Tanzania bado wapo watu wanaotumikishwa kama watumwa chini ya ukandamizaji wa watanzania na siyo wawekezaji hasa kwenye sekta ya madini.Kwenye makampuni ya drilling/uchorangaji kwa asilimia kubwa ni sehemu ambayo wafanyakazi wake hufanya kazi ngumu na za hatari sana na ni moja ya maeneo ya kinyonyaji ambapo utakuta makampuni haya hayawafanyishi kazi kwa taratibu na sheria za kazi.eneo hili limekuwa halina mtetezi kwa muda mrefu sasa kutokana pia na waajiriwa wengi maeneo haya ni vijana ambao wengi hawana elimu kubwa.
Katika kutembea maeneo mbali mbali ya uwekezaji katika sekta ya madini sikuwahi kuona kiongozi wa serikali akitetea maslahi ya watanzania ingawa wawekezaji wengi wamekuwa wakipitia kwa viongozi wa serikali na kuwaomba ushauri juu ya maslahi ya watakao waajiri,kwa mfano wakuu wa wilaya,wengi wamekuwa wakishauri viwango vidogo vya mishahara kiasi cha baadhi ya wawekezaji kuwashangaa na hata wengine kusema hawaitetei serikali yao kwani kwa kushauri viwango vidogo kiasi hicho wanainyima serikali yao mapato ya kodi.Hali hii kwa mtizamo pia inasababishwa na ubinafsi,mbunge,mkuu wa wilaya au afisa fulani asingependa kusikia malipo yanayomzidi kwani yupo mkuu wa wilaya fulani alidiriki kusema mishahara ya magiologisti ni mikubwa kuliko mkuu wa wilaya kwa maana ya kutaka ipunguzwe.
Nawaomba mjirekebishe wenye hizi tabia na tuwatetee watanzania bila ubinafsi na wanaohusika chukueni hatua.
Katika kutembea maeneo mbali mbali ya uwekezaji katika sekta ya madini sikuwahi kuona kiongozi wa serikali akitetea maslahi ya watanzania ingawa wawekezaji wengi wamekuwa wakipitia kwa viongozi wa serikali na kuwaomba ushauri juu ya maslahi ya watakao waajiri,kwa mfano wakuu wa wilaya,wengi wamekuwa wakishauri viwango vidogo vya mishahara kiasi cha baadhi ya wawekezaji kuwashangaa na hata wengine kusema hawaitetei serikali yao kwani kwa kushauri viwango vidogo kiasi hicho wanainyima serikali yao mapato ya kodi.Hali hii kwa mtizamo pia inasababishwa na ubinafsi,mbunge,mkuu wa wilaya au afisa fulani asingependa kusikia malipo yanayomzidi kwani yupo mkuu wa wilaya fulani alidiriki kusema mishahara ya magiologisti ni mikubwa kuliko mkuu wa wilaya kwa maana ya kutaka ipunguzwe.
Nawaomba mjirekebishe wenye hizi tabia na tuwatetee watanzania bila ubinafsi na wanaohusika chukueni hatua.