Shida na raha
JF-Expert Member
- Aug 8, 2014
- 3,774
- 3,460
Habari za majukumu wakubwa.. Kama kichwa cha habari kinavosema hapo juu.
Leo baada ya kutoka kitandani mke wangu ameniomba kitu ambacho kimenishangaza na sikuamini kwamba angefikia hatua ya kunishawishi nioe mke ambae amempenda yeye.
STORI INAANZA:
Kuna jirani yangu ana mdogo wake wa kike ambae ana takribani miaka 18 au 19 amekuja harusini hapa. Sasa katika kupiga stori likaingia suala la ndoa na mke wangu akampenda yule mdada ili aolewe na mimi na yuko radhi wakae nyumba moja.
Sasa nimejaribu kumuliza mke wangu kwanini umenichagulia mke huyo?
"Nimekuchagulia mke huyo kwasababu tunaendana tabia na pia yeye amependa kuolewa uke wenza na wewe vile vile familia yao nimeikubali kwakuwa haina ushirikina. Pili bado ni mtoto mdogo hasomi tena nahitaji umsitiri".
Ni kweli mimi kila siku wimbo wangu nikutaka kuoa mke wa pili lakini mke wangu anachoogopa ni kuja kuleta mshirikina akamfanyia masuala ya ajabu ili apendwe yeye na istoshe mke wangu ana wivu sana sasa nimeona ni fursa kwakuwa kamchagua mwenyewe acha niitumikie.
Sasa nimeona bora nije nalo hapa tushee kwa pamoja.
NB: Mke wangu yupo serious na hili na leo anamwita nije niongee nae.
Leo baada ya kutoka kitandani mke wangu ameniomba kitu ambacho kimenishangaza na sikuamini kwamba angefikia hatua ya kunishawishi nioe mke ambae amempenda yeye.
STORI INAANZA:
Kuna jirani yangu ana mdogo wake wa kike ambae ana takribani miaka 18 au 19 amekuja harusini hapa. Sasa katika kupiga stori likaingia suala la ndoa na mke wangu akampenda yule mdada ili aolewe na mimi na yuko radhi wakae nyumba moja.
Sasa nimejaribu kumuliza mke wangu kwanini umenichagulia mke huyo?
"Nimekuchagulia mke huyo kwasababu tunaendana tabia na pia yeye amependa kuolewa uke wenza na wewe vile vile familia yao nimeikubali kwakuwa haina ushirikina. Pili bado ni mtoto mdogo hasomi tena nahitaji umsitiri".
Ni kweli mimi kila siku wimbo wangu nikutaka kuoa mke wa pili lakini mke wangu anachoogopa ni kuja kuleta mshirikina akamfanyia masuala ya ajabu ili apendwe yeye na istoshe mke wangu ana wivu sana sasa nimeona ni fursa kwakuwa kamchagua mwenyewe acha niitumikie.
Sasa nimeona bora nije nalo hapa tushee kwa pamoja.
NB: Mke wangu yupo serious na hili na leo anamwita nije niongee nae.