Utoto wa miaka ya 80's-90's ulikuwa raha sana

mpasta

JF-Expert Member
Jan 17, 2011
917
1,997
Nikiwa Home nikiwaangalia watoto wangu naona kama utoto wao hauna kashikashi nyingi kama enzi zangu. Nikikumbuka enzi zile malezi yake kama jeshini vile..na taarifa nyingi tulikuwa tunafichwafichwa.

Mfano


(1) Akizaliwa mtoto Home, mnadanganywa mama ameenda kumnunua mtoto hospitali.

(2) Shuleni likipita gari la msalaba mwekundu, mwanafunzi mmoja akapiga yowe Mumianiiiii, nyonya damuuu, basi siku hiyo shule hamna masomo tena ni mbio kila kona.

(3) Kuna siku tulifungiwa maandazi kwenye gazeti la lugha la kiarabu mbaba mmoja akatutisha msile mtakuwa vichaa hiyo ni QURAN hiyo tukayatupa maandazi

(4) Mkitaka mpira wa miguu basi inabidi mkaokote Lylon kwenye maduka ya wahindi mtengene mpira ndio mcheze.

Lakini hawa Makamanda wetu wa Kidigitali Daah mambo yao soft sana, mpira wanataka uwanunulie dukani, hawajui hata Manati kazi yake nini, hata kuchomwa na miba za mbigiri miguu haziwachomi kutwa wamevaa viatu, hata mafunza miguuni hayawaingii.
 
Kipindi hiko mama akipika ugali mnawekeana zamu ya kukwangua ukoko sufuria..mama anaweka mchuzi kisha unasubiri ukoko ulainike kisha ukwangue,Ila siku yako ya kukwangua sufuria na vyombo zamu yako kuosha

Zamani Raha sn
OLD IS GOLD KWA KWELI
 
Utoto wa zamani ndio ulikuwa shida. Wa sasa hivi ndio Raha.
TV, Internet,school bus, breakfast za kisasa nk nk nk
Sisi tulisota hasaa. Lkn "uzur" wa utoto wa sasa umekuja na madhara mabaya MNOO...Bora wa utoto wa zaman.

*tough times create strong men..
strong men create easy times...
easy times create weak men weak men create tough times*
 
Iko wapi siku hizi :-

Michezo ya kukimbizana kwenye miti.

Kombolela.

Kifimbo cheza.

Findo gonoka(ukikutwa umeinama unapigwa buti la makalio).

Kwenda kuwinda (hapo ni full mbwa na manati)

Kutengeneza gari za mabua/mabox au waya.

Kulikuwa kuna mchezo wa kubuluza makalio kwenye Simba maalumu lililochorwa chini na mtu anakurushia mpira (hii tumechapwa sana kwa kumaliza kaptula kwenye makalio)

Tiari bado.

Ukuti .

Kutengeneza matoto ya udogo au Magari ya udongo.

Na nyingine nyingi.

Watoto wa siku hizi wanawekewa cartoon wakicheza sana wanaishia kombolela tofauti na hapo analetewa mamidoli ya kuchezea
 
Utoto wa zamani ndio ulikuwa shida. Wa sasa hivi ndio Raha.
TV, Internet,school bus, breakfast za kisasa nk nk nk
Sisi tulisota hasaa. Lkn uzur wa utoto wa sasa umekuja na madhara mabaya MNOO...Bora wa utoto wa zaman.

*tough times create strong men..
strong men create easy times...
easy times create weak men weak men create tough times*
zile kashikashi ndio raha yenyewe sio hawa Bloiler hawa wa kufuatwa na gari za shule hawana raha yoyote
 
Enzi hizo TV mnaangalia wikiend kwenye Banda la video tena inatoka mjini,Leo TV kila nyumba

Kuna siku mnakaa mnaamua kuhadithiana muvi za kina anord ya Jeni au komando kipensi,au jet li na maiko(tai chi ) alafu msioiona mnakuwa makini kusikiliza😅..leo nikienda Kwa bro watoto wake wakiniona wanalilia niwape simu wacheze gemu,dah namaind sn

Ukiwa na gazeti la sani unaenda nalo skuli Kisha anapewa mtu mmoja anayesoma vizuri anawasomea huku mmemzunguka..enzi hizo kina kipepe,sokomoko,mapung'o,ndumilakuwili,madenge wanatamba na wengi wetu hizi katuni tukidhani ni watu halisi na wanaishi dar
 
Iko wapi siku hizi :-

Michezo ya kukimbizana kwenye miti.

Kombolela.

Kifimbo cheza.

Findo gonoka(ukikutwa umeinama unapigwa buti la makalio).

Kwenda kuwinda (hapo ni full mbwa na manati)

Kutengeneza gari za mabua/mabox au waya.

Kulikuwa kuna mchezo wa kubuluza makalio kwenye Simba maalumu lililochorwa chini na mtu anakurushia mpira (hii tumechapwa sana kwa kumaliza kaptula kwenye makalio)

Tiari bado.

Ukuti .

Kutengeneza matoto ya udogo au Magari ya udongo.

Na nyingine nyingi.

Watoto wa siku hizi wanawekewa cartoon wakicheza sana wanaishia kombolela tofauti na hapo analetewa mamidoli ya kuchezea
Dah naona wazee watarajiwa unatukumbusha mbali sana maana sio mchezo tumekua kibabe sana
 
Iko wapi siku hizi :-

Michezo ya kukimbizana kwenye miti.

Kombolela.

Kifimbo cheza.

Findo gonoka(ukikutwa umeinama unapigwa buti la makalio).

Kwenda kuwinda (hapo ni full mbwa na manati)

Kutengeneza gari za mabua/mabox au waya.

Kulikuwa kuna mchezo wa kubuluza makalio kwenye Simba maalumu lililochorwa chini na mtu anakurushia mpira (hii tumechapwa sana kwa kumaliza kaptula kwenye makalio)

Tiari bado.

Ukuti .

Kutengeneza matoto ya udogo au Magari ya udongo.

Na nyingine nyingi.

Watoto wa siku hizi wanawekewa cartoon wakicheza sana wanaishia kombolela tofauti na hapo analetewa mamidoli ya kuchezea
DAAAH hiyo FINDO GONOKA aisseee tukiita KIZIBA kuna siku nusura mtoto mmoja atumbukie kisimani, alikuwa anachota maji ameinama kaja mwenzake kamzibua teke la matako
 
Utoto wa zamani ndio ulikuwa shida. Wa sasa hivi ndio Raha.
TV, Internet,school bus, breakfast za kisasa nk nk nk
Sisi tulisota hasaa. Lkn "uzur" wa utoto wa sasa umekuja na madhara mabaya MNOO...Bora wa utoto wa zaman.

*tough times create strong men..
strong men create easy times...
easy times create weak men weak men create tough times*
Nakazia " Tough times create strong men..
strong men create easy times... easy times create weak men, weak men create tough times"
 
Utoto wa zamani ndio ulikuwa shida. Wa sasa hivi ndio Raha.
TV, Internet,school bus, breakfast za kisasa nk nk nk
Sisi tulisota hasaa. Lkn uzur wa utoto wa sasa umekuja na madhara mabaya MNOO...Bora wa utoto wa zaman.

*tough times create strong men..
strong men create easy times...
easy times create weak men weak men create tough times*
Hizo starehe zinawagharimu watoto wa siku hizi.Wanapata uzito mkubwa wa miili,akili hazichangamki,hapati wasaa wa kuchanganyika na wenzake,ukakamavu wa miili hola,hawajui kuosha hata vyombo vya chakula tu.
Si hivyo tu,bali ubunifu wa kuchonga,kubumba,kuwinda maporini(vichakani na nyikani),uvumilivu(hata kwa kugongwa makwenzi tu)hawana.Ni meengi mnoo wanayakosa.Hata kujifunza ubondia tu hawana kwenye vile viwanja tuliviita viwanja vya dhambi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom