Utapeli hatari waibuka kupitia mitandao ya simu

Utapeli hatari waibuka kupitia mitandao ya simu

comrade igwe

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2015
Posts
7,295
Reaction score
3,950
Kuna baadhi ya watu wasio waamininifu wenye lengo la kutapeli wameanza mtindo wa kutafuta namba mbalimbali za watu wengine na kuanza kusambaza ujumbe mbalimbali za kuwataka wawatumie fedha kwa haraka ujumbe unaweza kuwa hivi "Habari ile pesa nitumie kwenye namba hii anataja namba .......... nipo kwa wakala line yangu ya simu sijasajili M-pesa fanya haraka nipo kwa wakala" sasa kwa kufuatilia ujumbe huo ambao ni watu wengi wameshazipata na kubainisha kutomtambua mhusika wa ujumbe huo, ombi langu mamlaka ya mawasiliano Tanzania waanze kufuatilia hizo namba na hatimae kuwapata wahusika wa utapeli huu ili wachukuliwe hatua za kisheria.
 
Nimetumiwa ujumbe huo juzi, nilichomjibu anajua na Mungu wake...
 
Kuna baadhi ya watu wasio waamininifu wenye lengo la kutapeli wameanza mtindo wa kutafuta namba mbalimbali za watu wengine na kuanza kusambaza ujumbe mbalimbali za kuwataka wawatumie fedha kwa haraka ujumbe unaweza kuwa hivi "Habari ile pesa nitumie kwenye namba hii anataja namba .......... nipo kwa wakala line yangu ya simu sijasajili M-pesa fanya haraka nipo kwa wakala" sasa kwa kufuatilia ujumbe huo ambao ni watu wengi wameshazipata na kubainisha kutomtambua mhusika wa ujumbe huo, ombi langu mamlaka ya mawasiliano Tanzania waanze kufuatilia hizo namba na hatimae kuwapata wahusika wa utapeli huu ili wachukuliwe hatua za kisheria.
Hao hao unaowaomba msaada ndio waasisi wa huo utapeli
 
Sasa huyo tapeli anajuaje kua wewe unadaiwa pesa hadi adiriki kusema nitumie kwenye namba hii? Baado sjaelewa hapo inakuaje kuaje
 
Sasa huyo tapeli anajuaje kua wewe unadaiwa pesa hadi adiriki kusema nitumie kwenye namba hii? Baado sjaelewa hapo inakuaje kuaje
.Wanachofanya ni kubahatisha,meseji hyo inatumwa kwa watu wengi hata 100,sasa inafahamika kuwa kila dakika kuna watu wanafanya miamala kwenye mitandao ya simu na kuna ambao waliombwa au walikuwa wanamakubaliano ya kutuma pesa sehemu,so ikiwa wewe ulikuwa na mpango wa kumtumia mtu hela saa saba mchana,alafu saa saba kasoro inaingia mesej kwenye simu yako kuwa "ile hela nitumie kwenye namba hii chap,niko kwa wakala",hapo kwa mwenye akili zilizotoshana kichwani lazima atampigia simu muhusika kuthibitisha,sasa wengine eidha kwa uzuzu,ama kuvurugwa watatuma mpunga bila kuthibitisha,unaweza ukajiuliza nani anaweza kuwa mjinga kiasi hiko,mpaka kutapeliwa kizembe ivo,amini usiamini hao watu wapo,tena ni wengi balaa.
 
Sasa huyo tapeli anajuaje kua wewe unadaiwa pesa hadi adiriki kusema nitumie kwenye namba hii? Baado sjaelewa hapo inakuaje kuaje

Mkuu huo ndio unaitwa utapeli watu wanafikiri namba nyingi halafu anatawanya msg,mimi kidogo niingie mkenge kama sio kumfuatilia nikipiga simu haipokelewi wala msg hazijibiwi lakini ujumbe unaendelea kutumiwa tu daah
 
Akisema Mimi ni X Nitumie kwa hii no ya kwangu ina matatizo, mpigie X kama ni ukweli na usitume mpaka umuone ana kwa ana kwani sauti zinachongwa
 
Mimi niliingiziwa pesa kwenye account ya nmb, kiasi cha shilingi millioni3.
Wakati sina habari, maana hata sms haiku-display,.
Wakatokea jamaa wawili smart sana nyumbani kwangu, wakidai wao ni wauzaji wa kiwanja, sasa wametokea kwa jamaa yangu, ni rafiki yangu ambaye walisema yuko bize na mishe zake, wameelewana naye millioni 5, kapungukiwa mill2. Hivyo kutokana na tunavyoaminiana naye,
katupia kwenye akaunti yangu mill3 ili nimkopeshe izo2 kwa sababu kiwanja hicho kilikuwa na ushindani mkubwa,watu wengi wanakitaka, lakini hawajafikia bei!
Hao jamaa nadhani walikuwa ni wataalamu wa mawasiliano, sababu nilivyoingia chumbani ili nichat na jamaa yangu kuhusu mipango yake hiyo, simu zake zote zikawa hazipatikani.
Nikaona isiwe shida, nikakomandi pesa yote iliyokuwa kwenye account ya nmb iingie crdb.
Zoezi hilo lilishindikana kwa sababu pesa waliyokuwa wameitupia tayari walikuwa wameiblock.
Hivyo ukiangalia salio, kweli kiwango hicho kipo, lakini ukitaka kukifagia, kinakataa kwamba salio halitoahelezi!
Nilichokifanya baada ya kugundua kwamba "nimetembelewa", kwanza nilikasirika na ukichukia, kuficha hasira yataka akili kuigiza furaha na bashasha usoni, nilifanya hivyo, lakini walinisoma, nadhani kwa muda niliotumia chumbani kwa tryal mbalimbali.
Kwa upole wa kuigiza huku nikifikiria haraka haraka cha kuwafanya, niliomba twende kwa jamaa yangu kwa kuwa hapatikani kwenye simu.
Hao jamaa wakasema wao hawafanyi biashara za usumbufu.
Kama sitoi hiyo pesa, basi hiyo fursa ya kupata kiwanja cha chee, jamaa yangu kakosa.
Majibu hayo yanatolewa huku wakitoka nje ya compound kwa speed.
Dah! Nifanyeje sasa?
Nilipata majibu mengi kichwani hadi ya kuua, wakati huo jamaa wameishatokomea zao.
Nilichotaka kueleza kwamba, utapeli wa kwenye mtandao ni mkubwa sana kuliko tunavyodhania, usiamini maandishi kabla ya kujiridhisha.
 
Back
Top Bottom