake kwenye umiliki wa uwanja wenu, kwa hivyo kiuhalisia wamambo kama ni kuchangia basi achangie hizo asilimia zote 49% ambazo makaratasi ya mahesabu yatamtambua yeye kama mmiliki bila kujali kwamba waliochanga ni mashabiki na wanachama ambao Ada Yao ya mwaka hulipa kwa mbinde na kujinyima, na wakati mwingine hata pesa ya kiingilio kwenye mechi inawashinda.
Ukiamua kutokuelewa shauri zako, na ukibisha ukweli huu we bisha tu!

Daima mbele nyuma mwiko!
 
Uwanja sawa, lakini Bilion mbili hapana!

Kwanza nina declare interest, mimi ni Yanga damu, na sijaandika haya kwa sababu mimi ni Yanga, Lah!
Miaka nenda miaka rudi masimango ya wadau wa Mpira kwa timu zetu mbili kubwa ni suala la uwanja, watu wanahoji kwa Club iliyoanzishwa mwaka 11 February 1935 mpaka leo kukodi uwanja wa mazoezi, hii hapana!

Kwa hili bila kumung'unya maneno, nasema kongole kwa wana Simba kama kweli mna dhamira ya dhati ya kuujenga uwanja wenu.
Japo sijui hiyo bajeti ya Bilion thelathini mmeipataje na kujiwekea lengo ilhali hata michoro hamna.

Lakini anyways, hiyo sio ishu kwangu, inawezekana mmeamua kufanya Siri japo najua hamna kitu kama hicho. Kwenye hayo mambo ya umma hakunaga siri coz mwisho wa siku lazima utangaze tenda ili kuipata kampuni ya kuifanya hiyo kazi ambayo ndio itakupa andiko la gharama halisi za ujenzi.

Lakini Kuna ukakasi mkubwa, kiongozi ameamsha kampeni hiyo akiahidi kuchangia Bil. 2, hii kwangu naweka BIG NO.
Kwanza nikuhakikishieni, kimahesabu Inawezekana kabisa kuuujenga uwanja wa Mpira wenye viwango vyovyote kwa michango, asikudanganye mtu eti haliwezekani, akabeza, muache abeze, kwani hata uwanja wa taifa si umejengwa na michango yetu hiyo hiyo iliyobadilishwa tu Jina ikaitwa KODI.

Hesabu rahisi tu, kwani wanachama Milioni nne wa Simba wakilipa Ada Yao ya uanachama kwa mwaka si inapatikana Bilion 48?, tena inavuka na lengo, kwa hili Simba mnaweza msikatishwe tamaa, na hata Yanga wakiamua wataweza, ni suala la kuamua tu!

Sasa nirudi kwenye hoja yangu ya msingi, bwana mkubwa yeye ameahidi kutoa Bilioni mbili, si haba, ni fedha pia na inaweza kuwa msaada mkubwa sana kwenye kampeni ya uhamasishaji uchangiaji!

Lakini shida yangu ni moja tu, hivi kimahesabu hizo Bilioni Mbili si asilimia 7.5 tu ya Bilioni 30?
Yes,sijabahatisha bhana, ni asilimia saba unusu tu.

Sasa kama ni hivyo, watu wa Simba msiogope kuhoji, mimi nakuonesheni njia ya kuanzia kuhoji, huyo Tajiri si inadaiwa amenunua hisa zile 49%?

Sasa kama mlikuwa hamjui ni kwamba kila asset itakayosajiliwa kwa Jina la Simba sports Club asilimia 49% itakuwa ni ya bwana mkubwa, bila kujali hiyo Mali imepatikanaje.

Hii ndio kusema kwamba, hata huo uwanja kama hati yake inasoma au itasoma Jina la Simba SPORTS club, Shea yenu WANA simba ni ile asilimia 51% na 49% inayobaki ni Mali ya bwana mkubwa.

Maana yangu ni kwamba kwa bwana mkubwa kuchangia Bil 2 ya uwanja maana yake amechangia asilimia 7.5 tu lakini kwenye hati za umiliki atachukua 49%,sijui mnanielewa!??
Si juzi mmetangaza mmeingia kwenye mfumo wa hisa na yeye amelipa Bil. 20?

Yaani maana yake zaidi ni kwamba zile 41.5% za umiliki wake katika uwanja zote atanunuliwa na wanachama na wapenzi WA simba,hii haiko sawa bhana, Sasa hapa ndio wale jamaa wa FCC inabidi watumiwe kuhoji kwa sababu tunazungumzia umiliki wa hisa, tunazungumzia biashara hapa ambao mwisho wa mwaka watu inabidi wakae mezani kugawana kilichopatilana na kila mtu atapata kulingana na uwiano wa umiliki wake wa HISA.

LAKINI nisiwakatisheni tamaa, mna hiyari aidha mumnunulie Tajiri wenu hizo Shea 41.5% au mmwambie ukweli bila kumuogopa kwamba huo anaoita mchango si mchango ni fedha za manunuzi ya hisa zake kwenye umiliki wa uwanja wenu, kwa hivyo kiuhalisia wamambo kama ni kuchangia basi achangie hizo asilimia zote 49% ambazo makaratasi ya mahesabu yatamtambua yeye kama mmiliki bila kujali kwamba waliochanga ni mashabiki na wanachama ambao Ada Yao ya mwaka hulipa kwa mbinde na kujinyima, na wakati mwingine hata pesa ya kiingilio kwenye mechi inawashinda.
Ukiamua kutokuelewa shauri zako, na ukibisha ukweli huu we bisha tu!

Daima mbele nyuma mwiko!
Wewe kinachokuuma nini? Sisi tunachotaka ni mataji na uwanja. Huo ushauri peleka huko Utopoloni kwenu.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Japokuwa mimi ni Simba dam dam ila hili nililipinga tangu mwanzo ila wakaishia kuniita mwana utopolo na wengine wakadiriki hata kuniuliza nateseka nikiwa wapi, ila huo ndio uhalisia hapa Mo anatupiga kama wana simba.
 
Japokuwa mimi ni Simba dam dam ila hili nililipinga tangu mwanzo ila wakaishia kuniita mwana utopolo na wengine wakadiriki hata kuniuliza nateseka nikiwa wapi, ila huo ndio uhalisia hapa Mo anatupiga kama wana simba.
Naikumbuka vyema post yako, halafu wenzio wakakushikia kama mwewe. Ndio asili ya mashabiki wa kibongo usiwaguse viongozi au usiseme ukweli utaambiwa wewe sio mwana yanga mwenzetu au wewe sio mwana simba mwenzetu.
 
Heri aliyenacho hata kama ni kidogo kuliko asiyekuwanacho kabisa. Umesha declare kuwa wewe ni hasimu wa simba hivyo chochote utakachoshauri kitachukuliwa katika mizania hiyo. Mwenye wivu wa maendeleo hawezi kukushauri vema, anatamani ubakie ulivyo ili usimzidi.
 
21 Reactions
Reply
Back
Top Bottom