naona watu ambao si walimu wanazungumzia ualimu kwa vitu wasivyovifaham vya kiualimu. kama swala la elimu bure,mimi kama mwalimu ambae pia nina kacheo fulani ni kuwa nilipeka kwa mikono yangu taarifa ya bajeti ya matumizi ya shule kwa mwaka ujao,pia nilipeleka taarifa ya madeni yote ya shule yaliyokuwa yanadaiwa.natabiri walimu mliokuwa mnapenda kupiga pesa kupitia speed test za asubuhi,remedial,test za wik na mwezi na tuition za wizi imekula kwenu.nilishatukanwa sana kwa kupinga remidial na vitest vya ajabu ajabu kuwa ni miladi ya watu kujiingizia pesa ila mungu kanisikiliza.nasema wale mliokuwa mnawaibia watoto wa masikini na kugawana elfu 50 kila siku imekula kwenu.safi kabisa serikali