Ushauri wa bure kwa CHADEMA

mtoto wa mchungaji

JF-Expert Member
Joined
Oct 24, 2020
Posts
279
Reaction score
480
Katika soko la ushindani huwa mzalishaji anaangalia nini mlaji anataka na huyo mzalishaji uzingatia hicho na kukileta sokoni na hapo huwa anapata kitu kinaitwa supa au abnomal profiti, yaani faida ya juu.

Haya ni tofauti na chama cha Chadema kumlisha mlaji, wenyewe hawapendi, wanapenda kumlisha mlaji kitu wanachokita wao, na siyo mlaji anachotaka, kwamfano swala la korona. Kiukweli hata kama mtakataa watanzania hawapendi lokudauni, awapendi kuvaa barakoa, awapendi hata hizo chanjo na hata kupewa hofu na taarifa za korona hawapendi. Hili lijueni jamani. Lakini Chadema wanalivalia njuga, ndiyo mada, kaulimbiu, hoja, sera mpya.

Hapa tuwe wakweli, hivi ni kweli Chadema wanapenda afya za watanzania kiasi hiki? angalia Lisu tulivyompokea pale uwanja wa ndege alishuka amevaa barakoa kuubwa lakini katikati ya maandamano tena alipofika mitaa ya Buguluni tu alipouona ule umati mkubwa na hata mtu mmoja ajavaa barakoa na yeye akaitupia chini hili afanane na watanzania wenzake. Na ikumbukwe Lisu hakuvaa tena barakoa kipindichote cha kampeni mapaka tulipomwona anasafiri kurudi Uberigiji ndiyo alionekana kuivaa tena.

Kwanini mnang'ang'ania hili jambo mpaka chama kinakufa kwani kila misheni huwa ina plani B. Inamaana hakuna wasomi Chadema wa kutoa ushauri kama huu hadi mimi mtoto wa mchungani niseme. Amsheni dude wanaume kwani dume limeondoka sasa mama, mnataka kusema hamnahoja kabisa ila Korona? acheni masiara goli limetanuka lakini hamtaki kupanda mbele.

Juzi kati nilikuwa namsikiliza mwenyekiti wa Chadema taifa na katika hotuba yake aliongea mambo mengi ya msingi lakini mwishoni akaanza kuboa watu, mara mimi nimesha chanjwa na itapendeza watanzania wote tuchanjwe, hivi hii ni hoja kweli yaani kuchanjwa kwa mwenyekiti ndiyo iwe watanzanioa wote milioni 60. Acheni haya mambo, kuweni siriasi kidogo.

Kunaubaya gani familia ya Chadema ikiamua kujichanja wao kama chama, mi naona watanzania watawapenda zaidi, mbona kunawatanzania wengi tu tunawajua wamechanjwa wengine walikufa na wengine wapo hai wanadunda, kwanini msijifunze kwa mama Samia yeye alisema anaunda tume ya Korona, lakini alipochungulia walaji tu akagundua kuwa hawapendi hiyo bidhaa si mmemwona kapotezea na kazi inaendelea.

Jamani mlaji mlaji ndiyo mteja ndiyo mfalme ananafasi yake, utashangaa Chadema jinsi walivyolivalia njuga suala la vutambulisho vya mjasiliamali mdogo, ohoo vinamapungufu, havifai. Hilo ni kweli hata mtoto wa darasa la saba anaweza kuyaona hayo mapungufu ila CCM walimwangalia mlaji kuelekea uchaguzi mkuu ninyi kwanini hamstukii hizi ishu badala yake mnachonganishwa na wapiga kura kijinga.

Inamaana mpaka leo hamjui fitina za CCM ambaye ni mshidani wenu basi mtakaa sana, kama ningekuwa ni mimi nagombea urais kupitia CDM, pale ningesema elfu 20 ni nyingi mimi mkinichagua ntaweka elfu 10 tu ungeona walaji tabia zao zilivyo.

Lamwisho kwa kumalizia, hata Mwalimu Nyerere aliwai sema yeye hakuwa malaika alikuwa anakosea, Chadema hasa wanachama na wafuasi anzeni kuamini hata kidogo tu kuwa Mwenyekiti wa maisha wa Chadema anakoseaga.
 
Sasa mtoto wa mchungaji kwanini usiendelee kuchunga kondoo au nayo imekuwa kazi ngumu.
 
Hiyo issue ya vitambulisho vilikuwa vya low quality havina necessary information itayomwezesha mtumiaji kufaidika nacho, Lissu akiwa mgombea wa Chadema akasema akipata nafasi ya kuongoza atavifanya hivyo vitambulisho viwe na thamani kwa machinga ikiwezekana apate mkopo bank, na hili hata CCM walikuja copy.

Hupendi Chadema wazungumzie issue ya Corona ili iweje? tujidanganye tunaishi kisiwani au? Rais mwenyewe kasema anaunda Tume, Corona ni issue sensitive sana ulimwenguni kwa sasa.

Kutokuizungumzia ni uzwazwa, suala la Lissu kuvaa barakoa na kuivua ni uamuzi wake, Corona inakuja kwa phase then inatulia, sasa kama wakati ule wa Lissu ilikuwa imetulia unataka wasivae tena barakoa hata ilivyorudi phase two kirusi toka S.A?

Mtoto wa mchungaji unaangamia kwa kukosa maarifa, isome biblia vizuri kabla hujaanza kuwalaumu waliokuzidi uwezo wa kufikiria.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…