ameline
JF-Expert Member
- Jan 8, 2013
- 2,292
- 1,152
Jamani nadhani kila mmoja anaona jinsi hali ya ajira ilivyo ngumu hapa nchini Tz,vijana wengi wamemaliza chuo lakini hawana wanalolifanya zaidi ni kuzurura ovyo mitaani na kulala mpaka saa saba wengine wanaishia kuangalia series za movies nk. si kwamba wanapenda, bali imewalazimu.Lingine ni kwamba si kila unaemuona bank kasomea finance and account wengine ni sociologist,BA education etc.au kila unaemuona akifundisha kasomea ualimu, hapana, imewalazimu kufanyia kazi mambo ambayo hawakuyasomea kutokana na kukosa hiyo nafasi ya field yake,na kukuta opportunity ambayo either inahitaji training au sivyo anafanya anaajiriwa!
Sasa kuna brother mmoja amegraduate last year BAGE mambo ya Geography and evironmental studies, akaja kupendeza ofisini pale victory collection, kwa kua alikua mjanja tukapiga story mbili tatu nikampa business card nikamwambia kama nikiona post sehemu yeyote basi nitamchek akasema poa.
sasa kuna rafiki yangu ambaye alinipigia simu juzi tuesd, akaniambia kuna nafasi ya kusimamia hotel ya baba yake ambayo anaifungua tar 21 this month, mshahara akasema ni laki 2 lakini jinsi biashara itakavyokua mhusika ataongezewa, akaniambia purposely kwa ajili yangu kwani kuna watu kibao tena watu wazima wanaililia hiyo nafasi ya umeneja wa hoteli lakini wanaambulia kuwa tayari amepatikana, na hyo dada alinilenga mmi ndo nichukue nafasi hiyo. niliitamani sana nafasi hiyo ila kutokana na kutingwa sana na mambo yangu na kuna kaproject nakafanyia evaluation ambapo kamkataba kanaisha march this year, nikasema ngoja basi nimchek yule brother chap, kumpigia majibu aliyonipa ndiyo yaliyonifanya niachie post hii yaani,.
ILIKUA HIVI:
Baada ya kumpigia ile jumanne akaniambia mh nashukuru sister ila siwezi kufanya hiyo kazi kwani haiendani hata kwa asilimia moja na field yangu, halafu mshahara ni mdogo sana, nikamwambia unaishi wapi? akaniambia usa river hapa arusha, basi nikamchek yule sister kama kuna commission ya malazi na msosi akaniambia hamna shida kwa heshima yangu, coz nlimwambia kuna mdogo wangu ambaye ni huyu kaka sasa, atapewa room hapo hotel kwa miez 6 bure then akiwa anatafuta, msosi mara tatu kwa siku unapata, hotel yenyewe ipo ngaramtoni hapa arusha. nikamchek tena nikamwambia hizo commission akaniambia mshahara sasa sister ndo ishu, siwezi kuyafikia malengo yangu kwa mshahara huo, na degree yangu laki mbili???? hapana, ndivyo msg yake ilivyosema,,.basi nikamwambia poa all the best in searching for good job with wonderful salary..nikamwona huyu ameishia kuiona hiyo laki mbili tu hakujua kama comisison aliyopewa imemsave nauli, msosi na gharama zinginezo zisizo na ulazima, yaan kwa kifupi kwa mwezi hiyo laki mbili inaweza kutulia kwenye a/c tuli bila kuguswa.
USHAURI WANGU KWA VIJANA TUNAOTAFUTA AJIRA
mnapopata bahati kama hizi jamani msiziache ziende, hebu ona mfano hyu brothermen ameachia laki mbili wakat hana la kufanya home, haingizi hata mia,bora hata muuza karanga,. unadhani kufanikiwa kunaanzia juu jamani?? tuulizeni sisi tulianzia wapi mapaka tukawa kama tulivyo. unapopata kazi yeyote ambayo itakufanya uwe busy na una uhakika wa kupata hata elfu 2 kila siku, kwa ushaur wangu fanya usiache, weka degree yako chini piga kazi, hata kama ni kuuza duka, we fanya kwani siri ya malengo yako si iko moyoni mwako jamani??? ukiona mchongo mwingine unaondoka unaufata, yaan hakuna mazingira magumu kama ya kutafuta kazi wakati huna chochote unachofanya, yaan haupo kazini wala hujishughulish na chochote then unatafuta kazi, yaaan utachoka sana, unaweza ukawa dukani ukajuana na wateja leo na kesho haohao ndo wakakutoa,.,.hebu naomba tukue kiakili jamani umri unakwenda, majukumu yanakuja, miaka inakimbia bado unasubiri tu mshahara wa laki 5? pigana kijana ujikomboe wewe na jamaa zako.
SAMAHANINI SANA JAMANI MIMI HUWA SIISHIWI MANENO KWANI MNAJUA MIMI NI SOCIOLOGIST, NAJUA NIMEWACHOSHA ILA NASHUKURU KWA KUUPATA UJUMBE HUU NADHANI UTAKUA FUNDISHO NA MUUFANYIE KAZI.
Napatikana amelinechao@gmail.com
Sasa kuna brother mmoja amegraduate last year BAGE mambo ya Geography and evironmental studies, akaja kupendeza ofisini pale victory collection, kwa kua alikua mjanja tukapiga story mbili tatu nikampa business card nikamwambia kama nikiona post sehemu yeyote basi nitamchek akasema poa.
sasa kuna rafiki yangu ambaye alinipigia simu juzi tuesd, akaniambia kuna nafasi ya kusimamia hotel ya baba yake ambayo anaifungua tar 21 this month, mshahara akasema ni laki 2 lakini jinsi biashara itakavyokua mhusika ataongezewa, akaniambia purposely kwa ajili yangu kwani kuna watu kibao tena watu wazima wanaililia hiyo nafasi ya umeneja wa hoteli lakini wanaambulia kuwa tayari amepatikana, na hyo dada alinilenga mmi ndo nichukue nafasi hiyo. niliitamani sana nafasi hiyo ila kutokana na kutingwa sana na mambo yangu na kuna kaproject nakafanyia evaluation ambapo kamkataba kanaisha march this year, nikasema ngoja basi nimchek yule brother chap, kumpigia majibu aliyonipa ndiyo yaliyonifanya niachie post hii yaani,.
ILIKUA HIVI:
Baada ya kumpigia ile jumanne akaniambia mh nashukuru sister ila siwezi kufanya hiyo kazi kwani haiendani hata kwa asilimia moja na field yangu, halafu mshahara ni mdogo sana, nikamwambia unaishi wapi? akaniambia usa river hapa arusha, basi nikamchek yule sister kama kuna commission ya malazi na msosi akaniambia hamna shida kwa heshima yangu, coz nlimwambia kuna mdogo wangu ambaye ni huyu kaka sasa, atapewa room hapo hotel kwa miez 6 bure then akiwa anatafuta, msosi mara tatu kwa siku unapata, hotel yenyewe ipo ngaramtoni hapa arusha. nikamchek tena nikamwambia hizo commission akaniambia mshahara sasa sister ndo ishu, siwezi kuyafikia malengo yangu kwa mshahara huo, na degree yangu laki mbili???? hapana, ndivyo msg yake ilivyosema,,.basi nikamwambia poa all the best in searching for good job with wonderful salary..nikamwona huyu ameishia kuiona hiyo laki mbili tu hakujua kama comisison aliyopewa imemsave nauli, msosi na gharama zinginezo zisizo na ulazima, yaan kwa kifupi kwa mwezi hiyo laki mbili inaweza kutulia kwenye a/c tuli bila kuguswa.
USHAURI WANGU KWA VIJANA TUNAOTAFUTA AJIRA
mnapopata bahati kama hizi jamani msiziache ziende, hebu ona mfano hyu brothermen ameachia laki mbili wakat hana la kufanya home, haingizi hata mia,bora hata muuza karanga,. unadhani kufanikiwa kunaanzia juu jamani?? tuulizeni sisi tulianzia wapi mapaka tukawa kama tulivyo. unapopata kazi yeyote ambayo itakufanya uwe busy na una uhakika wa kupata hata elfu 2 kila siku, kwa ushaur wangu fanya usiache, weka degree yako chini piga kazi, hata kama ni kuuza duka, we fanya kwani siri ya malengo yako si iko moyoni mwako jamani??? ukiona mchongo mwingine unaondoka unaufata, yaan hakuna mazingira magumu kama ya kutafuta kazi wakati huna chochote unachofanya, yaan haupo kazini wala hujishughulish na chochote then unatafuta kazi, yaaan utachoka sana, unaweza ukawa dukani ukajuana na wateja leo na kesho haohao ndo wakakutoa,.,.hebu naomba tukue kiakili jamani umri unakwenda, majukumu yanakuja, miaka inakimbia bado unasubiri tu mshahara wa laki 5? pigana kijana ujikomboe wewe na jamaa zako.
SAMAHANINI SANA JAMANI MIMI HUWA SIISHIWI MANENO KWANI MNAJUA MIMI NI SOCIOLOGIST, NAJUA NIMEWACHOSHA ILA NASHUKURU KWA KUUPATA UJUMBE HUU NADHANI UTAKUA FUNDISHO NA MUUFANYIE KAZI.
Napatikana amelinechao@gmail.com