UVCCM mbona hamchangii ripoti ya CAG?

Lord OSAGYEFO

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2021
Posts
3,079
Reaction score
4,891
Hakika inashangaza sana Kiona Vijana UVCCM wapo KIMYA KABISA juu yanayojiri katika RIPOTI ya CAG Aliyomkabidhi Mwenyekiti wa Ccm Na RAIS wa Tanzania.Nilitarajia kuwasikia VIJANA UVCCM wakiichambua kwa KINA RIPOTI hiyo na kutoa Maoni yao lakini Wapo Kimya kama Vile hakuna RIPOTI
 
🤣🤣🤣🤣wameikacha kama hawaioni vile
 
Wako busy wanajichubua na katibu mwenezi wao,wako busy na mkorogo
 
Kama taifa tuwe na misingi na taasisi imara ( Katiba Bora). Haya mambo ya hofu fulani aseme yamerudisha nyuma na kukwamisha taifa.
Miradi ya kwenye mabango waweke thamani ya mradi pia.
 
Hawajapata taarifa rasmi
 
Ccm wanajua kujipatia sifa kwenye kushinda chaguzi kwingine kote hakuna maana wanayo fahamu
 
Ripot za CAG huwa ni SAwa na ngojera za kusoma KILA mwaka, huwa hazifanyiwi Kazi wala hazizuii wezi kuiba.
Mwakani tutazisikia tena, sijui sasa CAG ana Kazi gani zaidi ya kuchonganisha watu na serikali, kama ripoti hazifanyiwi Kazi si SAwa na ngojera tu.
 
Magu alikuwa bize kuua upinzani huku watu wako bize kuiba
 
Hawawezi kuchangia maana hata wenyewe hawaelewi, wanadhangaa tu, mmoja amekuja na uzi wa kuwananga mods kwamba wamenunuliwa na chadema, tunasubiri evidence ya muamala wa manunuzi
 
Mkuu watasema nini wakati karibu 90% walikuwa waimba mapambio ya SHUJAA! Walisifu na kutukuza hata pale pasipofaa, walinanga wenye mawazo kinzani na walishangilia watu kufungwa na kuteswa. Walipiga propaganda juu ya miradi ya kifisadi ile ya chato airport, walikenua meno kuhusu GAWIO la taasisi kumbe zinapata hasara.
CAG kaja kuumbua UNAFIKI na uongo wao, watajadili nini?
 
Report ya CAG ni aibu kubwa kwa ccm.
 
Watachangia vuta subira wanasubir chadem mjibu hoja ya kupokea malilo hewa ya milion 37 alafu mmeuchuna kimyaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…