Utumishi hii sio fair kabisa

Utumishi hii sio fair kabisa

fazam

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2014
Posts
1,868
Reaction score
1,291
wadau mimi ni mmoja wa vijana tuliofanya written interview post ya admission & examination officer tpsc tar 11 desemba....nikafanikiwa kuitwa oral tarehe 12 desemba..cha ajabu tukiwa tunaendelea kufanyiwa interview akaletwa kijana mpya ambaye hatukumuona kwenye written na kuambiwa kuwa ni mwenzetu tukabaki tukishanga na kukosa la kufanya...nkifikiria nakosa imani tena na utumishi...bora ningehadithiwa lkn nilishuhudia mwenyewe...kama kuna mtu unamfahamu alifanya interview hio muulize
 
Huyo lazima apite,mwenzenu kivip wakat hajafanya written mbona ubabaishaji utumishi
 
duh!!sasa nani aliwaambie huyo ni mwenzenu?....!!mi sajawahi ona hiyo kitu itakuwa labda hapo Utumishi tu eti kiongozi anawatambulisha mtu.!!!!....kwani written interview mlikuwa wangapi hadi mkajitambua na kujua mtu mgeni?
 
brother m co mjinga kiasi hicho written tulifanya 16 tu...kwa hyo tukawa tunafahamiana coz tulikaa chumba kimoja.......kushindwa oral co sababu ya kushindwa kusema ukweli
 
amini nlichoandika aliletwa na mshkaji aliyekua anakusanya vyeti na kuvipeleka kwenye committee
 
16 tu bro...na alitambulishwa na staff wa utumishi aliyekuwa akituita na kuchukua vyeti kuvipeleka kwenye panel kabla hujaingia
 
brother m co mjinga kiasi hicho written tulifanya 16 tu...kwa hyo tukawa tunafahamiana coz tulikaa chumba kimoja.......kushindwa oral co sababu ya kushindwa kusema ukweli
 
Watanzania bhana, ungechaguliwa wala usingetoboa uozo huo,... hi tanzania bhana aya mambo yapo, MKIAMBIWAGA MNAONA KAMA TUNAPGA SIASA NCHI YETU IYO IMEOZA... NIKUIZIKA SERIKAL NDO SOLUHISHO YA YOTE....... MWANANGU MI MWENYEWE NIMESHUUDIA IYO MISION POSsible...
 
wadau mimi ni mmoja wa vijana tuliofanya written interview post ya admission & examination officer tpsc tar 11 desemba....nikafanikiwa kuitwa oral tarehe 12 desemba..cha ajabu tukiwa tunaendelea kufanyiwa interview akaletwa kijana mpya ambaye hatukumuona kwenye written na kuambiwa kuwa ni mwenzetu tukabaki tukishanga na kukosa la kufanya...nkifikiria nakosa imani tena na utumishi...bora ningehadithiwa lkn nilishuhudia mwenyewe...kama kuna mtu unamfahamu alifanya interview hio muulize

Mkuu kumbuka hii ni Tanzania what matters most is whom you knows and not What you knows!!!! kikubwa kushukuru Mungu umepata bahati ya kuitwa kwa mara ya pili ila usi judge saana kumuona huyo mtu Je ungemkuta ofisini kabisa anasign Mkataba ingekuwaje??!! be nice n patient The almighty God is with you wahanga tusie na marefa katika suala la job hunting n seeking. All the best at your selections wadau wote.
Raise your sons n daughters more than u have matured.... That's ma only dedication Will left by ma father!!!!:glasses-nerdy:
 
Duh kweli tanzania yetu hii inazidi kua ngumu siku hadi siku. Sasa kwa sisi tusiokua na watu wakutushika mikono tutafika wap jaman.
 
wadau mimi ni mmoja wa vijana tuliofanya written interview post ya admission & examination officer tpsc tar 11 desemba....nikafanikiwa kuitwa oral tarehe 12 desemba..cha ajabu tukiwa tunaendelea kufanyiwa interview akaletwa kijana mpya ambaye hatukumuona kwenye written na kuambiwa kuwa ni mwenzetu tukabaki tukishanga na kukosa la kufanya...nkifikiria nakosa imani tena na utumishi...bora ningehadithiwa lkn nilishuhudia mwenyewe...kama kuna mtu unamfahamu alifanya interview hio muulize

ninachojua utumishi hufanya interview za aina mbili..practical na oral..
watu wa mtindo huo sio.kwamba kachomekwa ila anakuwa alifanya interview ya kwanza ya kazi hiyo hiyo hakufanya oral..so anaitwa ili amalizie..mfano madereva na masekretari..
 
utumishi bado ni chombo ninachokiamini kwa ajira za watoto wa wakulima...hakuna upendeleo..idara hii ipo smart..kikubwa vijana tujiweke.sawa kwa interview sio kuamini ulichokifanya ni sahih wky hata maandalizi ni poor
 
bro acha ujinga matokeo ya oral hayajatoka na mshkaji hakufanya written......
 
brother m co mjinga kiasi hicho written tulifanya 16 tu...kwa hyo tukawa tunafahamiana coz tulikaa chumba kimoja.......kushindwa oral co sababu ya kushindwa kusema ukweli

Watu 16 written? Tangu lini utumishi wakawafanyisha written interview watu 16
 
wewe usijisumbue kwenda PCCB wale wananuka na siwapendi kabisa, tulifanya interview pale PCCB kwenyewe wameitwa watu kwenye ajira wanane ambao kwa hakika hawakuwa shortlisted na siwajui kabisa,na tulipeleka malalamiko tukachinjiwa baharini hakuna aliyethubutu kuwafuatilia kwani mwisho wa siku tukaambiwa ni watoto na wajomba za watendaji wa serikali na wafanyakazi wa PCCB, aidha kuna mmoja alikuwa anatamba kwa kumwambia rafiki yake tunayefahamiana kuwa alikuwa anasoma CPA hajaamua aende depo au lah lakini mwisho wa siku amekwenda na yuko kazini sasa, kwa ufupi serikalini pameoza kabisa na tunahitaji mabadiliko kibao,nilikuwa kwenye interview hiyohiyo na masters yangu eti mtu ananiuliza nitaje majina ya mawaziri 10 waliowahi kushika wizara ya mali asili na utalii, then nitaje sababu zilizofanya waondoke wote,afu mtu anakuzomea palepale.
 
huna haja ya kutishika kaka, nilihudhuria interview ya tpsc mwezi mei mwaka huu. watu tuliokuwa shortlisted tulikuwa 6 lakini tuliofika tulikuwa 3, maya zaidi wakaja wengine 2 ambao hawakuwa shortlisted kwa maelezo kuwa wameruhusiwa, it seems walikuwa na vimemo vya wakubwa...
Trust me hakuna mmoja wao alipata hyo kazi, niliitwa peke angu kazini!! sometimes watu kama hao unakuta wamepewa vimemo wanaenda zaidi ya interview moja, so usife moyo..lolote laweza kutokea
 
tuliitwa 35 tukaenda 16...walitaka kuanzia gpa ya 3.5 na zaidi kwa wa2 wa IT, STATISTICS, MATHS....yawezekan wa2 waliidharau,,,,
 
Back
Top Bottom