Utofauti wa Dr Magufuli na Lowassa

Utofauti wa Dr Magufuli na Lowassa

Jamar Said

Member
Joined
Sep 2, 2015
Posts
19
Reaction score
35
Ni ukweli usiopingika kuwa Lowassa anajaza watu kwenye mikutano yake. Lakini katika siasa kinaangaliwa pia ubora wa mikusanyiko hiyo. Mikusanyiko ya Lowassa inaleta kumbukumbu za Mh Mrema mwaka 95, si kwamba Watanzania hawaelewi somo. Kuna watu aina mbili wafikao mkutanoni, kwa mfano: kuna wanaokwenda mkutanoni kumuangalia huyo Lowassa mwenyewe kwa macho yao na pia kuna wanaokwenda kuchambua sera za wagombea. Kwa sasa Lowassa hajawa na jipya la kuwaambia watanzania na kuwapa matumaini halisia.

Ukweli Lowassa, hata kama Watanzania wangekua hawajaamka na wakafanya makosa kumchagua, Lowassa kwenye moyo wake angelimuhitaji Magufuli amsaidie kuendesha Serikali ili kazi ya kweli ya kujenga nchi na watu wakaiona inafanyika inavyotakiwa iwe. Hata hivyo Watanzania wengi ambao ni wapiga kura vilevile hufikiria kama Lowassa, Wanamtazama Magufuli kuwa kwa sasa ndio mtu wa kwenda kunyoosha mambo.

Sasa kuna kikwazo gani cha Watanzania wenyewe kumchagua Dr John Pombe Magufuli kwa maana katangaza nia thabiti ya kuikomboa nchi ya Tanzania. Kuna ambao hawapendi kiongozi mwadilifu na mfuatiliaji, lakini kwa mtu wa kawaida kama mimi ninaeishi Tandahimba na kwa kuwa tuko wengi tunaomuona huyu Magufuli kuwa ndiye atakaekua mkombozi wa kweli kwa wanyonge wa nchi hii, basi kura yangu ni yeye. AMENI
 
Hata kama Lowassa akijitokeza hadharani akasema" Kweli mimi ni fisadi/mwizi niliiba"
HATUTAKUBALI tutajua AMENUNULIWA!!


Tutampa KURA Hata mfanyeje?
 
Sera za ccm hazichambuliki.moja ni hizo hizo kila mwaka pili watanzania hawapo hivyo.kilichopo kwa watz ni uchovu.wamechoka na ccm na wapo tayari kuchagua mavi na kukiepuka choo cha u mma.najua wajua uchafu wa vyoo vya umma naomba kuwasilisha.
 
utofauti wao
1. Mmoja kashtuka kakimbia kutoka chooni, Mmoja kaendelea kubaki na maelfu wako chooni
2. Mmoja anamwaga sera, Mwingine anaishia kulalamika tu wakati chama lake ndio liko madarakani
3. Mmoja anachukia umaskini, mwingine anaupenda umaskini hadi kufikia kuhonga vimada vyake nyumba za serikali
4, Mmoja ni mabadailiko mwingine ni Pombe (kwa tunaompenda MUNGU TUNAJUA POMBE ILIVYO MACHUKIZO MBELE ZA MUNGU)

Ntarudi badae, ngoja ninywe chai kwanza,
 
Hakuna kingozi yeyote atakaeleta mabadiliko akiwa ndani ya CCM kwisha.
Mabadiliko ya kweli yatapatikana nje ya CCM.
VOTE FOR UKAWA,
VOTE FOR LOWASA.
 
Sijui watu hawafikirii,je mnakumbuka mwaka 2005,watu tulikuwa na imani kubwa na kikwete na alituhaidi mengi,na watu wakasema ili ni chaguo la mungu,je kafanya nini?,magfuli sawa ni mtenda kazi ila uko ndani ya ccm mfumi wao ndio unaowaangusha,so la msingi ni KUPIGA CHINI CCM.ili kuwepo na mabadiliko
 
Ni ukweli usiopingika kuwa Lowassa anajaza watu kwenye mikutano yake. Lakini katika siasa kinaangaliwa pia ubora wa mikusanyiko hiyo. Mikusanyiko ya Lowassa inaleta kumbukumbu za Mh Mrema mwaka 95, si kwamba Watanzania hawaelewi somo. Kuna watu aina mbili wafikao mkutanoni, kwa mfano: kuna wanaokwenda mkutanoni kumuangalia huyo Lowassa mwenyewe kwa macho yao na pia kuna wanaokwenda kuchambua sera za wagombea. Kwa sasa Lowassa hajawa na jipya la kuwaambia watanzania na kuwapa matumaini halisia.

Ukweli Lowassa, hata kama Watanzania wangekua hawajaamka na wakafanya makosa kumchagua, Lowassa kwenye moyo wake angelimuhitaji Magufuli amsaidie kuendesha Serikali ili kazi ya kweli ya kujenga nchi na watu wakaiona inafanyika inavyotakiwa iwe. Hata hivyo Watanzania wengi ambao ni wapiga kura vilevile hufikiria kama Lowassa, Wanamtazama Magufuli kuwa kwa sasa ndio mtu wa kwenda kunyoosha mambo.

Sasa kuna kikwazo gani cha Watanzania wenyewe kumchagua Dr John Pombe Magufuli kwa maana katangaza nia thabiti ya kuikomboa nchi ya Tanzania. Kuna ambao hawapendi kiongozi mwadilifu na mfuatiliaji, lakini kwa mtu wa kawaida kama mimi ninaeishi Tandahimba na kwa kuwa tuko wengi tunaomuona huyu Magufuli kuwa ndiye atakaekua mkombozi wa kweli kwa wanyonge wa nchi hii, basi kura yangu ni yeye. AMENI

huu upumbavu kamtongozee mkeo sio sisi.
msitufanye watanzania mazuzu kias hcho
 
Sema analalamika harufu ya choo cha public na ajabu hataki toka huko chooni. Sio tu kuvimbiwa, ataugua sana.
 
Kwani magufuli analipi jpya?? Porojo kama zile za jk tu! Ndiyo maana ile kauli mbiu ya maisha bora kwa kila mtanzania haijaweza kugusiwa maana imekuwa maumivu kwa watanzania, magufuli yupo kwenye mfumo ule ule na watu wale wale bado hapo dhana ya ukombozi haitatimia! Tunahtaji mabadliko japokuwa mgombea wa upinzani katoka ccm, tunaamini upinzani Una mfumo bora utakaleta maendeleo ya uhakika ambayo yamekuwa yakitafutwa na wengi kwa miaka zaidi ya 50 ya uhuru! Ccm sasa baaaaaaaaaaaaac mfuate mwenzio KANU!!!
 
Join Date : 2nd September 2015
Posts : 2
Rep Power : 0
Likes Received 0
Likes Given 0

Karibu Jamii Forums
 
ccm wameahidi vitu vingi sana kwa miaka hamsini ila wameshindwa kutimiza bora hata enzi za mwalimu kidgo aliweza kusomesha wanafunzi bure licha ya umaskini mkubwa kipindi hicho,sasa ccm hawawezi kunidanganya tena na ngonjera za magufuli
 
Ni ukweli usiopingika kuwa Lowassa anajaza watu kwenye mikutano yake. Lakini katika siasa kinaangaliwa pia ubora wa mikusanyiko hiyo. Mikusanyiko ya Lowassa inaleta kumbukumbu za Mh Mrema mwaka 95, si kwamba Watanzania hawaelewi somo. Kuna watu aina mbili wafikao mkutanoni, kwa mfano: kuna wanaokwenda mkutanoni kumuangalia huyo Lowassa mwenyewe kwa macho yao na pia kuna wanaokwenda kuchambua sera za wagombea. Kwa sasa Lowassa hajawa na jipya la kuwaambia watanzania na kuwapa matumaini halisia.

Unadhani tunahitaji jipya? La hasha! Tunamuhitaji Lowassa as a person.

Mmezoea muwe mnaiba nyinyi tuuuuuuu, sasa kaeni kitako muona namna inavyouma kuibiwa.
 
ccm wameahidi vitu vingi sana kwa miaka hamsini ila wameshindwa kutimiza bora hata enzi za mwalimu kidgo aliweza kusomesha wanafunzi bure licha ya umaskini mkubwa kipindi hicho,sasa ccm hawawezi kunidanganya tena na ngonjera za magufuli

Kufuli za nini babu wakati hata nyumba zenyewe hatuna? Nyumba waliuziana wao wenyewe, sisi watuuzie makufuli, humo simo.

images
 
Vyama vyote viwili CHADEMA na CCM vinaimba wimbo mmoja wa MABADILIKO,Watanzania tusidanganyike hata kidogo mabadiliko yanapatikana nnje ya CCM.CCM ni walaghai sana
 
Mtu mmoja hawezi kuleta mabadiliko. Rais ni taasisi, sio mtu mmoja. Kwa hiyo hata huyo mgombea wao ni mzuri kiasi gani, lakini ukweli ni kwamba kazungukwa na wapigaji, warafi na wabinafsi. HATUWEZI KUMPA KURA ZETU MWAKA HUU. Tuliwaamini kwa miaka mingi iliyopita, lakini wameshindwa!!!
 
Back
Top Bottom