MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 10,213
- 22,278
Nawasalimu kwa jina la Chama Cha Mapinduzi.
Bila kupoteza muda niende kwenye mada. Binafsi nimeona kuna haja ya vijana wenzetu wa CHADEMA kuandaliwa semina ya dharura ili kuwaondoa na huu mkwamo mbaya wa kisiasa uliowakumba. Kwa muda mrefu sasa vijana wa CHADEMA wamekosa muelekeo wa wapi pa kwenda na nini cha kusimamia. Hawajui washike lipi. Imefikia hatua mtu anayejiita Kigogo kawa mshauri wa BAVICHA katika mwelekeo wa kuwavuruga. Kwa kweli vijana wanahitaji msaada wa dharura.
Je hili tatizo lilianzia wapi? Tatizo la hawa vijana kukosa mwelekeo lilianzia toka siku walipoamua kumkabidhi akili zao mwenyekiti wa kudumu Sultani Mbowe. Toka hiyo siku wamekuwa wakifuata fikra zote za mwenyekiti. Pengine hawakujua kwamba Mbowe ni binadamu hawezi kudumu milele kwahiyo ilipaswa na wao watumie akili zao badala ya kumkabidhi Mbowe azitumie kwa niaba yao. Kwa sasa tatizo ni kubwa baada ya Mbowe kuwa gerezani kama mahabusu kwa muda mrefu. Kwa huu muda ambao tunasubiri Mbowe amalize kesi yake na kurudi mtaani na akili alizokabidhiwa na vijana nimeona bora vijana wapate semina ya dharura.
Mwanachama maarufu ndani ya CCM Komredi Lemutuz atafaa sana kutoa semina hiyo kwa kushirikiana na manguli wengine wa siasa kama ndugu Polepole. CCM wachukulie ni jambo la kizalendo ili kuweka sawa mzani wa demokrasia. Ni jambo la kusikitisha kuona chama pinzani kinakufa kirahisi. Uwepo wao unachangamsha.
Bila kupoteza muda niende kwenye mada. Binafsi nimeona kuna haja ya vijana wenzetu wa CHADEMA kuandaliwa semina ya dharura ili kuwaondoa na huu mkwamo mbaya wa kisiasa uliowakumba. Kwa muda mrefu sasa vijana wa CHADEMA wamekosa muelekeo wa wapi pa kwenda na nini cha kusimamia. Hawajui washike lipi. Imefikia hatua mtu anayejiita Kigogo kawa mshauri wa BAVICHA katika mwelekeo wa kuwavuruga. Kwa kweli vijana wanahitaji msaada wa dharura.
Je hili tatizo lilianzia wapi? Tatizo la hawa vijana kukosa mwelekeo lilianzia toka siku walipoamua kumkabidhi akili zao mwenyekiti wa kudumu Sultani Mbowe. Toka hiyo siku wamekuwa wakifuata fikra zote za mwenyekiti. Pengine hawakujua kwamba Mbowe ni binadamu hawezi kudumu milele kwahiyo ilipaswa na wao watumie akili zao badala ya kumkabidhi Mbowe azitumie kwa niaba yao. Kwa sasa tatizo ni kubwa baada ya Mbowe kuwa gerezani kama mahabusu kwa muda mrefu. Kwa huu muda ambao tunasubiri Mbowe amalize kesi yake na kurudi mtaani na akili alizokabidhiwa na vijana nimeona bora vijana wapate semina ya dharura.
Mwanachama maarufu ndani ya CCM Komredi Lemutuz atafaa sana kutoa semina hiyo kwa kushirikiana na manguli wengine wa siasa kama ndugu Polepole. CCM wachukulie ni jambo la kizalendo ili kuweka sawa mzani wa demokrasia. Ni jambo la kusikitisha kuona chama pinzani kinakufa kirahisi. Uwepo wao unachangamsha.