Ushauri kwa chama cha CHADEMA!

Ushauri kwa chama cha CHADEMA!

kayumba

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2010
Posts
653
Reaction score
73
Kulingana na kesi inayowakabili viongozi wengi na wabunge wa CHADEMA, kule Arusha ni busara kuanza kujiandaa. Wajiandae kwa matokeo ya aina zote; moja ni endapo watashinda kesi na pili ni endapo watashindwa kesi.

Ushauri wangu ni endapo watashindwa, manake pale kutakuwepo na vifungo! Chama kijiandae na hiyo scinario ya pili ili kisijekushutukizwa. Kitendo cha kuongeza idadi ya mashitaka ni kuonyesha nia ya serikali katika hiyo kesi!

Nawakilisha!
 
Ni wabishi hao,wana wanasheriaa kama mchanga vile haendi mtu gerezani,...ila kama ulivosema pia,ni vyema kujiandaa kwa yote
 
hii kesi iataendele a hadi 2016, na lengo ni kuwapotezea muda kadiri inavyowezekana; tena wasipokuwa makini na haya maandamano ya nchi nzima, watakua na kesi zaidi ya 5 pembe tofauti za nchi na kuwafanya karibia kila wiki wawe mahakamani kusikiliza mashauri yasiyoisha.
 
Chadema wamejipanga, wapo makini na wanaelewa wanachokifanya, kesi nyingi ni kuonyesha jinsi walivyo fanikiwa na kila chama kinajaribu kuwarudisha nyuma. Chadema songa mbele.
 
Ukombozi huwa hauletwi kwenye kisahani unapiganiwa kama unaogopa kifungo kaa nyumbani ulee wajukuu, angalia Mandela, Tsvangrai, na Odinga

Morgan_Tsvangirai_after_beating_200px.jpg
images
images


Leo Tsvangai na Odinga wanafunguliwa milango ya magari yao.

images
images
 
Nasoma sheria kwa makini saaana sasa, hivi karibuni nitakuwa Arusha kuwatetea CDM ninayoipenda. Nitajitolea, sitaki kulipwa hata senti. Hafungwi mtu. Duniani kote kama hamjui, uhuru wa pili (badala ya ule wa 1961) ndiyo mgumu kuliko wote kuupigania. Kesi za kutengeneza hazifungi mtu. Ni fabrications, hakuna kitu. Hata hivyo tuko tayari kwa lolote, ushauri wako ni mzuri ...............
 
hamna kesi ya kujibu pale, ni upuuzi mtupu na njia ya kuwalaghai wananchi ambao wameshafunguka macho kwamba cdm wana makosa... Just stupid and idiotic strategies, nadhani ccm na viongozi wa chama na serikali wamelogwa na aliyewaloga kafa sijui nani atawaagua, wanatumia mbinu za kitoto na za kijinga mno hata mtoto wa darasa la kwanza huwezi kumdanganya kwa hizo strategy zao... They simply need an overhaul otherwise it wont work for them...
 
Back
Top Bottom