Utafanyaje?...Ulimwacha mkeo na sasa..?

Utafanyaje?...Ulimwacha mkeo na sasa..?

JENDALUJEJE

Member
Joined
Nov 18, 2012
Posts
43
Reaction score
22
Ulikuwa na mke wa ndoa,mlipendana sana.....mliishi kwa miaka 4,2kabla ya ndoa na baada ya ndoa 2.

Katika muda huo,mkeo alishabeba mimba mara2 zikaharibika kwa tatizo la homorne........mkiwa katika kutafuta ufumbuzi wa kitabibu................ukawa unachepuka kwa mdada fulani..................ikasababisha mkatengana na mkeo.

Ulipoulizwa na wazazi ukadai hujawahi hata kutongoza tangu uoe.....wk mbili baada ya mkeo kuondoka yule bi mdada akaanza kukutembelea hme,mara anapika,mara anafua...ilimradi mbwembwe nyingi,baada ya miezi 2,mdada akadai "NINA MIMBA YAKO",akahamia kabisa!

Wazazi wakakusihi,mrudishe mkeo,ukadai "HUYU MTOTO ATAKAYEZALIWA ATAHITAJI MAPENZI YA WAZAZI WAWILI"..........ukamtwanga talaka mkeo,ukatuma posa kwa mdada na mahari juu.Ukauza kiwanja ulichonunua na mkeo na kuanza ujenzi fasta kwenye kiwanja ulichumnunulia mdada kwa madai unamwandalia mtoto.

Siku za nyuma ulishapata wasiwasi kuhusu mtoto huyo,ukazuka ugomvi mkubwa,mama mkwe wako akaja fasta toka kijijini kuamua kesi,ukaendelea kuishi na binti yake.

Tangu alipozaliwa huyu mtoto, mdada aliweka vijiti vya uzazi wa mpango,akidai mpaka mfunge ndoa ya kanisani na vigelegele kama uliyofunga na mkeo wa kwanza,ndio atazaa mtoto wa pili!

Mkeo alishakubembeleza myamalize ukagoma,nduguze wamemshauri atafute mwanaume mwingine azae naye,amegoma.....anasema anataka aone mwisho wako!

Mtoto alipofikisha miaka 4,anajitokeza njemba,tena ya mtaani mlipohamia(nyumba alitafuta huyo mdada,hapakuwa na dalali) na kudai mtoto ni wake na anamtaka.Mbaya zaidi sura ya mtoto ni copy right na huyo jamaa.Siku za nyuma,shemejio(binamu na mkeo mpya,ambaye ndie anayemlea mtoto huyo)aliwahi kukuuliza, "HIVI SHEMEJI UNAMWONAJE "JINA LA MTOTO"?.....kafanana na nani?akamalizia na kauli....MJINI HAPA!Mwanamke akiulizwa,anajibu..."Fanya maamuzi yoyote kama unahisi si mtoto wako"

Ndugu wote walishakususa,na hakuna anayekutembelea,wanakuja ndugu wa mke tu,yaani uko bize upande wa ukweni.......mke mpya alipigwa stop na wifi zake,asikanyage kijijini kwenu,nawe ukajibu kwa mbwembwe......ulishaamua hurudi nyuma!

Nimejitahidi kufupisha..............
Hebu wadau toeni msaada,wapi pa kuanzia jamani........yamemtokea ndugu yangu kabisa,sasa kawa kama amechanganyikiwa.



 
Akapime DNA, kama mtoto ni wake aendelee kumtunza na aachane na ndugu waliomtenga, afanye kazi kwa bidii awe na noti ndugu watarudi tu, pesa si mchezo, kama itabainika mtoto si wake basi ampige chini mama na mtoto wake halafu akamuombe msamaha mke wa awali, kila mtu huishi maisha yake ili mradi yawe yanamfurahisha.
 
Akapime DNA, kama mtoto ni wake aendelee kumtunza na aachane na ndugu waliomtenga, afanye kazi kwa bidii awe na noti ndugu watarudi tu, pesa si mchezo, kama itabainika mtoto si wake basi ampige chini mama na mtoto wake halafu akamuombe msamaha mke wa awali, kila mtu huishi maisha yake ili mradi yawe yanamfurahisha.

Dalili zote zimeshaonyesha kuwa mtoto si wake......na kumbe sakata hilo lilikuwepo tangu mtoto alipozaliwa tu.....naye anakiri hilo japo inamuwia vigumu kulikubali....hasa ukizingatia tayari amezoea kuitwa baba fulani,...pia anaona heshima yake itakuwa imeshuka kiasi fulani kwani alishatangaza misimamo na familia yake mpya siku za nyuma...............pia kinachomsumbua ni kuanza maisha upya......na umri wake umeshasogea.....

Wazazi na viongozi wa dini aliwajibu dharau....sasa ataanzia wapi ili arudie aliyoyaita matapishi?
 
hakuna jinsi, aikabili aibu yake...(si aliitafuta mwenyewe?) na asonge mbele.......

Ndo maana kila siku nasema kwenye ndo wanaume huwa mnatafutaga viranga vingi sana....
 
Tena hawakomi,kila kukicha na vituko vipya!....hawa kaka zetu sijui mwalimu wao nani???
 
Mpe pole ndugu yetu,asiumie sana maana,ukubwa ndio huu!
::
Ashirikishe wazee ambao wana mtazamo wa kukubali mapito,wanayopitia vijana.Kama atapata ufumbuzi wa jinsi wa kutatua tatizo kuliko kulikuza zaidi.
::
Vipimo vya DNA ni jambo la muhimu ingawa pia,awe tayari kukubaliana na matokeo kwa moyo mkuu.
::
Fumbo la nani alistahili kuwa mke wake,ni mtihani ambao umetupata wengi.Hali ikiwa ngumu unaegemea kule unakopendwa zaidi.
::
Jenga tabia ya kumwomba Mungu kwa imani yako,usiitumainie hekima yako mwenyewe.
=
 
Mpe pole ndugu yetu,asiumie sana maana,ukubwa ndio huu!
::
Ashirikishe wazee ambao wana mtazamo wa kukubali mapito,wanayopitia vijana.Kama atapata ufumbuzi wa jinsi wa kutatua tatizo kuliko kulikuza zaidi.
::
Vipimo vya DNA ni jambo la muhimu ingawa pia,awe tayari kukubaliana na matokeo kwa moyo mkuu.
::
Fumbo la nani alistahili kuwa mke wake,ni mtihani ambao umetupata wengi.Hali ikiwa ngumu unaegemea kule unakopendwa zaidi.
::
Jenga tabia ya kumwomba Mungu kwa imani yako,usiitumainie hekima yako mwenyewe.
=


Tatizo la ndugu yetu huyu ni kuwa na misimamo hata kama amesimamia kuti kavu......na mama wa mtoto kamtaight kuwa akienda kupima DNA ina maana hamuamini..........asirudi kumuita mke.......arudi na talaka mkononi...

Mke wa kwanza alishamwacha kwa talaka ya mahakamani aliyoenda kuidai yeye bro mwenyewe.........(walikuwa na ndoa ya kanisani).......hapa mi sielewi......sasa watoana tena au....mi naona kama movie hivi.......kweli maisha ukiyachezea????
 
umevuna ulichopanda,ulipanda muhogo unategemea uvune mpunga?
 
Dalili zote zimeshaonyesha kuwa mtoto si wake......na kumbe sakata hilo lilikuwepo tangu mtoto alipozaliwa tu.....naye anakiri hilo japo inamuwia vigumu kulikubali....hasa ukizingatia tayari amezoea kuitwa baba fulani,...pia anaona heshima yake itakuwa imeshuka kiasi fulani kwani alishatangaza misimamo na familia yake mpya siku za nyuma...............pia kinachomsumbua ni kuanza maisha upya......na umri wake umeshasogea.....

Wazazi na viongozi wa dini aliwajibu dharau....sasa ataanzia wapi ili arudie aliyoyaita matapishi?

achana naye, mtu kama hataki kusaidiwa huwezi kumlazimisha umsaidie. Huyo tunamwita ****.
 
achana naye, mtu kama hataki kusaidiwa huwezi kumlazimisha umsaidie. Huyo tunamwita ****.

At the end of the day ni ndugu,japo ni wa mbali kidogo........tena wa kwanza kuzaliwa kwenye familia yao hivyo alipaswa awe na mwongozo mzuri kwa walioko chini yake na tunaomzunguka.........

Nataka nimkalishe chini nimshauri kwani huwa ananisiliza kidogo.......japo tulitubuana sababu ya kihoja hiki.....bado nawiwa kumsaidia..............ndio mana nahitaji mawazo yenu wadau
 
mijanamke ndivyo ilivyo kama mlikuwa hamjui...sio ya kuiaminia kabisaaa katika suala la mtoto full kukubambikizia....mkiambiwa jibatulieni msepe mwasema oh huo uhuni. ona sasa unalea toto la mwenzio. hahaha wanawake wa siku hizi sio wa kwako peke yako mpo wengi ati!!

sasa lakufanya ni kukubali umebugi men! piga chini huyo ni dada alafu tulizana mwenyewe. wala usiende kwa wife mliyetengana. hapa sasa ni maisha ya kibachelor tuuu!!!
 
Tatizo la ndugu yetu huyu ni kuwa na misimamo hata kama amesimamia kuti kavu......na mama wa mtoto kamtaight kuwa akienda kupima DNA ina maana hamuamini..........asirudi kumuita mke.......arudi na talaka mkononi...

Mke wa kwanza alishamwacha kwa talaka ya mahakamani aliyoenda kuidai yeye bro mwenyewe.........(walikuwa na ndoa ya kanisani).......hapa mi sielewi......sasa watoana tena au....mi naona kama movie hivi.......kweli maisha ukiyachezea????

Mwache ale jeuri yake
 
Usimumize mkeo moyo wake bila makosa,kuna watu wengine wako kwenye ndoa zaidi ya miaka 15 mke hajaharibu mimba wala haja shika mimba lakini ustahmilivu wanao seuze wewe mkeo amesha wahi kushika mimba ikaharibika, kua na subra na muachie mungu kilio chako atakupa mtoto kutoka kwa mkeo,huyo mwanamke leo unawasiwasi kua mtoto sio wako kesho atakuletea maradhi ndio utakufa kabla siku si zako...
 
Kama tayari uhakika upo si mwanae, basi ni heri arudiane na mkewe wa kwanza, ajishushe aombe msamaha.
Maana ndiye mwanamke anayempenda kwa dhati.
 
At the end of the day ni ndugu,japo ni wa mbali kidogo........tena wa kwanza kuzaliwa kwenye familia yao hivyo alipaswa awe na mwongozo mzuri kwa walioko chini yake na tunaomzunguka.........

Nataka nimkalishe chini nimshauri kwani huwa ananisiliza kidogo.......japo tulitubuana sababu ya kihoja hiki.....bado nawiwa kumsaidia..............ndio mana nahitaji mawazo yenu wadau

nadhani wewe ni Kipofu, unajaribu kumuongoza Kipofu mwenzako. Kila la kheli ndugu.
 
Back
Top Bottom