Usinyakue madaraka yasiyo yako

mwengeso

JF-Expert Member
Nov 27, 2014
9,219
6,650
Mwaka 2016 umekuwa mwaka wa malumbano ya kisiasa, maagizo kutoka kwa watu walio na wasio na madaraka na pia lawana nyingi tu juu utawala wa Serikali ya awamu ya tano.

Gazeti la Nipashe, Jumapili, Januari 1, 2017 limechapisha angalizo, ambalo naamini linatoa mwelekeo sahihi wa uongozi na waongozwa, kwa ujumla wao, ili kufikia malengo ya binafsi naya kitaifa kwa mwaka 2017.

Kwamba: "Unapochukua hatua fulani bila kuagizwa, kuelekezwa, au kuwa na madaraka halali ya kufanya hivyo, wewe unajichukulia madaraka mikononi.

Hasira, jaziba, ubabe na kufuata bendera, huwavuta watu kujipa kazi sio zao".

Hivyo basi ni BUSARA kuheshimu Dola na sheria zake.

HERI NA FANAKA MWAKA 2017
 
Back
Top Bottom