ushauri wa bure kwa CDM

ushauri wa bure kwa CDM

Abdull Kazi

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2012
Posts
345
Reaction score
306
Wakati huu ambao chama chenu kina hali ya sintofahamu kutokana na mgogoro unaoendelea ingekuwa ni wakati muafaka kwa wanachama wapenzi na washabiki kwa ujumla,wakajielekeza kutafuta namna bora ya kufikia mwisho badala ya kutumia mitandao ya kijamii na vyombo vingie vya habari kuwajaza mihemko viongozi wenu.

Karibu asilima 90 ya wanaochangia ktk mitandao wanaishia kutoa kashfa kwa upande ambao hawaafikiani nao...hali inayotoa mwanya kwa maadui wa chama chenu kupenyeza sumu watakavyo na kwa kuwa mmeshamini kila mmoja kuwa adui yake ni yule asiuekubaliana nae wenzenu wanazidi kushambulia kadiri wawezavyo mtakapotahamaki mtakuwa mmechelewa fanyeni jambo moja sasa timuaneni au mkubaliane kusameheana mpate muda wa kufanya mambo mengine
 
CCM na masalia na zitto mwenyewe hawatatutoa kwenye agenda ya mabadiliko he has to go,
 
Mie natoa ushauri kuwa, viongozi wabuni utaratibu mzuri ili sisi wanachama tuamue hatima ya Zitto.
 
Mkuu tatizo ni ombwe kubwa na udhaifu mkubwa wa kiongozi unaodhihirishwa wazi wazi na the so called Kamati Kuu ya chama, Pamoja na mwenyekiti Mbowe, Hao ndio waliolitibua na kutupa matumain mengi lakin sasa wapo kimya na kutuacha wanachama tukitoleana kashfa sisi kwa sisi tusijiue tushike lipi na tuache kipi, Hii inanikumbusha novel ya "The Beautyful ones are not yet born " ambapo bus driver(President Nkurumah) alikuwa akiendesha gari lakin hajui nin kinatokea nyuma kati ya conductor na abiria.
 
Mie natoa ushauri kuwa, viongozi wabuni utaratibu mzuri ili sisi wanachama tuamue hatima ya Zitto.
Si mwenzenu huyo cdm.huoni hata mapokezi yake kigoma walizuia watu wasipeperushe bendera pia wasivae sare za cdm?
 
Si mwenzenu huyo cdm.huoni hata mapokezi yake kigoma walizuia watu wasipeperushe bendera pia wasivae sare za cdm?

Ndio maana nimetoa ushauri kuwa hii issue wairudishe kwetu sisi wanachamana tuamue, Chadema tunaamini katika nguvu ya umma..
 
Chadema ni chama chenye nguvu sana na kinaweza kuchukua madaraka ndani ya nchi hivo wanapaswa kuaminiana na kuwa kma timu ili kuweza kufikia malengo ila akijitokeza mtu akawa tofauti na wenzake!{msaliti}anapaswa kuondolewa bila kujali anawadhifa gani ndani ya chama!!
 
Mimi nadhani waendelee kutimuana hadi abaki babu na dj tu,..pamoja na wabeba sumu bila kusahau dj
 
Mimi nakufa na kamati kuu CDM Hivi Chadema ni mali ya Zito au Kwani zito ameonywa mara ngapi hivi mkimfukuza kunatatizo gani mpaka mtupotezee muda wakumfukuza sheta huyu ambaye sasa anajiona ye ndo yeye hamjui kua kuchelewesha maamuzi mnachangia kuangamiza chama tukisema CC yote sasa huenda nayo imenunuliwa,tutakua tumekosea kama kweli hakuna aliye juu ya chama, kwanini mumng'ang'anie zito wanasema hata kitoeo ukipendeje kikisha chacha haunabudi kukimwaga, ukilazimisha kukila utapata mathala wote tulimpenda Zito ila kahalibika afukuzwe kuchelewa kumfukuza kutakua namathala makubwa kwani kwasasa Zito anajua anachokifanya na wafuasi wake.
 
Ushauri wako nauunga mkono, chama hakijengwi kwa mifarakano hata kidogo, chama ni viongozi, chama ni vikao, na chama ni wana chama! Migogoro hii inawanufaisha ccm na kuwabomoa wapinzani. Matendo ya wapinzani yanawafanya kuelekea 2015 ikulu iwe ndoto!
 
Back
Top Bottom