Usafirishaji wa mizigo bandarini

Usafirishaji wa mizigo bandarini

Kichakoro

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2008
Posts
3,429
Reaction score
6,393
Ndugu wanaJF,

Kumekuwa na kelele nyingi sana kwamba "dereva wa Bus hawafahamu abiria wote". Kwamba wasafirishaji wa mizigo ya meli hawafahamu shehena walizobeba. Sio Kweli

Tuanze na utaratibu wa Percels: Unapopeleka percel DHL, EXPRESS MAIL etc lazima useme kilichopo ili kikipotea waweze kujua namna ya kukulipa.

Utaratibu wa Meli: unapotaka kukodisha container lazima useme unakwenda kupakia mzigo wapi ni nini kitakachokuwepo kwenye container n.k wanaoseal container na shipping line/agency na kuanza mchakato wa kuandika Bill of Ladding inayoitemise kila kilichopo kwenye container.

Wakati wa ufungaji wa container government agencies including usalama wanakuwepo kuhakiki ikiwa ni pamoja na kufanya container scanning pale wanapokua na wasiwasi kilichopo ndani ya container ni material ambayo hairuhusiwi kusafirishwa katika meli za kawaida na bila kibali maalum. Mfano explosives, vifaa vya kijeshi n.k

Sasa Basi: Je Kinana shipping line walizingatia taratibu zote za usafirishaji wa mizigo nje ya nchi? Kama ndio walishindwaje kubaini mzigo uliokuwepo?

Kama kinana shiping agency hawakufuata taratibu kwa nini hawajafungiwa? TUAMINI WALIPIGWA FINE YA UZEMBE

Je mbona suala hilo limejirudia tena? same mzigo same destination?


HII NDIO SABABU YA MSINGI KINANA KUENDELEA KUHUSUSHWA NA BIASHARA HARAMU YA UJANGILI.
 
Ukikutwa na Bangi bilicanas hatuwezi kwenda kumkamata Mbowe, umeeleza vizuri taratibu lakin umesahau au hujui kuwa kwenye Magendo bill of Lading huwa haziorodheshi biashara haramu kwa hiyo hutumia mbinu mfanoKama ndani ya magogo wanaweka bangi basi bill of lading haioneshi bangi bali itaonesha magogo na mwenye meli hashiriki kwenye ukaguzi kama vile wakati wa Scanning bali anashiriki ku Observe wakati wa ufungaji mzigo uliokwisha pekuliwa kwa hiyo kama Gogo ndani lina bangi hawezi kujua, Kinana anawanyima usingizi sana Dozi zimeanza kwenye Uchaguzi wa mabaraza ya Tume ya Katiba mpya mwisho wake October 2015
 
Jitihada zenu za kumtetea kinana kwamba hausiki na ivory trade ni bure! Kwani kwa watanzania kinana ni jangili wa tembo wao, huo ndio ukweli na wananchi ndicho wanachokisema. Mteteeni kwa kila neno lakini mjue wananchi wamepoteza imani na ccm yenu kwa ufisadi wa raslimali za nchi yetu.tunawachukia sana serikali ya ccm kwani ndio chanzo cha maisha yet kuwa magumu. 'masikini hana cha kupoteza"
 
Mimi nashangaa sana jinsi wizi unavyobainika kwenye baadhi ya wizara na wahusika kutajwa hadharani lakini serikali inawafumbia macho na kuwakinga dhidi ya ushetani wanaoufanya wengi wa vigogo waliopo ndani ya serikali ya CCM, Akina Mramba na wenzie kufikishwa kwao mahakamani nahisi ni baada ya makubaliano yao na uongozi uliokuwepo ili serikali tawala ionekane kana kwamba inashughulikia ipasavyo vitendo vya ufisadi kumbe ni wizi mtupu na huenda baada ya zile kesi haohao watuhumiwa walilipwa kiasi kadhaa kutokana na kuchafuliwa majina yao kwenye zile kesi. hii ndio Tanzania ambayo ukibahatika kuwa kiongozi serikalini unafanya unayotaka bila kubugudhiwa na kiumbe yeyote.
 
Tuanze na utaratibu wa Percels: Unapopeleka percel DHL, EXPRESS MAIL etc lazima useme kilichopo ili kikipotea waweze kujua namna ya kukulipa.
Si kweli.

Sio kila kinachotumwa kikipotea kinalipwa, inategemea kama ulinunua insurance na uli declare value na wana policy hiyo ya kulipa. Kwa hiyo hawawezi kukulazimisha kusema kilichomo kwa sababu tu eti "ili kikipotea tukulipe." Mimi sitaki mnilipe, kikipotea kimepotea, hapo vipi bado mnanilazimisha niseme nimebeba nini?

Utaratibu wa Meli: unapotaka kukodisha container lazima useme unakwenda kupakia mzigo wapi ni nini kitakachokuwepo
Unapotaka kukodisha container? Vipi ukiwa na container lako nyumbani kwako? Una uwezo wa ku smuggle matani na matani ya pembe za ndovu utashindwa ku procure kikotena ambacho Mchaga anacho anauzia duka la dawa za mbu?

"Lazima useme" haina maana kwamba utasema ukweli! Nani atasema "Jamani nimebeba meno ya tembo"!

Wakati wa ufungaji wa container government agencies including usalama wanakuwepo kuhakiki ikiwa ni pamoja na kufanya container scanning pale wanapokua na wasiwasi kilichopo ndani ya container ni material ambayo hairuhusiwi kusafirishwa katika meli za kawaida na bila kibali maalum. Mfano explosives, vifaa vya kijeshi n.k
Kwa hiyo kama hawana wasiwasi basi hawaji hao usalama wala hakuna cha scanning kitakachofanyika, sio? Manake wana scan wanapokuwa na wasiwasi! Watu wengine bana....hahahaaa....

"Wakati wa ufungaji wa container government agencies wanakuwepo..." Kwa hiyo ukifunga container la kahawa kiwandani kwako hao Usalama watajua Bwana Kichakoro leo anafunga container twende tuka show up kwake ku scan makontena yake?! Scanning? Bongo... what? Nini Bongo, hata United Kingdom of Great Britain hakuna kitu kama hicho!

Hueleweki, na unapoeleweka huna ukweli, to put it very mildly.
 
Si kweli.

Sio kila kinachotumwa kikipotea kinalipwa, inategemea kama ulinunua insurance na uli declare value na wana policy hiyo ya kulipa. Kwa hiyo hawawezi kukulazimisha kusema kilichomo kwa sababu tu eti "ili kikipotea tukulipe." Mimi sitaki mnilipe, kikipotea kimepotea, hapo vipi bado mnanilazimisha niseme nimebeba nini?

Unapotaka kukodisha container? Vipi ukiwa na container lako nyumbani kwako? Una uwezo wa ku smuggle matani na matani ya pembe za ndovu utashindwa ku procure kikotena ambacho Mchaga anacho anauzia duka la dawa za mbu?

"Lazima useme" haina maana kwamba utasema ukweli! Nani atasema "Jamani nimebeba meno ya tembo"!

Kwa hiyo kama hawana wasiwasi basi hawaji hao usalama wala hakuna cha scanning kitakachofanyika, sio? Manake wana scan wanapokuwa na wasiwasi! Watu wengine bana....hahahaaa....

"Wakati wa ufungaji wa container government agencies wanakuwepo..." Kwa hiyo ukifunga container la kahawa kiwandani kwako hao Usalama watajua Bwana Kichakoro leo anafunga container twende tuka show up kwake ku scan makontena yake?! Scanning? Bongo... what? Nini Bongo, hata United Kingdom of Great Britain hakuna kitu kama hicho!

Hueleweki, na unapoeleweka huna ukweli, to put it very mildly.


Hoji kama msomi na sio wanywa chibuku.

International business zina taratibu zake sio unafikiri ni sawa na kusafirisha mahindi kutoka nyumbani kwako kupeleka kariakoo.
 
nishapakia makontena mengi tu UK truck inakuja na driver peke yake.....driver anafungua then anaenda kukaa ndani ya cabin or nearer coffee shop....napakia nikimaliza anakuja kufunga na NEW SEAL driver hahusiki na ukaguzi.....kwenye BILL OF LADING naorodhesha whats inside nikiorodhesha tofauti na vilivyopo inakula kwako bandarini....hakuna mwanausalama wala mjumbe.....container halifunguliwi hadi BONGO infront of consignee mimi au niliemuandika kwenye BL.....i guess wanalifanyia scanning bandarini kabla ya kupakia melini....
 
Hoji kama msomi na sio wanywa chibuku.

International business zina taratibu zake sio unafikiri ni sawa na kusafirisha mahindi kutoka nyumbani kwako kupeleka kariakoo.
Sawa nakunywa chibuku, lakini nimekataa kudanganywa na ambae hanywi chibuku.

Sio kweli kwamba kila parcel shipment italipwa kama ikipotea.

Sio kweli kwamba Usalama wanakuja nyumbani kwako au popote unapofungia container eti kuli scan.

Na sio kweli kwamba unapoambiwa sema kilichomo ni lazima utasema, muuza ndovu hasemi "nimebeba pembe"!

Kwa hiyo basi, conclusion yeyote utakayojenga based on those fallacies na yenyewe lazima itakuwa fyongo, na udanganya mchana mchana kuhusu vitu common kama ku ship with DHL, sasa sijui nani anakunywa chibuku nyingi zaidi, mimi wewe?
 
...kwenye BILL OF LADING naorodhesha whats inside nikiorodhesha tofauti na vilivyopo inakula kwako bandarini....hakuna mwanausalama wala mjumbe.....container halifunguliwi hadi BONGO infront of consignee mimi au niliemuandika kwenye BL.....i guess wanalifanyia scanning bandarini kabla ya kupakia melini....
Sio kweli kwamba ukiorodhesha ambacho si kweli basi "inakula kwako bandarini," makontena ya miharadati na mapembe ya ndovu na ma weapons na ma cocaine yasingekuwa yanakatisha bandarini kwa sababu kwenye bill of lading hakuna anaeulizwa "humu kwenye container kuna nini?... akajibu "pembe za ndovu"!

Halafu unaongelea shipping ya UK kuja bongo, ambayo ni tofauti na shipping ya Bongo kupeleka mizigo nje ya Bongo, utachanganya vitu. Kinana alikuwa anasafirisha meno ya tembo kwenda nje ya Tanzania.
 
Sio kweli kwamba ukiorodhesha ambacho si kweli basi "inakula kwako bandarini," makontena ya miharadati na mapembe ya ndovu na ma weapons na ma cocaine yasingekuwa yanakatisha bandarini kwa sababu kwenye bill of lading hakuna anaeulizwa "humu kwenye container kuna nini?... akajibu "pembe za ndovu"!

Halafu unaongelea shipping ya UK kuja bongo, ambayo ni tofauti na shipping ya Bongo kupeleka mizigo nje ya Bongo, utachanganya vitu. Kinana alikuwa anasafirisha meno ya tembo kwenda nje ya Tanzania.

u must be joking.......get a 40 feet container with 2 cars and in ur BL declare there is 1 car then u will know what i mean.....

i guess u dont know whay BILL OF LADING IS.......
 
u must be joking.......get a 40 feet container with 2 cars and in ur BL declare there is 1 car then u will know what i mean.....

i guess u dont know whay BILL OF LADING IS.......
Okay sawa, sijui bill of lading maana yake nini, manake ni kitu kikuuubwa na complicated kweli kweli!

Sasa kama huwezi kusema uongo kwenye bill of lading, nambie, pembe za ndovu na bangi na heroine zinasafirishwa vipi kwenye meli? Uta declare kwenye bill of lading "humu ndani nimebeba magunia ya heroine"??? Watu wanasafirisha cargo za contraband kwenye ndege, itakuwa makontena kwenye meli? We vipi? Biashara haramu unazielewa wewe?

Na ni kwa nini ukikamatwa airport na madawa tumboni hawaendi kumkamata agent wa ndege uliyemlipa nauli? Investigations zetu na sheria za logistics zetu na maswali tunayomuuliza Kinana na tuhuma zenyewe ni very tenuous, hatujakusanya evidence za ushiriki wake, kusema "hapa Kinana ulitakiwa ujue kwenye kontena kuna nini."

Kinana atasema ilikuwaje container likakatisha bandarini Dar? Nyinyi si mmelikagua? Nyinyi mna scanner mmeshindwa kujua mimi nitajua?
 
Back
Top Bottom