Najua nia yake ya kufanya hivyo inaweza kuwa kwa maana ya kufanya kinachoitwa kujenga chama chake, lakini akumbuke hao hao anaodhani anawajenga kuna siku watamuita mkosa adabu siku atakapowapinga, let it be kutafuta uongozi ndani ya chama au vyovyote. kumbuka wanaokushangilia na kukuita mfalme leo, kesho watakupiga mawe. jitahidi kuwa na mahusiano ambayo ni cross cutting kwa maana ya kuheshimu watu kwa utu na ubinadamu wao. Nani ajuaye? mtumwa wa leo anaweza kuwa mtawala kesho. kama ulimheshimu, kumbuka natumia kumheshimu na siyo kutomkosoa, atakuheshimu pia.