Ushauri kwa serikali namna ya kumaliza mgogoro na Nchi Wahisani

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,014
144,372
Baada ya nchi nyingine wahisani kuungana na Marekani katika kusitisha misaada,naona itakuwa vigumu sana kwa serikali kupuuza jambo hili licha ya kauli za kujitutumua kuwa tunaweza ku-manage kuendesha nchi bila misaada ya wahisani.

Huenda tunaweza lakini tatizo ni kuwa hatukujipanga na tunahitaji muda kujipanga na muda huo kwa sasa haupo kwani tumeshachelewa.

Hivyo,kwa mtazamo wangu,naishauri serikali kuunda kitu kinachoitwa "Goverment Negotiating Team" kwenda kuonana na nchi wahisani kutafuta suluhu ya mgogoro huu.

Kwa sasa tunaweza kuweka msimamo wa kuachana na bwana wakubwa hawa ila wakati utafika tutajikuta tunakwama na tutapaswa kuwarudia kwa aibu unless serikali ichukue hatua za dharura kupunguza matumizi yasiyo ya lazima kuanzia Ikulu mpaka kwenye ofisi ya Mtendaji wa Mtaa.

Hata hivyo,tukumbuke tuna changamoto za kuandaa uchaguzi wa serikali za mitaa,deni la Taifa,milioni 50 kwa kila kijiji,elimu bure,kura ya maoni au kuanza upya kwa Bunge la katiba, fedha za kuendesha Bunge la Bajeti,n.k.Tusipokuwa makini tutajikuta hakuna miradi ya maendeleo inayofanyika au kukamilika.

Timu hiyo ya Wataalamu inaweza kuundwa na watu wafuatao;

1.Raisi Mstaafu Kikwete(mwenyekiti wa jopo)

2.Waziri wa Mambo ya Nje

3.Waziri wa Fedha

4.Katibu Mkuu Wizara ya Fedha

5.Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi

6.Waziri wa Sheria

7.Katibu Mkuu Wizara ya Sheria

Raisi Mstaafu Kikwete anafaa zaidi kwasababu amekuwa karibu sana na wazungu hawa katika kipindi cha uongozi wake hivyo anaweza kuwa na msaada zaidi katika jambo hili kama mwenyekiti wa Jopo.

Hao wengine kwa nafasi zao wanahusika moja kwa moja na swala hili.

Waziri wa Sheria na Katibu wake Mkuu wanaweza kuhusishwa katika Timu kama watu watakaohusika kutoa ufafanuzi(commitment) ya serikali kuhusu kupitia upya Sheria ya Makosa ya Mtandao.

Watu wengine wanaoweza kuwepo kwenye Timu hii ni mwakilishi wa serikali ya Zanzibar na mwakilishi wa vyama vya siasa ambao watakuwa na wajibu wa kueleza commitment ya serikali ya Zanzibar na Vyama vya Siasa katika kumaliza mgogoro wa uchaguzi wa Zanzibar.

Mwisho,jambo hili liwe funzo katika kuendesha chaguzi zetu na zaidi iwe funzo la sisi kujitegemea kwa kubuni na kusimamia vyanzo vyetu vya mapato na kuachana kabisa na mawazo ya kutegemea wahisani.

Lazima nikiri kuwa ni aibu na fedheha sana kuishi kwa kutegemea misaada lakini ni aibu na fedheha zaidi kubembeleza misaada lakini pia lazima tujiulize tumefikaje hapa na tunatokaje.
 
hivi hii inayoitwa misaada si mikopo ambayo ukikidhi vigezo unakula! kwanini watu hawaipendi wanahubiri kujitegemea
 
Ushauri mzuri sana, mi ukweli nami ningependa tujitegemee lakini kama ulivyo sema hatujipanga kiivo, tunahitaji hizo pesa kwa sasa, na serikali iandae mpango mkakati wa kuondoa au kupunguza kabisa utegemezi , tunaweza kujidanganya tukazima moto pengine kwa kukopa China na kuzidi kuongeza deni
 
Ngoja watu waje wakushambulie kumpendekeza JK , propadanga machinery ya nchi ilishasema hafai hata kama watu wanajua anafaa!
 
hizi thread za kimatonya pelekeni huko ufipa mkakadili the beat way kua ombaomba sio mnatuletea hapa watu serious tunaotaka kujitegemea.
 
hizi thread za kimatonya pelekeni huko ufipa mkakadili the beat way kua ombaomba sio mnatuletea hapa watu serious tunaotaka kujitegemea.
Tumefika hapa kwasababu ya "umatonja" wa miaka 55 tangu tujitawale.

Kama kwa miaka 55 hukuwahi kuuona huo umatonja ndio unakuja kuona leo hii,basi nenda Mirembe for medical check up.
 
Mkuu sawa lakini Kikwete ndiye chanzo cha mgogoro HAFAI HAFAI HAFAI. Pia ujue huu ni mgogoro ulioasisiwa na CCM kwa hiyo msithubutu kuingia kichwa kichwa. Mtazungushwa wee muishie patupu.
 
Jakaya ana matatizo yake mengi sana ila hili la diplomasia hana mpinzani ,alicheza na diplomasia mpaka Membe akaonekana hana kazi ,kumbuka swala la EAC na coalition yao kina Membe na Sita walishakimbilia kutoa sijui matamko gani ,ila Jakaya mwishoni akatuliza Tanzania itakua nchi ya mwisho kujitoa EAC , Anafaa sana kuwa kwenye hiyo timu ,
Mnyarwanda Kagame alijitutumua mpaka kutisha sijui atampiga na asijue amepigwa na nini ,siku kadhaa mbele Kagame yupo na Mkwere Bandarini Dar

Malawi sijui na fyokofyoko zao ,Jk akamtuliza yule mwana mama Joyce banda ,



Tatizo ni nani mwanzilishi wa mgogoro wa Zanzibar ???
 
hizi thread za kimatonya pelekeni huko ufipa mkakadili the beat way kua ombaomba sio mnatuletea hapa watu serious tunaotaka kujitegemea.
check huyu ndondocha kujitegemea wakati jana wamepiga vigeregere kwa msaada wa japan
 
Mkuu sawa lakini Kikwete ndiye chanzo cha mgogoro HAFAI HAFAI HAFAI. Pia ujue huu ni mgogoro ulioasisiwa na CCM kwa hiyo msithubutu kuingia kichwa kichwa. Mtazungushwa wee muishie patupu.
Ni kweli ndio maana nasema waonyeshe commitment na vile vile waonyeshe time frame ya kutekeleza hayo.

Kikwete pamoja na mapungufu yake,ni rafiki mzuri wa wazungu hawa na anweza akawa na influence katika kuwashawishi pengine kuliko hata waziri wa mambo ya nje.

Nakwambia hivi sasa hawezi tena kufanya makosa kama haya.
 
Baada ya nchi nyingine wahisani kuungana na Marekani katika kusitisha misaada,naona itakuwa vigumu sana kwa serikali kupuuza jambo hili licha ya kauli za kujitutumua kuwa tunaweza ku-manage kuendesha nchi bila misaada ya wahisani.

Huenda tunaweza lakini tatizo ni kuwa hatukujipanga na tunahitaji muda kujipanga na muda huo kwa sasa haupo kwani tumeshachelewa.

Hivyo,kwa mtazamo wangu,naishauri serikali kuunda kitu kinachoitwa "Goverment Negotiating Team" kwenda kuonana na nchi wahisani kutafuta suluhu ya mgogoro huu.

Kwa sasa tunaweza kuweka msimamo wa kuachana na bwana wakubwa hawa ila wakati utafika tutajikuta tunakwama na tutapaswa kuwarudia kwa aibu unless serikali ichukue hatua za dharura kupunguza matumizi yasiyo ya lazima kuanzia Ikulu mpaka kwenye ofisi ya Mtendaji wa Mtaa.

Hata hivyo,tukumbuke tuna changamoto za kuandaa uchaguzi wa serikali za mitaa,deni la Taifa,elimu bure,kura ya maoni au kuanza upya kwa Bunge la katiba, fedha za kuendesha Bunge la Bajeti,n.k.Tusipokuwa makini tutajikuta hakuna miradi ya maendeleo inayofanyika au kukamilika.

Timu hiyo ya Wataalamu inaweza kuundwa na watu wafuatao;

1.Raisi Mstaafu Kikwete(mwenyekiti wa jopo)

2.Waziri wa Mambo ya Nje

3.Waziri wa Fedha

4.Katibu Mkuu Wizara ya Fedha

5.Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi

6.Waziri wa Sheria

7.Katibu Mkuu Wizara ya Sheria

Raisi Mstaafu Kikwete anafaa zaidi kwasababu amekuwa karibu sana na wazungu hawa katika kipindi cha uongozi wake hivyo anaweza kuwa na msaada zaidi katika jambo hili kama mwenyekiti wa Jopo.

Hao wengine kwa nafasi zao wanahusika moja kwa moja na swala hili.

Waziri wa Sheria na Katibu wake Mkuu wanaweza kuhusishwa katika Timu kama watu watakaohusika kutoa ufafanuzi(commitment) ya serikali kuhusu kupitia upya Sheria ya Makosa ya Mtandao.

Watu wengine wanaoweza kuwepo kwenye Timu hii ni mwakilishi wa serikali ya Zanzibar na mwakilishi wa vyama vya siasa ambao watakuwa na wajibu wa kueleza commitment ya serikali ya Zanzibar na Vyama vya Siasa katika kumaliza mgogoro wa uchaguzi wa Zanzibar.

Mwisho,jambo hili liwe funzo katika kuendesha chaguzi zetu na zaidi iwe funzo la sisi kujitegemea kwa kubuni na kusimamia vyanzo vyetu vya mapato na kuachana kabisa na mawazo ya kutegemea wahisani.

Salary Slip, wazo lako si baya. Hata hivyo naomba ujue na wanabodi wengine. Vita hapa ni Kati ya USA &Co dhidi ya China & Co. Marekani imeshtuka nguvu inayotumia China kumvuta Magufuli kupitia ushauri wa baadhi ya watu wakiongozwa na Waziri Kitwanga. Na kwa wakati huo ukumbuke hapa Tanzania Marekani ilikuwa na interest na JK kwa urithi wa Bernard Membe. Hivyo ujio wa Magufuli ni pigo kwa Marekani. Hawamjui hivyo hata hiyo "negotiations team" haiwezi kufanikiwa maana Magufuli ameshaonyesha side yake. Ni China & Co. Kwa maoni yangu Magufuli akomae na marafiki wa Tanzania hatimaye tutavuka maana USA inatuhitaji kuliko tunavyomhitaji.
 
Ngoja watu waje wakushambulie kumpendekeza JK , propadanga machinery ya nchi ilishasema hafai hata kama watu wanajua anafaa!
Mimi ni mmojawapo ya wale wasiomkubali JK. Huu mgogoro ulioleteleza kufutiwa ufadhili wa MCC2 - ubakaji wa demokrasia ZnZ - JK ameshiriki kikamilifu kuuchochea kwa hivyo anapoteza uhalali sio tu wa kuwa mwenyekiti wa jopo pendekezwa, bali pia kuwa mjumbe. JK amechochea mgogoro wa kisiasa wa ZnZ kwa namna mbili: kwanza aliingia madarakani (2005) akikiri kuwepo mpasuko na akajiapiza kuwa hilo lingekuwa mojawapo ya vipaumbele vyake. Lakini tumeshuhudia akishindwa kabisa kuleta suluhisho katika kipindi cha utawala wake wa miaka kumi. Pili, pamoja na kutoleta suluhisho, amechochea kama sio kupika ubakaji wa demokrasia uliofanywa na CCM katika uchaguzi wa Oct 2015 na kupoteza hata kile kidogo (SUK) ambacho jitihada na busara za Maalim Seif na Amani Karume zilikuwa zimekileta. Ni mchochezi, ni mnafiki, ni mzandiki, ni nyoka anayekug'ata huku akikuchekea. HAFAI KABISA.
 
Ni kweli ndio maana nasema waonyeshe commitment na vile vile waonyeshe time frame ya kutekeleza hayo.

Kikwete pamoja na mapungufu yake,ni rafiki mzuri wa wazungu hawa na anweza akawa na influence katika kuwashawishi pengine kuliko hata waziri wa mambo ya nje.

Nakwambia hivi sasa hawezi tena kufanya makosa kama haya.
Mkuu Tanzania ni mabingwa wa longo longo. Kikwete anajulikana kwa usanii. CCM inajulikana kwa ubabe na ukandamizaji. Hakuna negotiator hapo. Hao wote wanajulikana ni matapeli.
 
Back
Top Bottom