Ushindi wa CCM na viini macho vya Mwanamalundi

Ushindi wa CCM na viini macho vya Mwanamalundi

Civilian Coin

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2012
Posts
2,305
Reaction score
4,390
USHINDI WA CCM NA VIINI MACHO VYA MWANAMALUNDI.

Inasadikika CCM wameshinda kata takribani zote huku upinzani wakipata kata moja tu, mjinga ni mjinga tu na mpumbavu ana nafasi yake, wagombea wamejitoa kwa uonevu wenu wa kuminya Haki na Demokrasia halafu mnasema mmeshinda au mmeteuliwa na Tume ya Uchaguzi? Matokeo mengi mmeyapindua kwa nguvu ya Jeshi la Polisi na kuwatishia watu kuwaua halafu mnasema mmeshinda…

CCM sio Chama hata kidogo bali wanafanya Mazingaombwe ya danganya toto kuonesha kuna demokrasi giza ndani ya mwanga. Mpango wa CCM nikurudi kwenye mfumo wa chama kimoja kwa kuvihujumu vyama vya upinzani kwa kwakutumia nguvu za Kijeshi ambayo ni mbinu niliyowafundisha mimi mwenyewe kipindi nimejiunga CCM mwaka 2014 kabla sijaondoka mwaka huu 2017.

Aidha mipango michafu ya CCM ni kufanya unyama kila kona na kuwadhalilisha Wapinzani kwa namna yoyote ile na wengine napoongea hapa watakimbia Nchi na kwenda kuishi uhamishoni. Mwanamalundi alipokuwa akishindana ngoma maadui zake walikuwa wanageuza ushindi nakumpa adui yake ili Mwanamalundi aanguke na hiki ndicho anachofanya CCM. Wapinzani wanapaswa kuwa wabunifu tu ili kwenda kinyume na malengo ya CCM na ni rahisi sana kuwapindu CCM na Mzingaombwe yao. KAZI KWENU.

Mwaka 2020 or before…..Iam going to be a President of United Republic of Tanzania

DEOGRATIUS NALIMI KISANDU

28 NOVEMBA 2017
 
ulisimamisha mgombea wa chama chako kwenye hizo kata?
 
Hakuna Uchaguzi wala Jimbo ambalo Chadema waliwahi kukiri kushindwa kihalali!
 
Mbinu umesema uliwafundisha wewe ukiwa kule, leo wamefuzu na kuyatumia mafunzo yako halafu unakuja kulialia tena hapa? Mwehu kweli kweli.
 
Huu uchaguzi umeonyesha jinsi CCM ilivyo dhaifu na jinsi ambavyo watu hawaipendi CCM. Nina uhakika kama si nguvu za kijeshi zilizotumika, CCM haingeambulia hata kata moja. Uzuri ni kwamba hata CCM wenyewe wanajua kwamba mambo yalikuwa magumu kwao. Hat mwenyekiti mwenyewe anajiuliza ni kwa nini pamoja na yote aliyoyafanya bado chama chake kinategemea nguvu za kijeshi kushinda uchaguzi tena wa diwani. Mimi nilifikiri ili CCM ijitathmini namna gani inapendwa na wananchi wangeacha huu uchaguzi uwe wa huru na haki ili waone maeneo yenye matatizo au maeneo wasioyokubalika na kuwekeza nguvu huko. Unamwona hata Polepole anazungumza huku midomo inatetemeka, kamishna wa tume ya uchaguzi naye anazungumza huku midomo ikitetemeka pia.
 
Kuna ulazima wa ccm kukaa na kujitafakari juu ya kutokukubalika kwa wananchi hadi kwa nsaada wa vyombo vya ulinzi na usalama. Ni ushindi usio na ladha zaidi ya kukebehiwa na wananchi. Hakuna anayeuzungumzia ushindi huo wa kulazimisha kwa upendo na furaha bali kwa kuguna tu jambo linaloashiria kuwa huko mbele si kwema na watu wataniandaa kujihami badala ya kushindana. Amani ni bora kuliko madiwani wenu
 
USHINDI WA CCM NA VIINI MACHO VYA MWANAMALUNDI.

Inasadikika CCM wameshinda kata takribani zote huku upinzani wakipata kata moja tu, mjinga ni mjinga tu na mpumbavu ana nafasi yake, wagombea wamejitoa kwa uonevu wenu wa kuminya Haki na Demokrasia halafu mnasema mmeshinda au mmeteuliwa na Tume ya Uchaguzi? Matokeo mengi mmeyapindua kwa nguvu ya Jeshi la Polisi na kuwatishia watu kuwaua halafu mnasema mmeshinda…

CCM sio Chama hata kidogo bali wanafanya Mazingaombwe ya danganya toto kuonesha kuna demokrasi giza ndani ya mwanga. Mpango wa CCM nikurudi kwenye mfumo wa chama kimoja kwa kuvihujumu vyama vya upinzani kwa kwakutumia nguvu za Kijeshi ambayo ni mbinu niliyowafundisha mimi mwenyewe kipindi nimejiunga CCM mwaka 2014 kabla sijaondoka mwaka huu 2017.

Aidha mipango michafu ya CCM ni kufanya unyama kila kona na kuwadhalilisha Wapinzani kwa namna yoyote ile na wengine napoongea hapa watakimbia Nchi na kwenda kuishi uhamishoni. Mwanamalundi alipokuwa akishindana ngoma maadui zake walikuwa wanageuza ushindi nakumpa adui yake ili Mwanamalundi aanguke na hiki ndicho anachofanya CCM. Wapinzani wanapaswa kuwa wabunifu tu ili kwenda kinyume na malengo ya CCM na ni rahisi sana kuwapindu CCM na Mzingaombwe yao. KAZI KWENU.

Mwaka 2020 or before…..Iam going to be a President of United Republic of Tanzania

DEOGRATIUS NALIMI KISANDU

28 NOVEMBA 2017
bangi ni mmea hatalishi kwa afya ya akina Kisandu
 
Wape na hayo mafunzo huko chadema ili wasijitoe saa saba mchana siku ya kupiga kura!
 
Wamejitoa au walitolewa unataka kusema hawakumtii Mbowe.
 
Kuna ulazima wa ccm kukaa na kujitafakari juu ya kutokukubalika kwa wananchi hadi kwa nsaada wa vyombo vya ulinzi na usalama. Ni ushindi usio na ladha zaidi ya kukebehiwa na wananchi. Hakuna anayeuzungumzia ushindi huo wa kulazimisha kwa upendo na furaha bali kwa kuguna tu jambo linaloashiria kuwa huko mbele si kwema na watu wataniandaa kujihami badala ya kushindana. Amani ni bora kuliko madiwani wenu
ushindi usio na radha ccm hatuhitaji radha ya vanila wala embe ni mbele kwa mbele
 
Back
Top Bottom