Ushauri: Mbowe na CHADEMA rudini Bungeni japo kwa aibu

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Feb 17, 2016
17,506
16,003
Igwe wana JF!

Nimelazimika nimshaurriMbowe na WWabunge wake kurejea bungeni iijapokuwa kuna aibu mtakayopata kutokana na kiapo chenu ambacho hakina mantiki.Zingatia yafuatayo;

Wananchi katika majimbo takriban 70+ ya UKAWA wamekosa mtu wa kuhoji utekelezaji wa miradi ya barabara,afya,elimu nk na jana alhamisi KUB Mbowe umekosa fursa ya kumuhoji waziri mkuu maswali ya papo kwa papo.Mmetutia hasara!

Sababu zenu za kugoma ni malalamiko tu ambayo huwezi kumtia mtu hatiani,chuki yenu kwa Naibu Spika ilianza tokea siku ameteuliwa na CCM,mlitoa vijisababu vingi na hata kupendekeza baadhi ya wabunge ndani ya CCM angali mlikuwa na mgombea wenu Magdalena Sakaya.Mlitengeneza chuki binafsi na hata Lissu akahoji ni lini Tulia alijiunga CCM?,ni moja ya swali la kisiasa ambalo kimantiki na kiueledi huulizwa na mjinga.

Kwasasa mmeshotoa hati kwa Spika ya kumvua madaraka Naibu Spika sasa ili kuheshimu demokrasia yawapasa muingie bungeni mkisubiri hatma.Kule Afrika kusini mara kadhaa wabunge wa upinzani wametoa hoja kumuondoa spika wa bunge Bi.Beleka Mbete na wameshindwa kwa hoja na kura bungeni bila kutoka.Msiporudi Bungeni na hoja yenu ikashindwa dhamira zenu zitawasuta na mtajikuta mkitekeleza majukumu kwa kiwango cha chini.

Mmeonyesha silaha zenu za mwisho ndani ya miezi sita hakika mmejiweka katika nafasi kubwa ya anguko.Serikali imefanya mambo muhimu mapema ambayo kisiasa ni lazima uyafanye sasa ili katika mwaka wa tatu,nne na tano wa awamu ya kwanza wananchi wapate matunda ya mabadiliko hivyo kujihalalishia ushawishi kwa wananchi wengi walio maskini.Awamu ya kwanza ya mkapa alibezwa sana mwanzoni,watu wakaita zama za ukapa/ukata kutokana na sera ya kusimamia misingi na kubana matumizi na wananchi wakamwamini wakamchagua tena 2000 kwa asilimia 82 kutoka 60 aliyopata 1995.

Wanafunzi wa Chuo kikuu waligoma kudai nyongeza ya "boom" kutoka 1500 hadi 2500,Mkapa alimtuma aliyekuwa Mkurugenzi wa Elimu ya Juu Bw.Ahmed Mbegu kuzungumza na wanafunzi, wakakataa eti wanamtaka Raisi manake Sumaye alidharaulika sana na jumuiya ya Chuo kikuu,mgomo ukazidi likabandikwa tangazo kuwa kufika saa 10 jioni hairuhusiwi mwanafunzi yeyote kuonekana hostel wala darasani FFU wakasimamia zoezi kwa virungu na vichapo kwa waliokaidi.Baada ya hapo migomo ya kijinga iliisha na kubaki masuala ya msingi.

Mbowe na wabunge wengine wa Ukawa hamna jinsi aibu ya kiapo haiepukiki japo ni busara kurudi mapema kwa sababu hamtapata matokeo na watu wameshawaona nyie ni wakawaida.

Nawasilisha.
 
Bunge lipo mkutano wa 3 bado 17 ili bunge livunjwe. Je CHADEMA wataweza kususia kwa muda wote bila kujua ni mikutano ipi ya Bunge itaongozwa na Naibu Spika. Itawaondolea umakini NA wametoa nafasi kwa CCM kuwazingua kwa urahisi sana.
 
Hoja za UKAWA nyepesi sana zaidi wana wanazidi kujianika kweupe na kuwajua zaidi jinsi walivyo na siasa nyepesi.
 
Bunge lipo mkutano wa 3 bado 17 ili bunge livunjwe. Je CDM wataweza kususia kwa muda wote bila kujua ni mikutano ipi ya Bunge itaongozwa na Naibu Spika. Itawaondolea umakini NA wametoa nafasi kwa CCM kuwazingua kwa urahisi sana.
Hili jambo ni gumu kutekelezeka!
 
Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania pamoja na sheria, kanuni na taratibu huongozwa pia kwa kufuata "utamaduni" wa mabunge ya jumuiya ya madola na maamuzi ya maspika waliopita.

Kwa jinsi wanavyoenenda wabunge wa upinzani wapo "NJIA ILIYO SAHIHI"
 
Si ndio mfurahi mambo yenu CCM mtayapitisha bila usumbufu wowote!
Kila siku unamtukana Mbowe,leo unamshauri!Yawezekana umeshaona matokeo chanya kwa upande wao kwa kile wanachokifanya!
Mbowe na wengine,shikilieni hapo hapo
 
Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania pamoja na sheria, kanuni na taratibu huongozwa pia kwa kufuata "utamaduni" wa mabunge ya jumuia ya madola na maamuzi ya maspika waliopita.

Kwa jinsi wanavyoenenda wabunge wa upinzani wapo "NJIA ILIYO SAHIHI"
Haya tusubiri.
 
Si ndio mfurahi mambo yenu ccm mtayapitisha bila usumbufu wowote!
Kila siku unamtukana mbowe,leo unamshauri!Yawezekana umeshaona matokeo chanya kwa upande wao kwa kile wanachokifanya!
Mbowe na wengine,shikilieni hapo hapo
Sina kumbukumbu ya siku nimemtukana Mbowe bali namkosoa.Nimemshauri kwani hatafika mbali anajitengenezea ugumu mwenyewe siku za usoni.
 
hao wanakaa bungeni kila siku mbona majimbo yao maskini sana kuliko hata majimbo ya wapinzani,wanachojuwa hao ni kugonga meza na kuitikia ndiooooooo....
 
hao wanakaa bungeni kila siku mbona majimbo yao maskini sana kuliko hata majimbo ya wapinzani,wanachojuwa hao ni kugonga meza na kuitikia ndiooooooo....
Kwahiyo unataka kusema majimbo ya wapinzani ni tajiri kutokana na kazi iliyofanywa na wabunge hao ndani ya miezi 6?
 
Hebu hata siku moja njoo hapa mkosoe Magufuli hata kwa jambo moja!Mnaelekeza nguvu nyingi kuwakosoa wasio na dola badala kuelekeza nguvu kuwaangalia walioko madarakani!
Kila siku upinzani hiki,upinzani kile,mbowe kafanya hiki,mbowe afanye hiki!
Hebu badilikeni,hojini serikali itawezaje kutekeleza ahadi yake kama changamoto ndogo zinatusumbua sana!
Mwambieni Magufuli aache kupambana na demokrasia na badala yake apambane na mafisadi!Mwambieni kauli zake kwa masikini zinawaacha na maumivu makali na kumuona hana utu(rejea kauli yake kwa wanafunzi wa UDOM).
Mwambieni asimpake JK mafuta kwa mgongo wa chupa,anamsifia kwa mambo mengi ila anawatukana watoto wa udom ambao ni zao la mpango wa huyo huyo JK!
 
Hebu hata siku moja njoo hapa mkosoe Magufuli hata kwa jambo moja!Mnaelekeza nguvu nyingi kuwakosoa wasio na dola badala kuelekeza nguvu kuwaangalia walioko madarakani!
Kila siku upinzani hiki,upinzani kile,mbowe kafanya hiki,mbowe afanye hiki!
Hebu badilikeni,hojini serikali itawezaje kutekeleza ahadi yake kama changamoto ndogo zinatusumbua sana!
Mwambieni Magufuli aache kupambana na demokrasia na badala yake apambane na mafisadi!Mwambieni kauli zake kwa masikini zinawaacha na maumivu makali na kumuona hana utu(rejea kauli yake kwa wanafunzi wa UDOM).
Mwambieni asimpake JK mafuta kwa mgongo wa chupa,anamsifia kwa mambo mengi ila anawatukana watoto wa udom ambao ni zao la mpango wa huyo huyo JK!
Kumkosoa anapokosea atamkosoa na kama umeona kakosea Saidia kukosoa.
Magufuli si Mnafiki, anaita Kilaza pale unapokuwa kilaza na anakusifia pale unapostahili sifiwa.
Anamsifia JK kwa mazuri yake, na atamponda kwa uzembe wa kutofuatilia, kutojar yanayoendelea
 
Hebu hata siku moja njoo hapa mkosoe Magufuli hata kwa jambo moja!Mnaelekeza nguvu nyingi kuwakosoa wasio na dola badala kuelekeza nguvu kuwaangalia walioko madarakani!
Kila siku upinzani hiki,upinzani kile,mbowe kafanya hiki,mbowe afanye hiki!
Hebu badilikeni,hojini serikali itawezaje kutekeleza ahadi yake kama changamoto ndogo zinatusumbua sana!
Mwambieni Magufuli aache kupambana na demokrasia na badala yake apambane na mafisadi!Mwambieni kauli zake kwa masikini zinawaacha na maumivu makali na kumuona hana utu(rejea kauli yake kwa wanafunzi wa UDOM).
Mwambieni asimpake JK mafuta kwa mgongo wa chupa,anamsifia kwa mambo mengi ila anawatukana watoto wa udom ambao ni zao la mpango wa huyo huyo JK!
Mkuu mbona wewe hakuna siku umemsifu Magufuli?Wewe mkosoe Magufuli mimi namkosoa Mbowe.Hakuna Malaika.
 
Hebu hata siku moja njoo hapa mkosoe Magufuli hata kwa jambo moja!Mnaelekeza nguvu nyingi kuwakosoa wasio na dola badala kuelekeza nguvu kuwaangalia walioko madarakani!
Kila siku upinzani hiki,upinzani kile,mbowe kafanya hiki,mbowe afanye hiki!
Hebu badilikeni,hojini serikali itawezaje kutekeleza ahadi yake kama changamoto ndogo zinatusumbua sana!
Mwambieni Magufuli aache kupambana na demokrasia na badala yake apambane na mafisadi!Mwambieni kauli zake kwa masikini zinawaacha na maumivu makali na kumuona hana utu(rejea kauli yake kwa wanafunzi wa UDOM).
Mwambieni asimpake JK mafuta kwa mgongo wa chupa,anamsifia kwa mambo mengi ila anawatukana watoto wa udom ambao ni zao la mpango wa huyo huyo JK!

Kumbe Tulia Akison naibu spika ndiye Magufuri ? nimeamini maneno ya Lusinde kuwa kuna watu akili zao kama watoto walio tumboni mwa mama zao bado wakidhani tumbo la mama ndiyo.

Hoja zilizowatoa zipo bungeni JPM hayupo huko. Je enzi za JK wapinzani walitoka nje sababu ya kiti kukaliwa na Tulia au ubabe wa JPM ? mazoea hujenga tabia,ukijizoeza kulalamika daima utasalia kulalamika.
 
Ugonjwa wa kichaa huanzia kwenye kuropoka. Natumaini unapokea ushauri nasikia watu wa aina yako wanashauriwa kutumia omega3
 
Maajabu ya nchi hii ni kila mtu anajua, Rais hakosei na wala wapinzani nao hawakosei
 
Back
Top Bottom