Utaratibu ukoje kuhusu kupoteza laini ya simu?

Utaratibu ukoje kuhusu kupoteza laini ya simu?

Unahitaji loss report kwanza, halafu ndio uende nayo Tigo. Loss report zinapatikana kwenye tovuti rasmi ya polisi Tanzania
 
Huwa naona wengi wanaenda kwanza polisi wanafata maelekezo yote kisha wanaenda mtandao husika kukamilisha kurudishiwa laini
 
Nenda ofisi za Tigo, waelezee umepoteza line utapatiwa fomu utaijaza...Baada ya hapo ingia link hii http//lormis.tpf.go.tz ili kupata loss report, jaza taarifa zako kuhusu kupotelewa mali zako.

Kwa vile ni line na simu watakiwa ujaze loss report 2..Baada ya kuconfirm taarifa zako utapatiwa Control no.itumie kufanya malipo @ Tsh.500

Baada Needs malipo nenda kituo cha police wapatie hiyo fomu kutoka Tigo waoneshe na hizo taarifa ulizozijaza kwenye simu yako kwaajili ya kuapprove.Baada ya wao kuapprove print rudi Tigo shop urenew line yako.
 
Nenda kwa wale jamaa wa mitaani na kitambulisho chako mpe buku 5 unarenew line yako ndani ya dkk 5 unasepa ,kwenda polisi ni kupoteza mida

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Anaesema kwenda polisi in kupoteza mda simuungi mkono. Maaana huwezijua aliyekuibia ananiagani na wewe.
Mfano:tukio la kialifu limetokea kwa bahati mbaya laini yako ikaonekana hayo mazingira wewe unaweza kuwa mshukiwa mkuu wa hilo.

Mi nilipoteza simj kama week 2 zimepita nilienda tigo shop ya tegeta kibo nikapewa katatasi flani nikajaza nikaambiwa niende kituo cha polisi kawe au mbweni. Nikaenda mbweni nikaambiwa nikaripie hiyo lost report kwa wakala wa maxmalipo nikaenda nikapigwa buku jero ila kwenye form imeandikwa jero nikarudi kituoni wakaniulizia jinsi ilivyopotea nikajieleza pale basi . wakanipa form nyingine niarudi nayo tigo shop.nikarudisha lini na maisha yanasonga
 
Shukran
Nenda ofisi za Tigo, waelezee umepoteza line utapatiwa fomu utaijaza...Baada ya hapo ingia link hii http//lormis.tpf.go.tz ili kupata loss report, jaza taarifa zako kuhusu kupotelewa mali zako.

Kwa vile ni line na simu watakiwa ujaze loss report 2..Baada ya kuconfirm taarifa zako utapatiwa Control no.itumie kufanya malipo @ Tsh.500

Baada Needs malipo nenda kituo cha police wapatie hiyo fomu kutoka Tigo waoneshe na hizo taarifa ulizozijaza kwenye simu yako kwaajili ya kuapprove.Baada ya wao kuapprove print rudi Tigo shop urenew line yako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni vyema ukafanya utararibu wa kupata police loss report kwa kila kitu chako unachopoteza Ni muhimu Sana hata kama hukiitaji tena kitu hicho
 
Back
Top Bottom