Jamani tufanye kazi.
Hakuna serikali au mtu atakayekuletea mafanikio bila kufanya kazi.
Vijana tumekumbwa na pepo la malalamiko. Kila kitu tunalaumu, tunalaumu wazazi, viongozi, elimu tuliyopewa, tunalaumu wenzetu wakifanikiwa.
Tutoke nje ya malalamiko, tujitazame tumefanya nini kubadili hali zetu.
Nchi yetu ni nzuri ina fursa nyingi za kujiendeleza. Kuna vijiji unapata hata acre 5 kwa laki moja. Tuna soko kubwa la ndani kwa bidhaa yoyote itakayozalishwa kwa umakini.
Tuache mambo ya kulaumu laumu tu.
Wanaokuambia biashara ngumu serikali haiwaangalii wanaoanza na mtaji mdogo wao walianzaje? Kwanini wewe usianze kama wao?
Wanalalamika bei ya mbolea lakini wanalima, kwanini na wewe usilime?
Unalalamika hakuna ajira lakini wapo wanaoajiriwa?
Wenzako wanaendelea,wanaanza maisha wanajenga, wanaongeza vipato wanakuwa na familia bora wewe unaendelea kulaumu tu.
Mwisho umefeli kimaisha story yako kwa kizazi chako itakuwa ni ipi? Serikali imenifanya niwe maskini au itakuwa pamoja na vikwazo vingi lakini bado nimetoboa.
Hakikisha hupotezi muda wako mwingi kwenye kulaumu wengine maana hutafanikiwa kamwe. Shauri huku unafanya kazi. Ukiona mwenzako kafanikiwa jifunze usianze kujiwekea dhania kuwa ni fisadi au nguvu za giza.
Hakuna heshima kwenye umaskini.
Hakuna serikali au mtu atakayekuletea mafanikio bila kufanya kazi.
Vijana tumekumbwa na pepo la malalamiko. Kila kitu tunalaumu, tunalaumu wazazi, viongozi, elimu tuliyopewa, tunalaumu wenzetu wakifanikiwa.
Tutoke nje ya malalamiko, tujitazame tumefanya nini kubadili hali zetu.
Nchi yetu ni nzuri ina fursa nyingi za kujiendeleza. Kuna vijiji unapata hata acre 5 kwa laki moja. Tuna soko kubwa la ndani kwa bidhaa yoyote itakayozalishwa kwa umakini.
Tuache mambo ya kulaumu laumu tu.
Wanaokuambia biashara ngumu serikali haiwaangalii wanaoanza na mtaji mdogo wao walianzaje? Kwanini wewe usianze kama wao?
Wanalalamika bei ya mbolea lakini wanalima, kwanini na wewe usilime?
Unalalamika hakuna ajira lakini wapo wanaoajiriwa?
Wenzako wanaendelea,wanaanza maisha wanajenga, wanaongeza vipato wanakuwa na familia bora wewe unaendelea kulaumu tu.
Mwisho umefeli kimaisha story yako kwa kizazi chako itakuwa ni ipi? Serikali imenifanya niwe maskini au itakuwa pamoja na vikwazo vingi lakini bado nimetoboa.
Hakikisha hupotezi muda wako mwingi kwenye kulaumu wengine maana hutafanikiwa kamwe. Shauri huku unafanya kazi. Ukiona mwenzako kafanikiwa jifunze usianze kujiwekea dhania kuwa ni fisadi au nguvu za giza.
Hakuna heshima kwenye umaskini.
