Ushauri wako unahitajika

Ushauri wako unahitajika

Magoa

Member
Joined
Mar 20, 2013
Posts
28
Reaction score
5
Habari za muda huu mimi ni kijana nilikuwa na uhusiano na msichana mmoja na tuliweza kupata mtoto mmoja wa kiume hakika ya mapenzi yetu yalikuwa mazuri lakini na mapungufu ya kibinadamu yalikuwepo tatizo la huyo msichana lilopelekea tutengane ni roho ya uchoyo alikuwa hapendi ndugu zangu ilifikia hatua ninapomwachia pesa ya kula ye alikuwa hashughuliki na chakula badala yake anaenda kununua nguo nilimuelimisha lakini akifuata kama siku 7 au 10 anarudia ile tabia yake nilipomwambia kuwa mwenendo huu siutaki na sasa urudi kwenu ukaanze maisha yake hakukubali aliniomba msamaha na kuniahidi kuwa hatorudia mimi nikamkazia kuwa arudi tu maamuzi aliyoyafikia yeye alikunywa mafuta ya taa lakini hakufa baada ya tukio hilo kukawa na kikao alipoulizwa kwanini ulikunywa mafuta ya taa ? Alijibu kuwa mume wangu hanitaki tena nilipoulizwa mimi nikasema ni kweli simtaki kwa sababu ya tabia ya uchoyo aliyonayo wazee wakasema sio vizuri kwani tayari mna mtoto atakuja pata tabu ya malezi wazee walisisitiza juu ya hilo mimi nikayafunika na kuangalia matokeo ya baadae lakini mwendo ni ule ule nilipomrudisha kwao nako huko kanywa sumu pia hakufa kisa hawezi ishi bila mimi na mimi sijapenda mwenendo wake nifanyaje hapo wadau funguka kiukweli utani tupa kule na kama huna cha kusema we iache hii post
 
Ajaolewa na ndugu uliyemuowa ni wewe, so kutokuwapenda si hoja,, uwezi kujua sababu ya yeye kutokuwapenda

Busara ungemuuliza kwa nini apendi ndugu zako, uanzie hapo katika kutatua hilo tatizo
 
Unaishi nao ndugu zako?,..kama ndivyo nunua mahitaji ya chakula kama mchele, unga mafuta mboga wewe mwenyewe wapike,hela mkeo mpe ya matumizi yake akanunue nguo zake kwa kujinafasi by the way yuko kwake hao ndugu ni wapitaji huwezi kuwaoa labda kama humpendi tu huyo mwanamke,... Siwezi vunja ndoa kisa ndugu aisee
 
Tangu 2013 mnakuja kumpa ushauri leo
 
Back
Top Bottom