Usaili wa T. R. A ulivurugwa

Usaili wa T. R. A ulivurugwa

NJONJOBWINO

New Member
Joined
Aug 27, 2021
Posts
1
Reaction score
1
Eid Mubarack ndugu zangu watanzania na Viongozi wetu mbalimbali mliopewa mamlaka ya kusimamia haki katika Taifa letu,nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Leo naomba niongee na Viongozi wetu hawa wakiongozwa chini ya mh @samia_suluhu_hassan Mh Rais na waziri mwenye dhamana ya ajira.@tratanzania Ndugu viongozi wetu mlio pewa dhamana naomba niwaeleze kilichotokea kwenye uratibu wa hizi kazi zilizotangazwa na Tra,kilichotokea kada ya TMO kinaumiza na kutuachia vidonda sisi vijana tunaendelea kutafuta kazi katika Taifa hili kwa mifumo mliotuwekea.

Mchakato wa ajira za Tra kwenye maombi mpaka kuitwa kwenye usahili haukuwa na tatizo ila Tatizo limevurugwa hapa kwenye usahili hili nalo ni jipu linalopaswa litumbuliwe, ila mimi naomba nitumie 4R za Mh Rais kueleza tuhuma hizi nzito.

Waheshimiwa Viongozi Mtihani wa TRA kada ya Tax management officer 2 ulivuja asilimia 90% na huu ndio ushahidi nao uwasilisha kwenu ili muone namna iliyo bora zaidi kuweza kutatua ili janga.

(1)Mtihani wa Tra kada ya TMO ulifanyika wakati tofauti,Dodoma,Arusha,Dar es salam

(2)Ukaguzi uliofanyika ulikuwa ni wa ubabaishaji kilikaguliwa cheti kimoja,kitambulisho na Email baada ya hapo uliruhusiwa kuingia,Dodoma waliweka mabegi mbele,Arusha walirusiwa kila mtu kukaa na vifaa vyake chini ya meza.

(3)Wasimamizi walikua wachache kwenye chumba cha mtihani kiasi kwamba hall la watu elfu mbili kasoro lilisimamiwa na maafisa watatu Arusha kwa Dodoma hivyo hivyo maafisa wa husimamizi walikuwa wachache.

(4)Muda mfupi baada ya Mtihani kumalizika ulizagaa kwa njia ya whastapp kitu kinacho ashilia Mtihani huu ulivuja na hapa naambatanisha ushahidi wote ili mfanye uchunguzi zaidi.

(5) Utaratibu wa kusign in na kusahini out Arusha haukutumika kabisa kwa Dodoma kuna baadhi hawakusign out

Mwisho tunaomba hizi tuhuma zifanyiwe uchunguzi , ukwelli ukibainika Mchakato wa usahili urudiwe upya na ningependekeza hizi ajira zirudishwe utumishi maana Tra usimamizi hata wa watu kuchukua mizigo yao umewashinda,watu wamepoteza Vyeti,Simu,mabegi,Computer n.k kwa usimamizi wao mbovu.

View: https://www.instagram.com/p/DH4DdZNoBdO/?igsh=NzExZjkzODhpbXpj
 
Hivi customs officer ii nayo ilivuja?
 
Eid Mubarack ndugu zangu watanzania na Viongozi wetu mbalimbali mliopewa mamlaka ya kusimamia haki katika Taifa letu,nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Leo naomba niongee na Viongozi wetu hawa wakiongozwa chini ya mh @samia_suluhu_hassan Mh Rais na waziri mwenye dhamana ya ajira.@tratanzania Ndugu viongozi wetu mlio pewa dhamana naomba niwaeleze kilichotokea kwenye uratibu wa hizi kazi zilizotangazwa na Tra,kilichotokea kada ya TMO kinaumiza na kutuachia vidonda sisi vijana tunaendelea kutafuta kazi katika Taifa hili kwa mifumo mliotuwekea.

Mchakato wa ajira za Tra kwenye maombi mpaka kuitwa kwenye usahili haukuwa na tatizo ila Tatizo limevurugwa hapa kwenye usahili hili nalo ni jipu linalopaswa litumbuliwe, ila mimi naomba nitumie 4R za Mh Rais kueleza tuhuma hizi nzito.

Waheshimiwa Viongozi Mtihani wa TRA kada ya Tax management officer 2 ulivuja asilimia 90% na huu ndio ushahidi nao uwasilisha kwenu ili muone namna iliyo bora zaidi kuweza kutatua ili janga.

(1)Mtihani wa Tra kada ya TMO ulifanyika wakati tofauti,Dodoma,Arusha,Dar es salam

(2)Ukaguzi uliofanyika ulikuwa ni wa ubabaishaji kilikaguliwa cheti kimoja,kitambulisho na Email baada ya hapo uliruhusiwa kuingia,Dodoma waliweka mabegi mbele,Arusha walirusiwa kila mtu kukaa na vifaa vyake chini ya meza.

(3)Wasimamizi walikua wachache kwenye chumba cha mtihani kiasi kwamba hall la watu elfu mbili kasoro lilisimamiwa na maafisa watatu Arusha kwa Dodoma hivyo hivyo maafisa wa husimamizi walikuwa wachache.

(4)Muda mfupi baada ya Mtihani kumalizika ulizagaa kwa njia ya whastapp kitu kinacho ashilia Mtihani huu ulivuja na hapa naambatanisha ushahidi wote ili mfanye uchunguzi zaidi.

(5) Utaratibu wa kusign in na kusahini out Arusha haukutumika kabisa kwa Dodoma kuna baadhi hawakusign out

Mwisho tunaomba hizi tuhuma zifanyiwe uchunguzi , ukwelli ukibainika Mchakato wa usahili urudiwe upya na ningependekeza hizi ajira zirudishwe utumishi maana Tra usimamizi hata wa watu kuchukua mizigo yao umewashinda,watu wamepoteza Vyeti,Simu,mabegi,Computer n.k kwa usimamizi wao mbovu.

View: https://www.instagram.com/p/DH4DdZNoBdO/?igsh=NzExZjkzODhpbXpj

Dosari ilianza walipoita watu 6,000 kwa usahili kwenye nafasi 30 tu za ajira.
 
Kazi kujaza nyuzi za kuhusu tra, si ungecomment tu kwenye nyuzi zingine zenye topic kama hii?!! , hakukua na ulazima wa kufungua mpya.

kubali tu umeshindwa, kusambaziwa majibu ya mtihani baada ya interview haina mana kua pepa ilivuja, kuna watu inawezekana waliingia na simu ( hii hata utumishi inatokea sio kwa tra peke yake) wakapiga picha na wakatafuta majibu chat gpt wakayatuma online mda huo huo.

Kufanyika masaa tofauti sio sababu ya wengine kupata majibu ukizingatia nature ya mtihani wenyewe.

Hata wakifuta wakaleta mwingine hautafaulu vijana acheni ulalamishi lazima wengine mkose ili wengine wapate.
 
Walioiba mtihani kupata kazi, mnataka wafaulu mwape jukumu la kwenda kukusanya Kodi za wananchi?
 
Mimi naona watu wamejitokeza wengi mno na kuleta tafrani kutokana na manufaa ya huko tiaraei! Ingelikuwa kuna manufaa yanayokaribiana na taasisi nyingine za serikali nahakika hata idadi ya waombaji ingekuwa si kubwa sanaa. Hapo amini kwamba kuna watumishi wa umma walikuwepo pia, achilia mbali wale wa private wenye kulipwa mishahara mizuri tuu. Shida ni kwamba hapo ni kichaka! Duu, aliyeleta sera ya kuanzisha hii Taasisi alikuwa na nia njema, lakini sasa kimegeuka kuwa kama kichaka cha watu kufichana!
 
Back
Top Bottom