USIA wa Baba wa Taifa!


Hakika Nyerere alikuwa na maono. Serikali tatu ni kuua Muungano tu wala hakuna lingine. Serikali moja ndiyo haswaaaaa sawia lakini Zanzibar hawataki?

Huu Muungano unapasua kichwa sasa.

Huku site watu wameng'aka kweli wanataka tatu!!

 
Nasikia muda mfupi ujao leo utakuwa na mdahalo ITV pale Serena Hotel. Au ndio umeanza kupaniki na kuanza kutafuta majibu? Ha ha ha! Yetu macho nasubiria kuona ukavyojenga "hoja".

aaaah anagoja tumpe udambwiudambwi akajenga hoja na jinsi ya kujiandaa na maswal yasiyoepukika
 
Hii Sera mpya ndiyo ndiyo hasa itaokoa na kupendekeza muungano wetu. Na huu ndiyo muda wa kuchukua msimamo huu. Wengi wetu tutawaunga mkono. Kwani itasaidia sehemu moja ya muungano kuvunja Katiba kwa kupitia Katiba yake na kusaidia kuendelea kuwa nchi moja.
 
Nyerere akifufuka leo ameone warioba anavyotoa mishipa kuiua Tanzania atamlaani na warioba akimuona mwalim atakufa hapo hapo

Mkuu Wambeke, nakuhakikishia Nyerere angefufuka leo na kuiona Ikulu yake ilivyojeuka kijiwe cha dili, angeanguka hapo hapo na kufa upya! Tanzania mlishaiua wenyewe 2010 na wala msipoteze nguvu zenu bure kumtafuta Warioba uchawi!
 
mdahalo mtamu naamini usngetoka nduki ningefaid tactical zako kama moyes
 
Nape Nnauye

Naona umekimbia mjadala live ITV na kujificha huku JF.
Hii inaonesha ni jinsi CCM hamjakomaa na kuweza ku withstand mijadala migumu kabisa.
Hata ile sera yenu ya kura za wazi ni unafiq kabisa.
Hii Ni aibu kwako na kwa CCM kwa ujumla...
 
Last edited by a moderator:
Sera ya CCM inwahusu wanaCCM tu. Hii katiba ni ya wananchi wote, ukianza kuingiza habari ya sera yenu kwenye jambo la kitaifa ni upuuzi usio vumilika.
Hii mambo ya kuwa "chiriku" ati kwa sababu baba naye alikuwa "chiriku" ndio hapo kukosa akili.Endeleeni kuwapuuza wananchi, mkiwalazimishia mambo yenu-kuna siku watayakataa na kuwakataa pia.
 

We kweli elimu yako ya kuunga unga "Usia" ndio mdudu gani huyo?
 
Hatma ya tz iko mikononi mwa mtz mwenyewe na sio ccm, ungekuwa na akili ungetambua hili ama ww ndo unawakilisha wenye akili wenzako?
 

Yote mnayofanya refernce kwenye maneno ya Mwalimu mnatafuta yasiyo wagusa wenyenchi yenu,nasema wenyenchi yenu maana wale wenye mawazo tofauti na nyinyi hawastahili kwa raia wa Tanzania,hawa wanamajina yote mabaya, ndiyo wananchi.

Hebu fikiria leo Nyerere akafufuka na kutinga ofisini mwako,unauwezo wa kumweleza kwanini mlivunja katiba ya 2010?

Je hamuoni nyie ndiyo wenye makosa makubwa zaidi ya kuhatarisha uhuru na amani ya nchi,kwanza ndiyo wa kwanza kuvunja katiba,rushwa mahali pake bila kusahahu ufisadi,sasa Nyerere huyu mnemuenzi au mnamdhalilisha
 

Umejiandikia kutoka kichwani mwako ama umenukuu?
 

Chama Cha Mapinduzi chenye wanachama wenye akili, na ukweli, na ujasiri????

Ujasiri is not a problem kabisa. hata shetani anao ndiyo maana haoni aibu kuongoza maovu.
 
Kwa maana tu. Mwalimu bila ketafuna maneno alisema: WATANZANIA WANAHITAJI MABADILIKO. NA WASIPOYAPATA CCM,WATAYATAFUTA NJE YA CCM.

Kaa mkao wa UKAWA ndio habari ya mini. :loco:
 

Acha unafiki wewe, muda utasema.
 
Nasikia muda mfupi ujao leo utakuwa na mdahalo ITV pale Serena Hotel. Au ndio umeanza kupaniki na kuanza kutafuta majibu? Ha ha ha! Yetu macho nasubiria kuona ukavyojenga "hoja".

Ana hoja basi.
 
Hivi Wosia wa baba wa Taifa ni Kugawa Rushwa nje nje? Grrrrrrrrrrrrrrrrrrrr
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…