Ushauri Unahitajika: Mhimu Sana

Ushauri Unahitajika: Mhimu Sana

guzman_

JF-Expert Member
Joined
Jan 27, 2016
Posts
1,276
Reaction score
2,435
Habari za weekend wanaMMU
NI hivi.
Mwaka 2015 nilianza mahusiano na single maza mmoja hapa mkoani. Wakati huo alikuwa anafanya kazi kama mpishi kwenye mgahawa mmoja. Japo alikuwa single maza umri wake ulikuwa bado sana (22). Na ifahamike kuwa nilikuwa nimeshaoa na mke alikuwa akiishi mkoa tofauti. Nilikuwa muwazi kwake na aliheshimu hilo. 2016 tukapata mtoto wa kiume na nilimwachisha kazi na nikamsaidia kujenga nyumba kwenye kiwanja chake na kumpa mtaji wa kuuza nafaka. Kweli alionyesha ukomavu sana kwenye biashara mtaji ulikuwa na ikafika kipindi akawa na 10m kwenye akaunti yake.
2017 mwanzoni akabadilika akaanza maneno ya shombo na kusema hawezi endelea kudate na mme wa mtu. Nikasema sawa ila anipe ruhusa ya kwenda kumwangalia kijana wangu pale nikiwa nahitaji akakubali. Baada kama ya miezi 4 nikaenda kwake kumcheki mtoto kweli nilimkuta pale anacheza nje nikamchukua nikataka kwenda nae ndani sebureni kuingia naona akipigana denda na kijana mmoja sharobaro.
Nikavunga nikamwomba aje nje akanifokea sana kwa nini naenda bila taarifa. Nilichofanya nika chomoa laki 2 nikampa nikamwambia amfanyie shopping mtoto akagoma nikang'oa nanga.
Nikafanya upelelezi kumbe kale kajamaa kalikuwa graduate wa chuo na yule mchepuko wangu ndio alikuwa shuga mammy wake. Nikapiga moyo konde niliumia sana ila nikasema wacha iwe. Yule kijana alianza biashara na yule mama, kijana anaenda huko mikoani kutafuta nafaka yeye anauza. Baadaye nilisikia kijana alipewa kama 15m akatokomea nazo mwanza huko. Mama mtaji ukakata akaenda benki kukopa wakauza nyumba yake. Akahamia chumba kimoja kupanga.
Nilibadili lini so alikuwa hana uwezo wakunipata na niliondoka ule mkoa. Last week nilipata safari ya huko ndo nikaenda kumtafuta. Alikuwa kachoka sana na kijana wangu alikuwa ndo kama hajala siku mbili. Sikutaka kuongea nae nikampa business card nikampa laki 2 nikasepa.
Jioni yake akanipigia nikamwambia aje Hotel flani akaja nikapiga nae story mpaka saa 7 usiku nikamtafutia tax akaondoka.
Inshort ni kuwa hana kazi mtaji ulikata na aliuziwa nyumba hana ramani na ametokea familia duni sana.
Kabla nilimwomba kama ataniruhusu kumwoa mke wa pili alikubali ila baadaye baada ya kupata huyo kijana ndo akakengeuka. Sasa ivi ananiomba huku analia nimsamehe na yuko tayari kuolewa tumlee mtoto wote.
Ila mimi nataka nifanye utaratibu wa kumchukua kijana nikae nae yeye aendelee na shughuli zake. Shughuli ipo kwenye kumweleza bibi mkubwa aweze kumpokea huyu bwana mdogo. Najua kuna watu walishapitia haya nipeni ushauri namna ya kukabiliana na hili.
Asanteni Sana.
 
Shughuli ipo kwenye kumweleza bibi mkubwa aweze kumpokea huyu bwana mdogo. Najua kuna watu walishapitia haya nipeni ushauri namna ya kukabiliana na hili.
hili na mimi jibu nalitaka kwa kuwa ninampango wa kutafuta kidi nje ya fance
 
Broo guzman_ uliteleza na kuteleza si kuanguka kaka, ulijitahidi sana lakini ndio haikuwezekana. Bi mkubwa nina hakika hatokuwa na tatizo hata kidogo kama utampeleka huyo dogo kwake, tena nauhakika atafurahi sana, hoja hapa umueleze ukweli kwa jinsi ulivyotueleza hapa, hawa watu Mungu kawaumba na moyo wa ajabu sana, ila kaka mkubwa mi nikuombe kitu kimoja. tafuta walau laki tano muite huyu mzazi mwenzako mueleze tu kwa ustarabu kwamba achukue hio aanze biashara upya, na kwamba sasa akuruhusu umsaidie kulea huyo mtoto wakati yeye anahangaika kukuza mtaji, namba za simu anazo haitakuwa shida kuja kumuona mtoto katika utaratibu Fulani muda wowote ataohitaji. Utaishi kwa Amani sana kaka!!!!! Jirani yangu alifata damu yake kigoma ndani ndani huko, alivyokuja kwa Bi mkubwa na kumueleza Bi mkubwa alilia machozi ya furaha.
 
Wazazi wako umewaeleza? Wewe unamfahamu vzr mkeo kwahiyo unajua ukimweleza atatoa reaction gani ila yote kwa yote ww tafuta wakati mwafaka umwambia hata kama akigoma kumleta mtoto nyumbani basi mpeleke kwa wazazi wako tu
 
huyo achana nae anaonekana ana pepo la usingo maza, fanya juu chini umchukue mtoto
 
Kama kweli ulikuwa una mpango wa kumuoa awe mke wa 2 sioni kama kuna tatizo kumuambia mkeo kuhusu huyo kijana wako.
 
Tafuta shule nzuri ya garama,peleka mtoto bweni;hapo utakuwa umefanya uamuzi usioumiza upande wa bi mkubwa.
 
Kitanda hakizai kharamu nenda Kwa mkeo mwambie ulizaa nje akileta nongwa zake piga chini baki na watoto wako uwalee mwenyewe hela si unayo ya kuwahudumia
Sio rahisi kama unavyodhani na hela sio kila kitu
 
Wewe ndio wamjua mkeo kinagaubaga..Jishushe ongea na mkeo..naamini atakuelewa na kumpokea mtoto kikubwa acha kabisa mawasiliano na huyo kubwa jinga
 
Kitanda hakizai kharamu nenda Kwa mkeo mwambie ulizaa nje akileta nongwa zake piga chini baki na watoto wako uwalee mwenyewe hela si unayo ya kuwahudumia
Hapa pagumu sana
 
Broo guzman_ uliteleza na kuteleza si kuanguka kaka, ulijitahidi sana lakini ndio haikuwezekana. Bi mkubwa nina hakika hatokuwa na tatizo hata kidogo kama utampeleka huyo dogo kwake, tena nauhakika atafurahi sana, hoja hapa umueleze ukweli kwa jinsi ulivyotueleza hapa, hawa watu Mungu kawaumba na moyo wa ajabu sana, ila kaka mkubwa mi nikuombe kitu kimoja. tafuta walau laki tano muite huyu mzazi mwenzako mueleze tu kwa ustarabu kwamba achukue hio aanze biashara upya, na kwamba sasa akuruhusu umsaidie kulea huyo mtoto wakati yeye anahangaika kukuza mtaji, namba za simu anazo haitakuwa shida kuja kumuona mtoto katika utaratibu Fulani muda wowote ataohitaji. Utaishi kwa Amani sana kaka!!!!! Jirani yangu alifata damu yake kigoma ndani ndani huko, alivyokuja kwa Bi mkubwa na kumueleza Bi mkubwa alilia machozi ya furaha.
Thanks mkuu
 
Wewe ndio wamjua mkeo kinagaubaga..Jishushe ongea na mkeo..naamini atakuelewa na kumpokea mtoto kikubwa acha kabisa mawasiliano na huyo kubwa jinga
Ni kweli ila kila nikitamani kunyanyua mdomo nimweleze naona mambo mengi yatabadilika
 
Habari za weekend wanaMMU
NI hivi.
Mwaka 2015 nilianza mahusiano na single maza mmoja hapa mkoani. Wakati huo alikuwa anafanya kazi kama mpishi kwenye mgahawa mmoja. Japo alikuwa single maza umri wake ulikuwa bado sana (22). Na ifahamike kuwa nilikuwa nimeshaoa na mke alikuwa akiishi mkoa tofauti. Nilikuwa muwazi kwake na aliheshimu hilo. 2016 tukapata mtoto wa kiume na nilimwachisha kazi na nikamsaidia kujenga nyumba kwenye kiwanja chake na kumpa mtaji wa kuuza nafaka. Kweli alionyesha ukomavu sana kwenye biashara mtaji ulikuwa na ikafika kipindi akawa na 10m kwenye akaunti yake.
2017 mwanzoni akabadilika akaanza maneno ya shombo na kusema hawezi endelea kudate na mme wa mtu. Nikasema sawa ila anipe ruhusa ya kwenda kumwangalia kijana wangu pale nikiwa nahitaji akakubali. Baada kama ya miezi 4 nikaenda kwake kumcheki mtoto kweli nilimkuta pale anacheza nje nikamchukua nikataka kwenda nae ndani sebureni kuingia naona akipigana denda na kijana mmoja sharobaro.
Nikavunga nikamwomba aje nje akanifokea sana kwa nini naenda bila taarifa. Nilichofanya nika chomoa laki 2 nikampa nikamwambia amfanyie shopping mtoto akagoma nikang'oa nanga.
Nikafanya upelelezi kumbe kale kajamaa kalikuwa graduate wa chuo na yule mchepuko wangu ndio alikuwa shuga mammy wake. Nikapiga moyo konde niliumia sana ila nikasema wacha iwe. Yule kijana alianza biashara na yule mama, kijana anaenda huko mikoani kutafuta nafaka yeye anauza. Baadaye nilisikia kijana alipewa kama 15m akatokomea nazo mwanza huko. Mama mtaji ukakata akaenda benki kukopa wakauza nyumba yake. Akahamia chumba kimoja kupanga.
Nilibadili lini so alikuwa hana uwezo wakunipata na niliondoka ule mkoa. Last week nilipata safari ya huko ndo nikaenda kumtafuta. Alikuwa kachoka sana na kijana wangu alikuwa ndo kama hajala siku mbili. Sikutaka kuongea nae nikampa business card nikampa laki 2 nikasepa.
Jioni yake akanipigia nikamwambia aje Hotel flani akaja nikapiga nae story mpaka saa 7 usiku nikamtafutia tax akaondoka.
Inshort ni kuwa hana kazi mtaji ulikata na aliuziwa nyumba hana ramani na ametokea familia duni sana.
Kabla nilimwomba kama ataniruhusu kumwoa mke wa pili alikubali ila baadaye baada ya kupata huyo kijana ndo akakengeuka. Sasa ivi ananiomba huku analia nimsamehe na yuko tayari kuolewa tumlee mtoto wote.
Ila mimi nataka nifanye utaratibu wa kumchukua kijana nikae nae yeye aendelee na shughuli zake. Shughuli ipo kwenye kumweleza bibi mkubwa aweze kumpokea huyu bwana mdogo. Najua kuna watu walishapitia haya nipeni ushauri namna ya kukabiliana na hili.
Asanteni Sana.
Hahaha aseee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom