Huu mchoro kwy ukuta wa Shule ya Upili ya Ben Mkapa una maana gani, muktadha gani na mantiki gani kwa ustaarabu wa zama hizi. Je, siyo dhalili kwa utu wa binadamu hususan weusi?
Angepiga mzungu picha kwenda kuanika kwao kuonyesha jinsi tusivyofaa sote tungempigia makofi lakini nikipiga mimi picha au wewe atazuka mtu kuhoji kwanini umepiga picha wkt ule mchoro umewekwa pale kwa ajili ya umma (hata usipoupiga picha umma utauona tu na kuujadili hata kimoyomoyo).
Nadhani wakati umefika tuhariri na kudurusu historia yetu. Siyo kila kumbukumbu hata iliyo dhalili tunaienzi milele yote.
Ila tuna haja kweli ya kuenzi historia inayotuonyesha jinsi babu zetu walivyofanyishwa kazi ngumu za mauti na za kuwapunguzia thamani ya ubinadamu wao; kwa malipo ya tonge 7 za ugali na punje 3 za maharagwe?
Superiority of Eurocentric history over inferiority of Afrocentric history.