Uthibitisho: Magufuli hauziki

Uthibitisho: Magufuli hauziki

Determinantor

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
61,201
Reaction score
99,939
Sina maana mbaya kusema hili ila napenda Watanzania wajue tu kwa faida ya pekee.

Mgombea Urais kwa Ticket ya CCM jana alikuwa Dar huko Mbagala lakini hakukua na media coverage yeyote na leo hii pia kwenye magazeti habari yake haikuwa na umuhimu wowote ukiacha magazeti yao!

Leo ninavyoandika hapa ukiwauliza ni Wangapi wanajua kuwa Magufuli alifanya mkutano jana nakuhakikishia wengi watasema hawajui!

I stand to be corrected, hivi sivyo ilivyotakiwa kuwa. Na hapo mbeleni CCM mtakua na kipindi kigumu sana sana kumnadi mgombea wenu.

Mkutano wa jana ilikua kama wa Segere au mdundiko tu. Poleni sana,. Wote akili na maskio yalikua Ukawa maana ndio habari ya mjini.
 
magufuli ni mwepesi pamba ina afadhali ! fuatilia jimboni kwake utashangaa ! kapigwa hadi mtaa anaoishi .
 
Sina maana mbaya kusema hili ila napenda Watanzania wajue tu kwa faida ya pekee.

Mgombea Urais kwa Ticket ya CCM jana alikuwa Dar huko Mbagala lakini hakukua na media coverage yeyote na leo hii pia kwenye magazeti habari yake haikuwa na umuhimu wowote ukiacha magazeti yao!

Leo ninavyoandika hapa ukiwauliza ni Wangapi wanajua kuwa Magufuli alifanya mkutano jana nakuhakikishia wengi watasema hawajui!

I stand to be corrected, hivi sivyo ilivyotakiwa kuwa. Na hapo mbeleni CCM mtakua na kipindi kigumu sana sana kumnadi mgombea wenu.

Mkutano wa jana ilikua kama wa Segere au mdundiko tu. Poleni sana,. Wote akili na maskio yalikua Ukawa maana ndio habari ya mjini.

Walirusha live Azam two
 
Hizo porojo tu. Tutasikia Mengi mwaka huu...na ukweli utabaki palepale.
 
Yaani hii nchi cjui nani kailoga na watu wake

Yaani tumesha sahau
ESCROW
EPA
RICHMOND
KAGODA
BUZWAGI
MEREMETA
TEMBO KUUAWA
TWIGA KUPANDA NDEGE
MISAMAHA YA MADINI
MISWADA YA HOVYO YA GESI NA MAFUTA
KUPANDISHWA HOVYO BEI YA MAFUTA
WATOTO KUKAA CHINI

AKINA MAMA KUZALIA CHINI


MATAJIRI KUTHAMINIWA

UBOVU WA BARABARA

UBOVU WA RELLI

UHABA WA MAJI SAFI NA SALAMA

KUUZWA BENKI YA TAIFA

KUUZWA KWA SHIRIKA LA NDEGE


KUUZWA KWA NYUMBA ZA TAIFA

KIWIRA COAL MINE

UKOSEFU WA DAWA HOSPITALI ZA UMMA

KUSHUKA KWA ELIMU

MIGOMO YA WAALIMU NA MADAKTARI

MIGOMO YA WANAFUNZI

MIGOGORO YA ARDHI KUTOKANA NA SERIKALI KUWATHAMINI WAWEKEZAJI WA KIGENI

KUHODHI VIWANJA VYA MICHEZO

KUHODHI MAJJENGO YA UMMA

KULINDA WEZI, MAFISADI NA WAHUJUMU UCHUMI

KUUA VIWANDA ALIVYO VIJENGA MWALIMU NYERERE

KUUA MASHIRIKA YA UMMA

KUONGEZA MATABAKA KWA WANANCHI

KUUA WANAHARAKATI NA WAANDISHI WA HABARI ( MWANGOSI)

KUPITISHA RASIMU ISIO YA MUAFAKA
ILIYO
FEKI

HIvyo basi,
nashangazwa na watu waelewa humu wanaosema magufuli jembe
Wakati yupo serikalini tangu 1995
Ndani ya ccm

Nani ametuloga ??

Hapa magufuli ni pombe ile ile kwenye chupa mpya.

Maskini Tz


Au elimu ya uraia tatizo ???
 
magufuli ni mwepesi pamba ina afadhali ! fuatilia jimboni kwake utashangaa ! kapigwa hadi mtaa anaoishi .

Wewe huzijui siasa za chato. Tatizo ni mahindi ya msaada. Viongozi waandamizi wa ccm waliandikisha majina watu, then mahindi yalivyokuja walienda kuyauza sokoni, wananchi ndicho kilochowakasirisha. Ila magufuri anapendwa sema hao viongozi wa mitaa wa ccm ndiyo wananchi walifanya hivyo kuwakomoa
 
Nasema Magufuli hauziki na kwa namna yeyote ile CCM watapoteza tu
 
Back
Top Bottom