Utekelezaji Ilani ya CCM - ITV

Utekelezaji Ilani ya CCM - ITV

Goodrich

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2012
Posts
2,091
Reaction score
1,179
Kuna matangazo ya kipindi kitakachorushwa na ITV kuhusu utekelezaji wa ilani ya CCM.
Nimeamini kabisa ya kuwa hakuna cha kujivunia ambacho CCM na serikali yake imefanya tangu kuingia madarakani.
Maana katika matangazo hayo tu, wanaongelea miradi ya TASAF, mapambano ya Rushwa, na mengineyo ambayo ni ya utendaji wa kawaida kabisa wa kila siku wa serikali.

Ingetarajiwa waongelee mambo kama jinsi gani wameboresha sekta ya umeme, mtandao wa barabara, jinsi gani wameinua elimu ya msingi, sekondari nk, sekta ya afya, ajira, upitiaji mikataba ya madini na mambo kama hayo yenye muelekeo wa ki maendeleo.

Au basi kama ni ilani as it is, waingolee kama ilivyowekwa wazi na JK katika ahadi zake ikiwamo :
1. Kujenga reli mpya kutoka Dar es Salaam hadi mikoa ya Kanda ya Ziwa - Nzega, Tabora.
2. Mkoa wa Tanga kuwa Jiji la Viwanda - Tanga mjini.
3. Tabora kutumia maji ya Ziwa Victoria – Igunga.
4. Kulipa madeni ya chama cha Ushirika Mkoa wa Shinyanga (SHIRECU) – Shinyanga.
5. Kumaliza migogoro ya ardhi nchini – Dodoma.
6. Wakulima kuacha kutumia jembe la mkono - Dodoma mjini.
7. Kuwapatia trekta wakulima - Kata ya Mrijo, Dodoma.
8. Wananchi kutoondolewa kwenye Ranchi ya Misenyi – Kagera.
9. Kujenga Uwanja wa Ndege Misenyi – Kagera.
10. Kupanua Uwanja wa Ndege Bukoba - Bukoba Mjini.
11. Kujenga uwanja wa ndege mkubwa Kigoma - Kigoma Mjini.
12. Mtukula kupatiwa umeme kutoka Uganda – Kagera.
13. Mikoa ya Kagera, Kigoma, Lindi, Rukwa na Ruvuma kuunganishwa katika gridi ya taifa ya umeme – Kagera.
14. Kuimarisha Takukuru kwa miaka mitatu – Kagera.
15. Hukumu kwa waliopatikana na hatia ya kuua albino – Mbeya.
16. Kununua meli kubwa kuliko mv Bukoba – Kagera.
17. Kuanzisha benki ndogondogo kwa ajili ya wajasiriamali.
18. Serikali kuvisaidia vyama vya ushirika – Mwanza.
19. Kuimarisha usalama Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa kupeleka kikosi maalumu chenye vifaa kupambana na wahalifu – Mwanza.
20. Wilaya ya Geita kuwa hadhi ya mkoa Januari mwakani – Geita.
21. Kulinda Muungano kwa nguvu zote – Pemba.
22. Kuwajengea nyumba waathirika wa mafuriko Kilosa – Morogoro.
23. Kununua meli mpya kubwa Ziwa Nyasa - Mbeya mjini.
24. Kujenga bandari Kasanga – Rukwa
25. Kumaliza tatizo la walimu miaka mitano ijayo – Songea.
26. Kufufua mgodi wa makaa ya mawe Kiwira – Mbeya.
27. Kuzuia hatari ya Kisiwa cha Pangani kuzama – Tanga.
28. Kununua bajaji 400 kwa ajili ya kubeba wajawazito hasa vijijini – Iringa.
29. Kujenga barabara yenye kiwango cha lami kutoka Same hadi Kisiwani – Kihurio na kuiunganisha na barabara kuu ya Moshi-Dar es Salaam-Same mkoani Kilimanjaro.
30. Kumaliza tatizo la maji katika Wilaya ya Same - Same mjini.
31. Kuboresha barabara za Igunga-Tabora.
32. Kusambaza walimu 16,000 katika shule za sekondari zenye upungufu mkubwa wa walimu - Kisesa Magu.
33. Kununua vyandarua viwili kwa kila kaya - Mbeya mjini.
34. Kuzipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini kuwa za rufaa ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) - Hydom Manyara.
35. Kulinda amani nchini kwa kuzuia chokochoko za kidini, kikabila na kisiasa – Musoma.
36. Kulinda haki za walemavu – Makete.
37. Kujenga baabara ya Njombe - Makete kwa kiwango cha lami, urefu wa kilomita 109 - Iringa mjini.
38. Kujenga barabara Musoma-Mto wa Mbu Arusha – Arusha.
39. Kuanzisha Jimbo la Ulyankulu- Shinyanga mjini.
40. Kujenga barabara ya lami Manyoni-Kigoma-Kaliua, Tabora
41. Kukarabati barabara ya Arusha-Moshi - Arusha mjini.
42. Kuboresha barabara ya Hande
ni, Kondoa hadi Singida – Dodoma.
43. Kuwafidia wanakijiji ng’ombe waliopotea wakati wa ukame mwaka 2009 – Longido.
44. Vijiji vyote vilivyoko kilomita 15 kutoka kwenye bomba kuu la mradi mkuu wa maji wa Ziwa Victoria - Shinyanga-Kahama kuunganishiwa maji – Shinyanga.
45. Tatizo la umeme kufikia kikomo Novemba mwaka huu mkoani Arusha – Arusha mjini.
46. Kukopesha wavuvi zana za kilimo - Busekera, Wilaya ya Musoma.
47. Kuwapatia maji wakazi wa Wilaya ya Longido – Longido.
48. Kujenga barabara ya lami kupitia pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Seregenti – Ngorongoro.
49. Utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya kilimo kuwasaidia wafugaji kuweza kupata na kutunza mifugo yao vizuri - Mbulu mkoani Manyara.
50. Kusambaza maji nchi nzima - Babati vijijini.
51. Kusambaza umeme, utoaji wa huduma za afya, na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji na utoaji ruzuku kwa wakulima mwaka 2010-2015 - Babati vijijini.
52. Kuongeza mara tatu idadi ya wananchi wanaonufaika na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa mfumo wa vocha – Iringa.
53. Kuhakikisha Isimani inapata maji ya uhakika – Iringa.
54. Kuiwekea lami barabara inayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ambayo ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania – Iringa. 55. Kulinda usalama wa wananchi kwa ujumla ili kudumisha amani na sifa ya nchi –Ifunda.
56. Kutokomeza malaria 2015 - Bunda, Mkoa wa Mara.
57. Kuwapa wanawake nafasi zaidi - Kilolo, Iringa.
58. Ahadi kuisaidia Zanzibar kuendeleza miradi mbalimbali ya kijamii – Kibandamaiti, Mjini Zanzibar.
59.Kuipandisha hadhi hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar kuwa ya rufaa - Kibandamaiti mjini Zanzibar
60. Kuisaidia Zanzibar kila panapohitajika msaada – Kibandamaiti.
61. Serikali kujenga upya Bandari ya Mbamba Bay – Ruvuma.
62. Ununuzi wa meli mpya yenye uwezo wa kubeba tani 400 – Mbamba Bay, Ruvuma.
63. Kufufua chama kikuu cha ushirika cha wakulima wa Mbinga (MBICU) – Ruvuma.
64. Mtwara kuwa mji wa viwanda – Mtwara.
65.Ahadi ujenzi wa kwanda cha dawa ya kuua viluilui vya mbu – Kibaha.
66.Hospitali ya Tumbi kuwa ya mkoa – Kibaha.
67. Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha kutenga eneo maalumu la viwanda – Kibaha.

Tofauti na hapo wafanye kazi kwanza !
 
True, Yaani huo ndio ukweli.
Wafanye kazi kwanza kwa miaka miwili iliyobaki labda kitapatikana cha kujivunia.
Vinginevyo watajikuta wanaongelea miradi ya Malaria, MMEM, Mkukuta, Mkurabita, MMES ....................... ambayo ipo kimaandishi zaidi
 
Watanzania wazalendo wenzangu, mie ninachoshauri ni kufanya tu Mabadiliko 2014/2015. Tuachane na kupuuzia kabisa hizi ngonjera za ccm, Mabadiliko yana maana sana ktk kuziadabisha Serikali zilizopo Madarakani la sivyo tutakuja kujuta kama tukiendelea kucheka na Nyani, maana hata vizazi vyetu vitakuja kujuta kuzaliwa na sisi, hivi mafanikio haya wanayotaka kutupumbaza yana uwiano gani na Mashimo wanayotuachia Migodi mikubwa ya dhahabu? Kuna uwiano gani wa Maendeleo wanayoyatangaza na elimu kushuka hadi wastani wa std vii kufaulishwa kwa nguvu kwa wastani kushushwa hadi 40%?

Tafakari!
 
Watanzania wazalendo wenzangu, mie ninachoshauri ni kufanya tu Mabadiliko 2014/2015. Tuachane na kupuuzia kabisa hizi ngonjera za ccm, Mabadiliko yana maana sana ktk kuziadabisha Serikali zilizopo Madarakani la sivyo tutakuja kujuta kama tukiendelea kucheka na Nyani, maana hata vizazi vyetu vitakuja kujuta kuzaliwa na sisi, hivi mafanikio haya wanayotaka kutupumbaza yana uwiano gani na Mashimo wanayotuachia Migodi mikubwa ya dhahabu? Kuna uwiano gani wa Maendeleo wanayoyatangaza na elimu kushuka hadi wastani wa std vii kufaulishwa kwa nguvu kwa wastani kushushwa hadi 40%?

Tafakari!

Na kweli hizo ni ngonjera.
Ila ngonjera zao zinatugharimu sana kama taifa.
Wafanye kazi ya vitendo, sio bla bla wakati wao ndio wana serikali.
 
Wanatekeleza ilani kwenye TV, ama kweli, ada ya mja hunena lakini muungwana ni vitendo.
 
CCM hawana sera. Ahadi za Kikwete ni wajibu wa serikali ya chama chochote cha siasa kinachoshika dola. CCM wapo kwa gharama za ujinga wa wananchi walio wengi kwenye mambo ya msingi, otherwise wangeshatoweka zamani!
 
Just wondering ni nani analipia gharama za vipindi hivi kwenye tv/ radio- ni Serkali au Chama? Hii pia ni katika gharama za wanasiasa mikoani. Mwisho tupewe uchambuzi utakaoonyeha faida itakayopatikana vs gharama iliyotumika kwa wananchi kutokana na haya!
 
CCM hawana sera. Ahadi za Kikwete ni wajibu wa serikali ya chama chochote cha siasa kinachoshika dola. CCM wapo kwa gharama za ujinga wa wananchi walio wengi kwenye mambo ya msingi, otherwise wangeshatoweka zamani!

Ni kweli Mkuu Bartazari;

Ni kweli kabisa kwamba mtaji mkubwa wa ccm ni:

  1. Ujinga wa sisi Watanganyika
  2. Umasikini wa sisi Watanganyika tuliosababishiwa na mfumo wa Serikali ya ccm

Hakuna kitu ambacho ni cha kipumbavu kama kuimbiwa Ngonjera na Serikali ile ile iliyokuwepo tangu Nchi imepta uhuru wa Bendera, eti wametengeneza Barabara, wameleta maji, shule na Wamejenga Hospitali. Wadau kazi yoyote ya serikali inayokuwa madarakani inawajibika kuwaletekelezea Wananchi wake maswala hayo ya msingi, na huo ni wajibu wa lazima kwa kuwa wao ndio wenye majukumu ya kukusanya kodi hivyo kama ndo wenye ridhaa ya kukusanya kodi, vile vile ni lazima waboreshe huduma za lazima za ustawi wa jamii.

Kwa Mantiki hiyo mimi binafsi sioni kama yafuatayo ni mafanikio kwa serikali ya ccm ni jambo la kutupumbaza kwa miaka zaidi ya 50 waliyokaa Madarakani:-


  1. Ujenzi wa Barabara tena nyingi kwa Mikopo ya WB na ADB na misaada ya Wahisani
  2. Elimu ya kuongeza idadi ya Madarasa yasiyokuwa na hadhi ya watoto wetu kusomea ndani ya Nchi iliyona umri wa zaidi ya miaka 50 na rasilimali za kila namna, pamoja na sifa kwamba Serikali imejenga vyumba duni vya madarasa vingi visivyokuwa na huduma muhimu kama mashimo ya vyoo n.k, Watoto wa Darasa la Saba mwaka huu wamefaulishwa kwa alama 40% kutoka wastani wa 100%. Wadau maana rahisi hapa Elimu inashuka badala ya kupanda.
  3. Afya, Hospitali zilizojengwa wakati wa uhuru sasa hivi majengo yamechoka vibaya sana, pamoja na majengo kuchoka hata ile kupata paracetamol ama glooves za kuwasaidia akina Mama kujifungua ni ndoto. Na hata ukikuta kuna majengo mapya yaliyojengwa hivi karibuni, uliza uwiano wa Ghrama iliyotumika na ubora wa jengo lenyewe. Mfano jaribuni kufanya tafiti za Mochwari ya Hospitali ya Wilaya ya Geita iliyojengwa hivi karibuni haina hata Jokofu linalofanya kazi, yaani unakuta miili ya Ndugu zetu inatoa wadudu sakafuni.
  4. Maji, hadi miaka hii ya zaidi ya miaka 50 ya Uhuru ccm ikiwa madarakani, Watanzania zaidi ya 70% bado tunakunywa maji yasiyo salama yanayotokana na visima vifupi, mito na madimbwi yaliyotuama.
  5. Umeme, huu nao si wa uhakika hata kwa wale watanzania wasiozidi zaidi ya 13% waliobahatika kuupata kwa jasho zito.

Wadau kwa sababu hizo chache nilizoelezea hapo juu, ccm wana sababu zipi za kuendelea kuchezea akili zetu kulinganisha na muda wote huo tuliowapa dhamana ya kupanga ikulu?
Mimi nadhani mafanikio ya kutambia kama Serikali iliyokaa madarakani kwa zaidi ya Miaka yote hii bila kubadillishwa hata mara moja tena ikiwa na dhamana ya kusimamia rasilimali zote na misaada juu ingekuwa kama, Kufikia hatua ya kutoa Elimu bure, Afya bora kwa kila Mtanzania bure, Maji safi na salama kwa kila Mtanzania walau kwa zaidi ya 85% hadi sasa. Watanzania kuwa na uchumi wenye uwiano wa kipato cha moja kwa moja badala ya Uchumi unakua kumbe unakua kwa kuangalia kipato kidogo wanachowekeza Wawekezaji ukilinganisha na faida kubwa wanayotengeneza huku wakiwaacha Watanganyika na umasikini wa kutupwa.

Watanganyika, tafakarini kwa kina na msimamie maamuzi magumu katika uchaguzi ujao, na elimu hii ya kuwafumbua macho Watanganyika wajinga nikiwamo na mimi isiishie kwenye mitandao, kila Mtanganyika mwenye uchungu na Nchii yetu awe na jukumu la kuwaelimisha ndg zetu wasiokuwa na access na mitandao ajue cha kufanya uchaguzi ujao na kuachana propaganda hizi za kijinga za ccm.

Naomba kuwasilisha.
 
Just wondering ni nani analipia gharama za vipindi hivi kwenye tv/ radio- ni Serkali au Chama? Hii pia ni katika gharama za wanasiasa mikoani. Mwisho tupewe uchambuzi utakaoonyeha faida itakayopatikana vs gharama iliyotumika kwa wananchi kutokana na haya!

Sasa wana JF tufuatilie kipindi hiki, maana ni leo saa alhamisi 1.30 usiku, ili tujibu pumba zao !
 
ccm wamejitahidi kfunya kazi na kuboresha bei ya bidhaa muhimu mfano simenti imepanda kutoka 6000 hadi 16000, sukari kutoka sh 600 hadi 2400, bei ya bati kutoka 5400 hadi 15000, bei unga ngano kilo moja kutoka 400 hadi 1800. nk.

haya ni mafanikio makubwa ya kujivunia
 
ccm wamejitahidi kfunya kazi na kuboresha bei ya bidhaa muhimu mfano simenti imepanda kutoka 6000 hadi 16000, sukari kutoka sh 600 hadi 2400, bei ya bati kutoka 5400 hadi 15000, bei unga ngano kilo moja kutoka 400 hadi 1800. nk.

haya ni mafanikio makubwa ya kujivunia

Wakati JK anaingia madarakani bei ya Petrol ilikuwa TShs 1050 na sasa ni TShs 2100
Nauli ya daladala ilikuwa 150 na sasa ni 400
Bia ilikuwa TShs 1000 na sasa ni TShs 2000
Nishati ya umeme imepanda zaidi ya mara 2
Mbali ya hayo kiwango cha ufaulu kimeporomoka,

Tunatarajia waongelee masuala kama hayo leo saa 1.30 jioni
 
Kelele zote hizo ni bure tu. Kama uchumi wa mwananchi wa kawaida unazidi kudorora, basi wanapoteza muda tu. Ni sawa sawa na wale jamaa wa BOT na Statistics, wanapokuja na takwimu zao feki ilihali hali ya maisha ni ngumu! Wana Uchumi watudadavulie hapa!
 
wakuu, hivi maendeleo km yapo si wananchi wangeyafeel ktk maisha yao ya kila siku na sio hadi yatangazwe kwenye tv. ccm ni vilaza wa kutupwa. phuuuuuuu
 
Back
Top Bottom