Utrafiki Mwanza ni dili?

Utrafiki Mwanza ni dili?

Entim

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2013
Posts
4,024
Reaction score
2,271
Wanajamvi,mpeleke mwanao CCP Moshi akasomee utrafiki! naletahii kero na RPC Mwanza utusaidiehili.Leo nimekodi canter toka mwanza kwenda misungwi kwa TSH 70,000/=kubeba mifuko 35 ya cementi. Trafiki wa kwanza alitupiga mkono maeneo ya city center(Kenyataroad) akadai tumtoe hela ya kahawa tukampa… kituo cha relini tukawakuta kikosi cha matrafiki4 wakakagua na kudaihaina spring wakapewa elfu 10, nyegezi wakapiga mkono na kusema tairizimeisha, naye alidai hela.Nyashishi kamakawa lazima uwashike mnkono elfu 5 hadi10 uwe na kosa usiwe na kosa lazima uwatunze kituo cha mwisho kabla ya misungwi nao wakatukaba tuwatoe chochote.Toka mwanza –Mwanza ni km 40 tu,
My take….jamani ukitaka utajiri wa haraka mpeleke mwanao CCPMoshi akasomee utrafiki.

 
Mkuu kama hao Trafiki walikukera basi ungelipa faini ili wasiipate pesa yako.

Kwanza umeshiriki kutoa rushwa...
 
Ninadhani ujumbe wako unawafaa zaidi Wazazi wa Watoto waliofeli Kidato cha Nne au Sita kwa sababu sijawahi kusikia au kuona mwenye ushindi wa Division I, II au III akienda CCP!

Hata hivyo Watu wenye tabia kama yako ya kutumia magari mabovu, kutoa vi-rushwa vya ovyoovyo kisha kutumia Mitandao ya Kijamii kulalamika ni janga kwa Taifa.

Ni mawazo yangu tu!
 
Hapana, Ndg Machina veterani ukisema kuwa waliofeli shule wako polisi sio hvyo, siku hz hali imebadilika,,,
 
Hapana, Ndg Machina veterani ukisema kuwa waliofeli shule wako polisi sio hvyo, siku hz hali imebadilika,,,

Nafuta kauli, naomba msamaha kwako na kwa wote wataokuwa wameathirika kwa kauli hiyo! Ingawa kwa tabia za Polisi, hasa wa Barabarani, sitomshauri mwanangu aende CCP - ni fedheha kuombaomba rushwa za buku, buku 2, buku 5, n.k!
 
Ninadhani ujumbe wako unawafaa zaidi Wazazi wa Watoto waliofeli Kidato cha Nne au Sita kwa sababu sijawahi kusikia au kuona mwenye ushindi wa Division I, II au III akienda CCP!

Hata hivyo Watu wenye tabia kama yako ya kutumia magari mabovu, kutoa vi-rushwa vya ovyoovyo kisha kutumia Mitandao ya Kijamii kulalamika ni janga kwa Taifa.

Ni mawazo yangu tu!
Mkuu inaonekana unaishi karne iliyopita !Siku hizi nafasi kama hizo ni ngumu sana sidhani kama mwenye 4 anaweza chukuliwa unless uunganishwe na kigogo ama mlungula mrefu sana!


Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Sio kushiriki kutoa rushwa usipotoa wanakugandisha hata masaa 5 wanaendelea na kupokea rushwa kwenye magari mengine. Me yameniluta kama hayo na zaidi ila nasubiri kesi iishe ndio niweke post yangu coz hawa jamaa hawafai niwewapania kuwachana sana hata kuwashikisha hela ya takukuru kama j3 watanizingua
 
Hata Arusha ni deal kubwa sana, trafic wako vizuri kwa siku mtu anakusanya laki2-3 haya ni mambo ya kawaida sana, traffic police wananunua magari mapya kila saa kila siku, kumiliki daladala 5-10, toyo10-20, nyumba za kupanga vitu vya kawaida sana lkn wao wanaishi kwenye vijumba vyao vya polisi.
Traffic police wamegeuka ni wafanyabiashara, wakusanya hela kwa nguvu barabarani za kutia ndani ya matumbo yao. Wanagawana kuanzia kwa wakubwa mpaka hawa wadogo.
Gari iwe ina kosa haina kosa hela lazima utoe
 
hawa askari wa usalama barabarani ni wasumbufu sana hata kama gari ina kosa dogo ambalo linahitaji elim wao ni hela tu yani wamekaa kibiashara zaidi kuliko kazi sio mwanza tu ni tanzania nzima ndio maana utakuta wengi ni watoto wa vigogo yani mtu katoka depo moja kwa moja anapewa utrafiki mie naomba kumuuliza mohamed mpinga kamanda wa usalama barabarani kazi hasa ya trafik ni ipi je ni kukaa barabarani na kusimamisha kila gari linalopita na kuomba kadi ya gari na leseni au?na cha pili kwanini mtu anapoamua kulipa faini akiomba ile risiti ya njano official receipt anapewa vitisho au anaambiwa tutakuongezea kosa hilo limeshawahi kutokea pale stand ya buzuruga kwahiyo mie naishauri wizara ya mambo ya ndani vituo vyote wapewe machine za EFD na wale ambao wanatembea vile vitabu vya faini wapewe zile machine ndogo za efd kama wanazotumia kampuni ya coke cola nafikiri zitakua ni efd mobile
 
Haaaa hizo mashine za efd itakuwa ngumu itakuwa ni kama tukienda madukani huku dar unaambiwa bidhaa inauzwa 50 ila ukitaka na risiti hizo efd bei inaongezeka hadi 60 na watanzania tunavyopenda vya bei rahisi unakubali coz unaona hiyo risiti huna kazi nayo.
 
Back
Top Bottom