Akizungumzia kwa kina tukio hilo la kufanyiwa vitendo vya ushirikina vilivyopelekea yeye na wenzake kukimbia na kuacha kazi, Ngaya alidai wakiwa katika mazingira ya shule hupokea vitisho kutoka kwa baadhi ya wakazi wa kata hiyo hasa inapotokea kutoa adhabu kwa wanafunzi.
Alisema miongoni mwa matatizo wanayoyapata baada ya kupokea vitisho kutoka kwa baadhi ya wazazi wa watoto shuleni ni kuanguka na kupoteza fahamu, kujisikia maluweluwe na wakati mwingine kujikuta macho yakipata giza wakiwa wanafundisha darasani.