The Businessman
JF-Expert Member
- Jan 9, 2014
- 7,397
- 9,263
Nakumbuka miaka ya zamani hadi mwishoni wa mwaka 2009 ukipita sehemu za vyuoni huko huu umoja ndio ulikuwa sehemu yake ya kujidai na pia ulikuwa na nguvu na ushawishi. Kinyume na sasa umoja huu hausikiki mahala popote hata vyuoni huko watu wanaogopa kujitambulisha wao ni UVCCM japo ni wachache sana wanaojitambulisha. Sasa ni nini kimekipata Umoja huu mpaka umeshindwa hata kutambulika leo hii ukimuuliza hata mwanachama wa CCM kiongozi wa UVCCM TAIFA ni nani hawajui kidogo anayejulikana ni Paul Makonda na Jely Slaa.