Kama nimekuelewa vizuri biashara yako inahusu fani yako.Hiyo ni faida kubwa kwako maradufu.Kwa kuwa bado ni mwajiriwa miezi sita ya kwanza jipange vizuri na wewe na mkeo mjiandae kisaikolojia,pesa ya mshahara unayoipata ifanyie utaratibu wa akiba kwa miezi kama sita hivi.Baada ya huo muda omba likizo ukasimamie mwenyewe biashara yako na ufanye udhibiti mzuri wa mapato na matumizi yako katika kipindi chote cha likizo yako nzima.Iwapo utaifanya biashara yako ambayo kama ulivyosema ndiyo fani yako kwa ufanisi katika kipindi cha likizo yako, utakuwa tayari umejifunza mazingira ya ofisi yako mpya.Baada ya likizo nenda kaage kazini kuwa maisha yako sasa yako katika mikono na akili yako badala ya kutumiwa na tume taa kwa ujira mdogo hivyo.Niamini baada ya miaka mitano utagundua na kujutia muda uliopoteza kwa kuajiriwa.Karibu katika maisha ya kweli.
Alafu suala la kuacha kazi haliitaji ushauri, wala anayeacha kazi haweki matangazo!! Hili suala linatoka ndani, maana ni mustakabali wa maisha yako mwenyewe na si hao ndugu!!
Kwa huu wasiwasi wako ni heri ukaendelea na ndoa yako tu, huku mziki wake hutuweza!!
Ni kweli bro ,kupitia Biashara kuna Wa zaidi ya sita wamepata ajira na zaid ya hapo nalipa kodi ya serikali hivyo kuongeza pato la taifa, binafsi z sirizishwi na maisha ya wastaafu wengi wa serikali,najua nikiishi kama alivyoishi baba angu siweza pata maisha tofauti na wanayoishi watumishi wengi,taabia ya kumaliza charge ya simu kuangalia mshahara kama umetoka au la !? Inanikera sana.
Malengo yangu ni kuwa mfanyabiashara nitakayetoa ajira pia kwa watz wenzangu,kwani huwa inaniuma sana ninapoona nafasi 3 zinagombewa na watu 3000. Naomba Mungu anio gezee ujasiri ili niweze Fanya maamuzi magumu kwani binafsi naamini hakuna mafanikio yanayopatikana kwa maamuzi mepesi
Nina imani ukiamua unaweza kufanya kazi na wakati huo huo biashara inawezekana kabisa.. Faida yake ni kuwa utazidi kuongeza kipato n at the same time ni security tosha kwani una uhakika w mshahara mwisho wa mwezi.. Cha muhimu andaa mazingira mazuri ya usimamizi wa biashara zako
Acha ujinga wewe kama mengi na bakhresa wangengangania ajira, azam tv na itv zingekuwepo
Huu uoga tu. Kimsingi kama mtu ni mjasiriamali mzuri hela atakayopiga kwenye ujasiriamali hata afanyeje huko kazini changanya na biashara hapati.
Turudi kwenye mada:
Mkuu suala la msingi ni wewe unataka kufanya nini kwenye maisha yako. Huo ushauri hapo juu umejaa woga mwingi sana. Ukweli ni kwamba ukiacha kazi kuna mawili aidha utafanikiwa au unaweza kuanguka,na ni lazima ujiandae kisaikolojia kukubaliana na lolote kati ya hayo. Huo ndio ukweli na hakuna namna ya kukwepa hilo suala. Sema kuanguka pia sio mwisho wa maisha, unaweza kuanguka hata mara 100 na bado ukasimama tena alimradi tu uwe hai.
Kuna watu wamekushauri hapo juu kuwa ufanye utafiti ujiridhishe kuwa hiyo biashara ni endelevu. Ukweli ni kwamba hata ufanye utafiti wa aina gani huwezi kuwa na uhakika wa 100% na matokeo ya uamuzi wako huko mbeleni. Kitu cha msingi ni kwamba unapotaka kufanya uamuzi wowote hususan kwenye suala linalohusu maisha kama hili angalia kama ni kweli unataka kufanya hivyo na kama ndivyo je viashiria vinaonesha mafanikio mbeleni? Kama jibu ni ndiyo unachotakiwa kufanya ni kuamua na unapoamua unakuwa umekubali "kurisk". Usije kudanganyika kwamba ukitoka huko ni lazima ufanikiwe si kweli, narudia unaweza kufanikiwa au kuanguka.
Point unayotakiwa kuchukua hapa ni hii:
Kuanguka ni uwezekano lakini hata ikitokea utainuka na kuendeleza mapambano. Maisha ni kama vita tu.
Sio kwamba naanza au nataka kuanza nipo kwa hii game miaka 2 sasa,
Jamani Mimi ni mtumishi Wa halmashauri na mshahara wangu ni 1,100,000/= , pia nafanya Biashara amba inanilipa sana na kama nikiwekeza nguvu na muda wangu wote huko naamini in five years, umasikini kwangu utakuwa historia. Ila kila ninapoomba support kutoka kwa familia including my wife ili niache Kazi na kuendelea na Biashara hakuna anayeniunga mkono,Mke ndo anakuwa mkali kweli,mama anasema nisije muuwa kwa presha.Deep in my heart najua kabisa for sure utumishi huku kwa local government ni kuendeleza tu chain of poverty unless uwe mwizi. Naomba ushauri nifanyeje?
Wazo zuri,biashara anza taratibu ukiwa kazini na nenda nayo taratibu. Biashara inalipa ila ina risk na uncertainity kubwa. Mie ningekushauri anzisha biashara ya kitaasisi ili utumie labour+capital combination model wewe ubaki kazini na ufanye managerial functions tuu. Kumbuka hakuna kitu rahisi. Ninafanya biashara mwaka wa nne sasa toka nitoke chuo. Njoo kwenye biashara ado ado. Karibu na uwe na kifua
When you started the business, probably your wife, your brother, your friends didn't advise you. You saw the opportunity and you exploited it. Why do you think they will support your decision to quit your current job? They have always associated your success in business to luck and your current job. However, if they associate it to your ability to think, work hard, supervise, they will see you as person who can successed in business as well.
Mkeo anajua ambitions n ndoto zako maishani au ile bora liendele. Wengi wanakosea sana kabla ya kuoa. Hilo ni moja ya vitu ambavyo ur life partner lazima avijue kuhusu wewe na kinyume chake. Naona mtafaruku hapo na Bi. Mkubwa nae pia anaingia vipi kwenye halmashauri ya familia kama mshauri/mpendekezaji au sehemu ya uamuzi. Binafsi kama naweza fanya kazi/ biashara miaka 5 nikafikia pale ninapotaka nastaafu hata iwe ikulu ya wapi sio halmashauri tu...maisha ni zaidi ya ajira ndugu, fanya maisha.
Bakhresa hakuwa na choice ya kuacha kazi. Ile kazi aliyokuwa anaifanya ndiyo option pekee aliyokuwa nayo kwa kipindi kile anaanza. Halafu kazi si mbaya sana kama watu wanavyofanywa waamini, kwa mfano CEO wa airtel naye pia si mfanyakazi au?
Pigaaa kazii achaaa upuuzii ....hata km mshahar mdogo hlf una biashara sio kigexooo we kulaaa helaaa za serikali hizooo wakikutibuaa unaonesha makuchaaaaa
unafikiri na ngozi yako nyeusi na elimu yako ya vyuo vya kibongo utapews u ceo wa airtel...
ukitoa shirika la uma ttcl,,,nitajie kampuni moja tu ya simu multinational yenye ceo mweusi