uwezo mdogo sana kwani sina kazi kwani nilipata mimba nikiwa chuo cha ualim na sikuweza kuendelea
Pole sana mamii... kama wewe ni muumini mi nakushauri usali zaidi. Mwenyezi Mungu aliwaleta viumbe hao wazuri duniani kwa mpango mwema na hakika hatawaacha waadhirike.
Tumia tu lugha ya upole na unyenyekevu kumkumbusha baba yao juu ya jukumu lake kushiriki malezi ya wanae. Inawezekana ni umri unamsumbua, lakini hata mapepo. Pengine Mwenyezi Mungu anataka kukutumia wewe umuombee ili ambadilishe. Na pengine Mwenyezi Mungu ataitumia sauti yako kumfikishia ujumbe. Sauti ya Mungu ni sauti ya upole.
Siku ukijisikia kuongea nae kwa upole, jua ni sauti ya Mungu, lakini siku ukigombana nae au kumfokea, jua ni vishawishi vya shetani.
Wapende wanao na mpende baba yao. Hao watoto ni baraka za Mungu, na siku zote Mungu ni UPENDO, sio kesi wala magomvi, sio uchawi wala masengenyo.