Ushairi: KITASA

Ushairi: KITASA

Fikra Angavu

JF-Expert Member
Joined
Jul 14, 2013
Posts
301
Reaction score
106
KITASA

Kitasa changu kibovu, chanitesa mwenzenu.
Chaniacha na makovu, tafuteni cha kwenu.
Kucha kutwa kichovu, mwakichokonoa chenu?
Basi vyenu viwe vyenu, na changu niachieni.


Choko choko ni hazishi, mpaka kimepwaya.
Hata Ngo! ngo! hambishi, pasi soni wala haya!
Usiku ni hatarishi, tena mrefu naugwaya.
Basi vyenu viwe vyenu, na changu niachieni.

Sie tupendao chongo, tunaitaga kengeza.
Nisiwe tu muongo, mwenyewe chanipendeza.
Nisiwe tu muongo, werevu mwakilegeza.
Basi vyenu viwe vyenu, na changu niachieni.

Washenzi mwaomba maji, na mengine mna mwaga.
Upole si ukosaji, mnilalie kama chaga.
Jama hii ni dibaji, mjue kwa babu Tanga.
Basi vyenu viwe vyenu, na changu niachieni.
 
Hicho chako usemacho, ni kitasa kinanesa,
hicho hakina mwenecho,bora komeo ya isa
kinapenda korokocho,hakina hiyana kabisa,
Kitasa siyo komeo, si muhali kuchangiwa.
 
Dhana halisi ya mlango, kila mtu aweze pita,
Asikunje hata mgongo, ndani aweze kukita,
Alisema manifongo, ingia usijejuta,
Kuweka kitasa ni ubinafsi, acha mlango wazi majirani tuingie.

Wewe pia meingia, wengi umewakamua,
Mlango haukuzuia, ndani ulipekenyua,
Juuu wapumulia, leo walia ka mvua,
Boko ala wenziwe, lakini nae aliwa

Kama wewe umepita, acha na sisi tuonje,
Kwa hiari sio vita, ingia na utoke nje,
Using'ang'anie kuta, ubabe kama Sizonje,
Ingia ndani, maliza halafu toka nje na wenzio waweze kuingia
 
Dhana halisi ya mlango, kila mtu aweze pita,
Asikunje hata mgongo, ndani aweze kukita,
Alisema manifongo, ingia usijejuta,
Kuweka kitasa ni ubinafsi, acha mlango wazi majirani tuingie.

Wewe pia meingia, wengi umewakamua,
Mlango haukuzuia, ndani ulipekenyua,
Juuu wapumulia, leo walia ka mvua,
Boko ala wenziwe, lakini nae aliwa

Kama wewe umepita, acha na sisi tuonje,
Kwa hiari sio vita, ingia na utoke nje,
Using'ang'anie kuta, ubabe kama Sizonje,
Ingia ndani, maliza halafu toka nje na wenzio waweze kuingia
[emoji23][emoji23][emoji23] daah hahah
 
Kitasa siyo anasa, kukiweka mlangoni,
kazi yake si kunasa,jamaa na majirani,
Na wala siyo mlinzi, kuzuia hayawani,
acha kifunguliwe!
 
Rudi ewe la azizi, chonde mimi nakuomba,
Niepushe na uchizi, zako huba zanisomba,
Nalilia lako penzi, takusaka hata pemba,
Ukhuty chonde rudi, sikie kilio changu
Hahah... Daah safi sana..
 
Back
Top Bottom