Nawasalimia Wakuu!
Nimelazimika kuandika haya kutokana na ukweli kuwa kazi kubwa imefanyika ndani CDM ukilinganisha tulikotoka na tuliko. Pamoja na kazi hiyo tulioifanya na zinazoendelea kufanyika katika kuhakikisha CDM inachukua madaraka 2015 inanisikitisha kugundua kuwa watanzania wengi wameathirika na uwepo wa chama kimoja kwa miaka mingi, hata wale wadogo ambao walikuta mfumo mpya wamepokea athari kutoka kwa wakubwa zao.
Athari kubwa ni kuwa waoga wa kushiriki mambo ya siasa na wakiwa sio waoga wanakuwa passive wasio na msimamo, na wakiwa na msimamo basi ujue msimamo huo ni hewa! Sio siri CDM inapendwa na kukubalika haswaaa na vijana, ila ni mashabiki wangapi wa CDM ni wanachama halali wenye kadi? wanashiriki shughuli za kichama? wanahuzuria mikutano na wanachama hai? wangapi wamewahi kushiriki maandamano?
Utakuta mtu mnazi haswaa wa CDM ila siku ya maandamano anajibanza ila moyoni anaomba watu wafurike, na wakwanza kuangalia ITV kuona ilikuwaje?! kweli tutafika!?
2015 hiyooooo inakaribia, kwa mwendo huu hatutofika, tubadilike kwa kuanzia humu JF, jiulize una kadi ya CDM, tuache woga, mtu unamkuta online ni CDM damu ila ofisini akiulizwa we chama gani, anagwaya gwaya maana kusema GAMBA roho inamsuta, kusema yeye CDM anaogopa.
Anza kushiriki shughuli za chama mapema utapata nafasi ya kujua utendaji wa watu kiuhalisia, ili 2015 ukimpitisha mgombea unamjua kiundani. Inasikitisha sana kijana umemaliza chuo au six afu unakaa nyumbani unalia ajira hakuna, jiunge na chama wewe, utapata network na conections za kutokea, na hata exposure ya kimawazo.
Ni mimi
Mwanachama hai, mwenye kadi nashabiki halali wa CDM.
Nimelazimika kuandika haya kutokana na ukweli kuwa kazi kubwa imefanyika ndani CDM ukilinganisha tulikotoka na tuliko. Pamoja na kazi hiyo tulioifanya na zinazoendelea kufanyika katika kuhakikisha CDM inachukua madaraka 2015 inanisikitisha kugundua kuwa watanzania wengi wameathirika na uwepo wa chama kimoja kwa miaka mingi, hata wale wadogo ambao walikuta mfumo mpya wamepokea athari kutoka kwa wakubwa zao.
Athari kubwa ni kuwa waoga wa kushiriki mambo ya siasa na wakiwa sio waoga wanakuwa passive wasio na msimamo, na wakiwa na msimamo basi ujue msimamo huo ni hewa! Sio siri CDM inapendwa na kukubalika haswaaa na vijana, ila ni mashabiki wangapi wa CDM ni wanachama halali wenye kadi? wanashiriki shughuli za kichama? wanahuzuria mikutano na wanachama hai? wangapi wamewahi kushiriki maandamano?
Utakuta mtu mnazi haswaa wa CDM ila siku ya maandamano anajibanza ila moyoni anaomba watu wafurike, na wakwanza kuangalia ITV kuona ilikuwaje?! kweli tutafika!?
2015 hiyooooo inakaribia, kwa mwendo huu hatutofika, tubadilike kwa kuanzia humu JF, jiulize una kadi ya CDM, tuache woga, mtu unamkuta online ni CDM damu ila ofisini akiulizwa we chama gani, anagwaya gwaya maana kusema GAMBA roho inamsuta, kusema yeye CDM anaogopa.
Anza kushiriki shughuli za chama mapema utapata nafasi ya kujua utendaji wa watu kiuhalisia, ili 2015 ukimpitisha mgombea unamjua kiundani. Inasikitisha sana kijana umemaliza chuo au six afu unakaa nyumbani unalia ajira hakuna, jiunge na chama wewe, utapata network na conections za kutokea, na hata exposure ya kimawazo.
Ni mimi
Mwanachama hai, mwenye kadi nashabiki halali wa CDM.