Ushawahi usikia ugonjwa, Bipolar

Ushawahi usikia ugonjwa, Bipolar

nzalendo

JF-Expert Member
Joined
May 26, 2009
Posts
12,733
Reaction score
14,157
Naam maradhi yasiyo ya kuambukizwa yanazidi kuujaza ulimwengu. Kwa kifupi ugonjwa huu ni ile khali ya kubadili hisia kwa ghafla bila kuwa na sababu yeyote ya msingi,

Kwa mfano mtu anaweza kupandwa na hasira ghafla ilhali hajakosewa na mtu yeyote, Hali kadhalika mtu huyo huyo anaweza kuwa na furaha ya ajabu kwa ghafula bila kuwa na jambo la aina yeyote,

Watu wa namna hii nimeshawahi kukutana nao hasa maboss..na kwa kweli sikujua kama ni wagonjwa,,,yaani wafanyakazi asubuhi tunaulizana leo boss vp?...kama anafuraha basi hapo ndio waweza kupenyeza jambo lako vinginevyo ni mtihani.

Awali nilikuwa nachukulia ni mzaha na kuwaita vichaa baridi lakini baada ya kupata somo ndio nikaelewa ya kwamba ni ugonjwa,,,sijui nini nini mood swing na nini sijui mamaae.
 
Bipolar zipo aina nyingi.

Sisi kiujumla tunaita matatzo ya afya ya akili. Mwezi huu yupo sawa mwezi unaofuata mnapeleka muhimbili. Changamoto sana....
Mtihani sana...kumbe kuna waheshimiwa kibao wana hili tatizo, mpaka dawa wanatumia,,,umdhaniae ndiye, kumbe ndiye siye, aliye, ndiye, siye.
 
Soma na kitu kinaitwa personality disorders
Naam maradhi yasiyo ya kuambukizwa yanazidi kuujaza ulimwengu. Kwa kifupi ugonjwa huu ni ile khali ya kubadili hisia kwa ghafla bila kuwa na sababu yeyote ya msingi,

Kwa mfano mtu anaweza kupandwa na hasira ghafla ilhali hajakosewa na mtu yeyote, Hali kadhalika mtu huyo huyo anaweza kuwa na furaha ya ajabu kwa ghafula bila kuwa na jambo la aina yeyote,

Watu wa namna hii nimeshawahi kukutana nao hasa maboss..na kwa kweli sikujua kama ni wagonjwa,,,yaani wafanyakazi asubuhi tunaulizana leo boss vp?...kama anafuraha basi hapo ndio waweza kupenyeza jambo lako vinginevyo ni mtihani.

Awali nilikuwa nachukulia ni mzaha na kuwaita vichaa baridi lakini baada ya kupata somo ndio nikaelewa ya kwamba ni ugonjwa,,,sijui nini nini mood swing na nini sijui mamaae.
 
Ni zip hiz aina zs bipolar?
1. Bipolar I
Hii ndiyo aina kali zaidi. Mtu hupata:
Mania kamili — hali ya furaha/msisimko mkubwa sana, inayodumu angalau siku 7, inayohitaji kulazwa hospitalini mara nyingi
Inaweza kuambatana na psychosis (kupoteza uhalisia)
Depression inaweza kutokea lakini si lazima
2. Bipolar II
Hypomania (mania ndogo — si kali kama Bipolar I) na depression kali
Mtu bado anafanya kazi lakini ana hali zinazobadilika sana
Mara nyingi depression ndiyo tatizo kubwa zaidi kuliko hypomania
3. Cyclothymia (Cyclothymic Disorder)
Aina nyepesi zaidi
Mabadiliko ya hali ya chini (hypomania ndogo) na huzuni ndogo — hayafikii viwango kamili vya mania au depression
Hudumu miaka 2 au zaidi
Inaweza kuwa ngumu kutambua kwa sababu dalili ni ndogo
4. Bipolar "Other Specified" / "Unspecified"
Dalili za bipolar zinazoonekana lakini hazilingani kabisa na aina 1, 2, au cyclothymia
Inaweza kusababishwa na dawa, pombe, au ugonjwa mwingine wa kimwili.

Muhimu kutambua bipolar hauponi ila ina dawa za kukutuliza na pia tiba ya ushauri nasaha.
 
1. Bipolar I
Hii ndiyo aina kali zaidi. Mtu hupata:
Mania kamili — hali ya furaha/msisimko mkubwa sana, inayodumu angalau siku 7, inayohitaji kulazwa hospitalini mara nyingi
Inaweza kuambatana na psychosis (kupoteza uhalisia)
Depression inaweza kutokea lakini si lazima
2. Bipolar II
Hypomania (mania ndogo — si kali kama Bipolar I) na depression kali
Mtu bado anafanya kazi lakini ana hali zinazobadilika sana
Mara nyingi depression ndiyo tatizo kubwa zaidi kuliko hypomania
3. Cyclothymia (Cyclothymic Disorder)
Aina nyepesi zaidi
Mabadiliko ya hali ya chini (hypomania ndogo) na huzuni ndogo — hayafikii viwango kamili vya mania au depression
Hudumu miaka 2 au zaidi
Inaweza kuwa ngumu kutambua kwa sababu dalili ni ndogo
4. Bipolar "Other Specified" / "Unspecified"
Dalili za bipolar zinazoonekana lakini hazilingani kabisa na aina 1, 2, au cyclothymia
Inaweza kusababishwa na dawa, pombe, au ugonjwa mwingine wa kimwili.

Muhimu kutambua bipolar hauponi ila ina dawa za kukutuliza na pia tiba ya ushauri nasaha.
Shukran sana mkuu...
Haya mambo sikuyajua kabla,,,
Ninasakitika kwamba ni maradhi yasiyopona,,
Je? ni namna gani twaweza kuyakwepa? au angalau kujikinga?
 
NA PENGINE WAATHIRIKA WAKUBWA WAPO NDANI YA MAKANISA YALEEEE YA MBOGAMBOGA.
Ai DAUTI
 
Back
Top Bottom