Duh, kwa uandishi huu nashawishika kuhoji elimu yako.
Nikirudi kwenye mada...mambo ya kibenki mara nyingi wanajali sana vigezo na taratibu tofauti na taasisi nyingine za mitaani kwetu, kwa mfano mtiririko wako wa mapato/kuweka na kutoa, urasmi wa biashara/shughuli unazofanya, yaani leseni, vibali vya taasisi husika kama ni mzalishaji wa bidhaa fulani n.k.
Kurahisisha mambo ni vizuri ukafika kwenye benki husika, mojawapo kati ya ulizozitaja hapo juu, nina uhakika utapata taarifa zote unazohitaji.